Taa zenye mwanga mweupe VS mwanga wa yellow

Taa zenye mwanga mweupe VS mwanga wa yellow

lorry ikikutwanga full hamna kitu yani bora uzime😅😅😅na anga likiwa na mbalamwezi pia huoni kitu
Unapigwa mwanga alafu barabara haina mstari wa katikati na ile ya pembeni yaani ni balaa. Bora upigwe mwanga alafu barabara ina mistari ile inakuwa ina rangi flani ya manjano ina-reflect hivyo inakusaidia usitoke nje.
 
Kwa issue ya taa kila mtu na mtazano wakr
Lakin zile taa zenye yellowish ndo nzuri
Nilitoa siku za nyuma niafunga zile nyeupe
Zina fan ndani yake kuongeza ufanisi
Lakin
Muangaza wake ni mzuri giza likiwa kali na ukiwa peke yako road
Ila hazioneshi vizuri kama zile zenyr njano
Ukweli ni kwamba baada ta muda nilizigawa bure kabisa nikarudisha zile zimekuja na gari

Sent from my SM-A125F using JamiiForums mobile app
Zile ni za booster mkuu wa kaya
Ni kagari kangu Corolla xe, kazamani kidogo, hivi naweza funga taa hizi za booster na kupata mwanga wa kutosha maana natesekaga nikiwa road na mie huwa napenda kukatumikisha kwa safari za usiku usiku zisizo za masafa marefu sana
 
Unapigwa mwanga alafu barabara haina mstari wa katikati na ile ya pembeni yaani ni balaa. Bora upigwe mwanga alafu barabara ina mistari ile inakuwa ina rangi flani ya manjano ina-reflect hivyo inakusaidia usitoke nje.
ile inasaidia mno mkuu, hata mimi inaniokoaga
 
Wadau huyu driver wa super feo iliyopata ajali. Kuna mwenye video.clip yake
 
Ni kagari kangu Corolla xe, kazamani kidogo, hivi naweza funga taa hizi za booster na kupata mwanga wa kutosha maana natesekaga nikiwa road na mie huwa napenda kukatumikisha kwa safari za usiku usiku zisizo za masafa marefu sana
Unaweza mkuu unafunga vizuri kabisa tena ukipata booster kubwa na bulb zake utaenjoy.
 
Unaweza mkuu unafunga vizuri kabisa tena ukipata booster kubwa na bulb zake utaenjoy.
Nitabadilisha mkuu siku moja maana ki-corolla changu japo cha zamani lakini bado kinadai kwenye Engine hivyo nitajaribu kuweka
 
Ukitaka kujua ubovu wa taa nyeupe usafiri usiku ukutane na mvua ndio utajua hujui. Ukifika salama mwisho wa safari ninauhakika utaenda kung’oa hizo taa
Utakuwa unatumia taa za urembo za fuso. Unapokwenda kununua bulb nenda kanunue zenye standard na nguvu inayotakiwa.

Mfano mimi zote nilizofunga ni za LED. Na zile za fog nimeweka zenye jicho la lenzi.

Mvua nikipiga mbele naona vizuri tu bila changamoto yoyote. Ninachofanya ni kuwa makini nikiwa kwenye njia ya single lane kama hizi za mkoa nacontrol beam nisiwamulike madereva wengine usoni na kuwaharibia timing.

Cha kufahamu ni standards za hizi balbu. Sio unakwenda tu dukani unajinunulia kama nyanya unafunga kwenye gari nyingi zinakuwa ni za kawaida ila ukiwa unajua standards za taa utajua zipi sahihi.

Kuna tubulb unakuta tunawekwa hadi kwenye bajaji, au fuso kama urembo we unakuja funga kwenye gari sehemu ya fog light kisha unalalamika.

Kuwa makini
 
Kabisaa jana mm nilikuwa road kwa mara ya kwanza na izi taa nyeupe aisee nikasema izi taa ni chaka sanaaa

Yaan nilikiwa nikipishana na malori basi nilikiwa nazima izi taa, zenyewe ni nzuri ukiwa pekee yaan hakuna unae pishana nae weka full light on uta enjoy
Tazama taarifa (specifications) za hizo bulbs kwenye box. Tazama nguvu yake.

Ni sawa ukanunue subwoofer ya aboder halafu ulalamike jirani yako akiwasha home theater yake LG au Sony inafunika ya kwako kwa mziki mzuri.
 
Zile nyeupe zenye fan C6 hazina nguvu kabisa..mimi nilifunga na nilikua na safari siku husika ilibidi niweke za mwanga mweupe lakini ni za halogen ila ni 5000K zipp fresh ndo ninazozitumia hadi leo nikipiga full lazima uombe zipunguzwe..zile za yellowish nimeweka kwenye Fog lights.
But halogen ni mwanga wa orange hii mnayoita njano.
 
Dah...umenikumbusha....kuna wajinga waliniuzia pale lumumba taa nyeupe nikawa nasafiri naenda arusha alafu usiku ......bas mvua nayo hiyo mara wiper moja imeng'oka imeruka.....lami ndio siioni kabisaaa

Nlikua natumbua macho kwenye barabara utadhani mjusi kabanwa na mlango....mwisho wa siku ikabid nilale tu moshi asubuh nikaendelea.....nlivorud town cha kwanza ilikua ni kuing'oa ile mitaa....
Unajua hii kitu sio kweli kwasababu ukitazama hata gari za kisasa zote zinakuja na Bulb hizi za mwanga wa Blue white (LED) kama ni uongo tazama gari zote za kisasa ambazo wanatengeneza kwa standards za kimataifa wanaweka bulb za aina gani.

Tazama Vogue, Jaguar, Mercedes, Nissan, Ferrari, etc brand zote utaona wameachana na hizo bulb za halogen.

Nadhani ninyi ambazo zinawapa shida huwa mnakosea mnapokwenda kununua bulbs hamtazami standard yake na ubora.

Hebu ukienda nunua kwa wauzaji wanaozijua. Na utazame specifications za hiyo bulb.

Sio unanunua bulb ya nguvu ndogo halafu unalalamika hauoni ukimulikwa na dereva anaekuja mbele yako. Ofcourse bulbs yako ikiwa haina nguvu lazima mwanga wake utakuwa hafifu kwa dereva mwingine.

Lakini pia hizi bulb katika fog huwa zinasaidiana na zile fog light kwenye bumper na unaona vema tu.

Shida unakuta mtu katika sehemu ya fog lights ameweka bulb za urembo mradi tu zinawaka.

Zipo taa za fog za rangi ya LED na zipo Fog za mwanga wa orage yaani ule wa halogen. Wewe unachagua ufunge zipi ila ni vema kwenda na specifications.
 
Nyie wenye magari, kwanini mnawekaga taa nyeusi kwenye gari ? Sijui mnabandika tinted au vipi lakini gari nyingi siku hizi taa zake sio nyeupe unakuta ni nyeusi
Zina mwanga kweli ?
Nashangaa kwann traffic officers wanacheka nao. Unakuta mtu anaweka tinted kwenye taa ya break ili iweje yaani?!
 
Wewe utakuwa umefungiwa C6, kuna taa zinauzwa kuanzia 150,000 na kuendelea mwanga wake hata inyeshe mvua ni balaa
Kabisa. Watu wananunua hizi bulb za bei nafuu halafu wanalalamika. Hivi huwa wanaona bulb za VX, Prado, toyota land cruiser, Discovery, Harrier new model, Mercedes benz, BMW, VW ikipigwa low beem unaona hadi ramani ya Africa.

Sasa jiulize akipiga full itakuwaje. Na zile taa huwa zinakuja na lenzi yake. So ikiwashwa inalenga on point inapomulika so hakuna umande utaiblock hiyo beam.

Vijana wazito sana kujifunza. Changamoto kidogo tayari wanatoa conclusions badala ya kutuliza kichwa kudadisi shida imeanzia wapi.

Ndo maana wengi magari ya kiume yanawashinda wanapenda brand nyepesi kutumia kama Toyota maana hawataki kunoa akili zao na kuyajua magari.

Kuna ndugu yangu ni dereva alikaa na mzungu kwenye gari yake namna alikuwa naifuatilia alikuwa anaijua kuliko yule mzungu sasa ukikuta anamuelekeza utacheka maana uona mbongo anamfunza mzungu kuhusu gari na hatuna hata kiwanda cha magari [emoji23][emoji23][emoji23]
 
But halogen ni mwanga wa orange hii mnayoita njano.
Unachosema ni kweli lakini zimetofautiana kwenye zile kelvins..i.e 3000K ni mwanga wa njano, 5000K hii inakua nyeupe (nyingi kwa nje zinakuaga na rangi ya blue) halafu kuna 6000K, 8000k, 10000K hadi 12,000K mimi nimeweka halogen lakini ni 5000K ila inaweza kua ni Led ya 5000k maana sijicheki kwa umakini
 
It's way too expensive, sasa kama taa inaweza kufika hadi milioni 12-si ni bora kuongeza gari nyingine kabisa au kuendesha mchana- Binafsi hapana aisee

Hizo K ni color temperature sio pesa. Taa inavyozidi kuwa na K kubwa basi inazidi kuwa nyeupe, na ikizidi inakuwa blue.

Taa yoyote yenye chini ya 4300K basi ina mwanga wa njano, ikiwa 5000K hadi 6000K hivi , hiyo ni nyeupe, ikiwa kuanzia 8000K hadi 12000K hiyo ni Blue.

Kwa mantiki hiyo basi, halogen nyingi zipo chini ya 5000K, wakati LED na HID nyingi zinaanzia 43000K na kuendelea.
 
Hizo K ni color temperature sio pesa. Taa inavyozidi kuwa na K kubwa basi inazidi kuwa nyeupe, na ikizidi inakuwa blue.

Taa yoyote yenye chini ya 4300K basi ina mwanga wa njano, ikiwa 5000K hadi 6000K hivi , hiyo ni nyeupe, ikiwa kuanzia 8000K hadi 12000K hiyo ni Blue.

Kwa mantiki hiyo basi, halogen nyingi zipo chini ya 5000K, wakati LED na HID nyingi zinaanzia 43000K na kuendelea.
Nashukuru sana kwa kunijengea uelewa.
 
Road ya Dodoma - Iringa wamejitahidi na hizi barabara mpya mpya, kasheshe kipande cha Shinyanga - Mwanza alafu upigwe taa karibu na kona yaani unajikuta umenyoosha vichakani

Sie wenye magari ya kizamani yenye taa za kutumia busara ukiwa road huwa hatutaki tabu tukimwona mtu anakuja nyuma unampisha, akikupita tu unaunga unakuwa nyuma yake kwa gape la 5 - 10 metres ili akusaidie ku-block mwanga wa magari ya mbele yanayokuja. Kasheshe liwe mbele VIEITEEE yaani utaenda nalo dakika kadhaa baadae unaliona hiloooooo maana ukikomaa unaona ngoma sterling inatikisika
Aiseee Leo nimepata jibu banaa!!! Mwaka Jana kuna jamaa alikuwa ananifata Kwa nyuma kutoka shinyanga Hadi misungwi jino Kwa jino kila nikipunguza mwendo na yeye anapunga mwendo...hapa ndiyo napata jibu kuwa Yule Fala alinigeuza PAZIA la kuzuia mwanga!!! Barabarani kuna vituko Sana maana hii comment yako nimecheka sanaaaaa mwenyewe kumbe Ile style ya jamaa ilikuwa ni zuga.
Tulikuwa tunajiuliza mbona huyu jamaa anafata nyuma yetu hata kama nitapunguza speed Hadi 40
 
Back
Top Bottom