Taarifa wakazi wa Iringa waanza kula panya kama kitoweo!

Uzalendo wa Kitanzania

JF-Expert Member
Joined
Mar 8, 2020
Posts
3,585
Reaction score
8,106
Wadau hamjamboni nyote
Gazeti la mwwnanchi linaripoti kuwa Ndugu zetu huko Iringa Sasa wameamua kula panya kama kitoweo wakidai kina protein Kwa wingi sana

Taarifa kamili hapo chini
#Repost @mwananchi_official
——
Wakazi wa Kijiji cha Ndengisivili wilayani Kilolo mkoani Iringa, wamesema ulaji wa panya umekuwa silaha kubwa katika kupambana na uharibifu wa mazao yao hasa mahindi shambani.

Wamesema mbali na kuokoa mazao, nyama ya panya ina madini muhimu kwenye mwili wa binadamu jambo lililowafanya waipende nyama hiyo.

Kati ya utani unaowatambulisha zaidi wakazi wa Mkoa wa Iringa ni ulaji wa nyama ya mbwa ambao, hata hivyo hawajawahi kuukubali.

Hata hivyo, Wataalamu kutoka Chuo Kikuu cha Kilimo cha Sokoine (SUA) wametoa wito kwa Watanzania kula nyama ya panya kwa madai kuwa ina virutubisho adimu mwilini.

Akizungumza na Mwananchi leo Mei 10, 2024 wakati akiandaa panya kwa ajili ya kitoweo, mkazi wa Ndengisivili, Boas Kikoto amesema nyama ya panya ina madini muhimu kwenye mwili lakini pia unapunguza uharibifu wa mazao shambani.

Soma kwa undani www.mwananchi.co.tz

(Imeandaliwa na Tumain Msowoya)
#mwananchiupdates
#tunaliwezeshataifa
 
Safi sana watani zangu nyama ya panya siyo tu ina madini adimu bali ni tamu balaa.
 
Nyama ya sasara mchanga ni tamu sana.
 
Wanaoliwa Ni wale panya wakubwa wanaitwa Ngombwe...
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…