Msomi mzima huna upeo kiasi hiki? ni nini udini? basi na mafuta tusinunue toka Middle East. kina Mtikila walikuwa wanaandamana jee wametoka mashariki?
kiongozi wa TLP leo rwekamwa alikanganya bendera ya Taifa letu hadharani ametoka middle East?
kumbe ndio maana umekuwa ukimtuhumu Professor Kighoma Malima humu bila ushahidi. yaani ndugu yetu hata maiti unamchukia?
kama wewe mkweli juu ya Marehemu malima na uadilifu wake kwa nchi tupatie ripoti ya M.V BUKOBA?
mbona Mkapa aliitia kapuni? Malima kwa uadilifu wake alipinga ununuzi wa ile meli kuwa ni bomu aliyeleta tenda ile ni sir Kahama suala lile kwenda kwa Mwalimu Nyerere akamuunga Mkono Kahama halafu Malima akaamua kujiuzulu, na kwenda zake kufundisha Marekani.
Matokeo ya Malima tumeyaona wote kifupi ni majuto mjukuu.
mzee acha roho mbaya ya udini sote ni binadamu na nchi ya wote.ni bora mtuambie kuwa mko kwenye CRUSADE inawezekana ni wewe uliyepinga OIC bila kuzingatia maslahi makubwa kwa nchi mwenzetu museveni kawakubali OIC anakula kwa mrija sie tufe na udini wetu.
kama nchi za middle East hazifai vipi chuo kikuu cha Dodoma wanakifadhili? tukatae pesa zao.mpelekeni Bush atumalizie chuo kama ni mkweli.
Actually kuchoma bendera kwa nchi kama Marekani si kosa la jinai hata US Supreme Court iliruhusu uchomaji wa bendera kwa amani kama ishara ya political speech.Chuma
Bendera ni ishara ya taifa na tumeweka viwango ambavyo binadamu wanaweza kubishana bila kupigana. Unapofika kuweka dhihaka kwenye bendera, ngao na nyimbo za mataifa mbali mbali basi wewe unakuwa punguani. Kuna standards ambazo tumejiwekea ambazo kama huzifuati basi wewe unakuwa na kasoro.
Hili lipo hata kwenye elimu standards zinawekwa na baadaye zinafuatwa, kama huwezi kulielewa hili ni sawa na kurudi katika karne za nyuma na kuanza kuvaa nyasi au magamba ya miti.
USTAARABU NI KITU CHA BURE LAKINI GHARAMA YAKE NI KUBWA.
Invisible and the forces that be, nimetaka kuweka picha hapa. Siku hizi ni mpaka m-approve au?
hii thread nzima mie nitai-summarize ktk neno moja, nalo ni MADNESS!!!.
achaneni na mambo ya udini, mnajitia aibu za bure, mnaji-expose kwa undani zaidi na mwisho wa siku hakuna cha maana mtakachopata zaidi ya kuchora mistari ya utengano!!
nakumbuka kabla ya 9/11 hata hapa USA kuchoma bendera ya marekani haikuwa kinyume cha sheria!! watu kuandamana hapa hapa USA juu ya ujio wa bush kwenye mji wao ni kitu cha kawaida......mfano mji ninaoishi bush ni "sumu" na yeye analijua hilo kiasi haji!!!
sasa hili yengele hapa litawapeleka wapi nyinyi ma-extremist(wote waslam na kristo). tena bush mwenyewe atasema kwamba "nimeenda tanzania, nimekuta democrasia ya hali ya juu!! kwani watu wanahaki ya kuandamana juu ya lolote provided hawavunji sheria."
kuna watu both sides, wana/mna tamani sana kutokee mfarakano wa kidini nchini TZ. mie hata siwaelewi ni chepi mtakachofaidika nacho........inshallah, naomba mungu nia zenu mbaya zishindwe na mlegee!!!
KWANZA NI KUMWAMBIA KUWA WAO WANA VITA VYAO VYA UGAIDI NA SISI TUNA VYETU VYA UFISADI!NDIVYO TUNAVYOTAKA VIPEWE KIPAUMBELE..KWANI HUJUI WATU WANAOKUFA KWA MAGONJWA NA NJAA NI WENGI KULIKO WALE WALIOKUFA KWENYE MABOMU YA UBALOZI 98?UPO?Mushi Jambo gani la kitaifa linalomfanya Bush atembelee TZ?...
Hii tabia ya kuchoma bendera ya marekani (na kudai kuwa Death to America) ni tabia ya militants iliyoaniza mashariki ya kati na kusambaa. Inaelekea kuwa sasa hivi imeanza kuingia Tanzania; kwa hiyo Tanzania tujihadghali kwa vile hii ni dalili kuonyesha kuwa na sisi tumeanza kuwa na hao militants.
Mtalii kwanini usiwashauri kina njozi wapigie kelele ripoti ya MV Bukoba?
watu waandamane kumpinga BUSHI sera zake na sio kukimbilia eti ana isakama dini fulani.
Bushi ni mafia hana cha uislamu ama mkristo wote wakikaa mbele yake anawamafia vilevile
Haya mambo ya vita yameanza siku nyingi wanapigania maslahi Bushi ni mwendelezo tu wa hayo maslahi ,ni kitu cha ajabu sana kusema anapigana na uislamu jamani Bush IRAQ na ILAN anatafuta MAFUTA.Bongo anakuja kutafuta mahala pakuweka base yake ili akombe hayo mafuta ya Angola vijidhahabu vyetu,vya kongo na huko ghana,
Mkamap,
Mkuu wangu nadhani hutazami mapana ya issue nzima na nani muathirika.. Ni sawa na kusema Hata South Africa Kaburu alikuwa akitafuta Almasi , dhahabu na utajiri mwingine sio mtu mweusi kama kuuana waliuana toka enzi za Shaka Zulu...
Na kwa nini tuliandamana na pengine kwenda pigana cita huko South hali Ubaguzi upo kila kona duniani... kwa nini tusiende kila nchi yenye Ubaguzi na hasa Israel kama sisi tulikuwa tunatafuta haki?..
Ndugu zangu nitakuacheni na Hekima za Mzee Jumbe...by Mkandara.
Mzee Jumbe aliibiwa Genetrator ya Umeme akaamua kwenda Polisi yoa habari. Alipofika pale alikutana na mkuu wa Kituo na kuomba afungue mashtaka..
Baada ya kusikiliza mashtaka hayo huyo mkuu wa kituo alisema - Mzee Jumbe umekuja hapa shtaki kuibiwa generator kwa nini usutumie nafasi na muda huu kumshtaki Lowassa ambaye alitunyima nchi nzima Umeme? nadhani utakuwa umefanya la maana sana kwani hiyo generator yako sidhani kama itapatikana wala haitakusaidia kitu kufungua mashtaka...
Kwa hekima na Busara mzee Jumbe alisema:- 'Afande, maneno yako kweli tupu na hakika swala la Lowassa ni zito zaidi. Sasa unaonaje maadam nipo hapa wewe kama afande nakuomba fungua mashtaka na mimi hapa nipo kama shahidi wako!'
Nitakujibu swali la Pili...Swali lingine, hivi ugaidi tunaoushuhudia leo sehemu mbali mbali duniani eg Pakistan, Afghanistan, Iran etc, kama usingekuwa unatumia mwavuli wa dini ya kiislamu, ungefanikiwa?, I mean could they convince people like militants and fanatics to do what they do like blowing up buildings, themselves? Could they? WITHOUT USING THE NAME OF ISLAM?
Masanja,
Nitakujibu swali la Pili...
Kwanza unalitazama swala hili kwa zangi na huyaoni mengi kwa sababu hayakuhusu... So let me touch you pale panapo kuhusu.
Umeuliza matumizi ya dini ktk nchi hizo kufanya Ugaidi, sasa nakuuliza wewe ilikuwaje sisi waafrika tulitumia weusi wetu (rangi) ktk ukombozi wa Afrika?...na tuliunda magaidi kutokana na rangi zetu, whites walikuwa na fikra kama zako na walishindwa kabisa kuelewa.
.