Taarifa ya polisi mlipuko Arusha; Victor Ambros kufikishwa mahakamani


Wewe nawe sijui unafikiria kwa kutumia nini? hizo pesa zinatoka kwenye mfuko wa jeshi sio mfukoni mwake.
 

Unaposoma taarifa za serikali usisome kama kitabu cha Willy Gamba. Jifunze kuelewa ujumbe unaotolewea.

Kukusaidia tu ni kwamba raia hawa wameingia nchini kimagumashi. Kwa vile tarehe walizoingia zimeingiliana na tukio hili kumekuwa na ulazima wa kuwascreen kuwa hawahusiki.

Hawajaachiwa huru. Jeshi la polisi halijasema kuwa wameingia nchini kimagumashi, ila limesema kuwa wamekabidhiwa kwa mamlaka husika juu ya jinsi walivyoingia nchini.

Mara nyingi wafanyabiashara huingia nchini na visa za kitalii. Jambo ambalo ni kinyume cha kisheria.
 
Huyo Victor wamemuonea tu!kama wamekosa watu wa kuwashika,wangesema upepelezi unaendelea,huyo Ambrose hana kosa!kumpa kesi mauaji ni kumuonea!
mtaje ni nani sasa anahusika, mil.50 hiyo hapo.
 
Kwa maelezo hayo ya Jeshi la Polisi, bado sijaona kama huyo Victor ndiye mshukiwa nambari moja.
Jeshi la Polisi lieleze kwa undani namna bomu hilo linavyohusishwa na huyo bwana mdogo, sio kutueleza tu kuwa lilirushwa.
Ni jambo gani lililowashawishi hata kuamini kweli mtu huyo ndiye mhusika mkuu.
Ni nini motive ya yeye kufanya hivyo?
Kwa nini iwe ni kwa kanisa katoliki?
 
kazi kwelikweli...............................!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!??????????????
 
Nimepitia taarifa sijaelewa kisa cha Ambros kufikishwa mahakamani, hebu waliohudhuria mtupashe taarifa zaidi. Huyo kijana wameeleza ni mwendasha boda boda, Je yeye alikuwa na bomu na kulirusha au kosa lake ni nini? Au walikuwa na nia moja na mrusha bomu?.
 
nafasi ni yako sasa kumtaja mtuhumiwa kuna mil 50 zinakungoja mkuu
sidhani kama ambrose anajua chochote maana yeye inadaiwa kampeleka mteja mahali alipoelekezwa na mteja,so si rahisi kumjua mteja aliyembeba,nadhani mashahidi wapo waliomwona ambrose akimbeba ??mtuhumiwa aliyechapa mwendo baada ya tukio sababu tukio lilitokea mchana,ambros anatakiwa apate mawakili akina tundu lisu,abdhala safari ili wamtetee apate haki yake,chadema si lazima wawatetee wanachama wao tuu pia na hata raia kama huyo tena yatima,nafikiri hili litawajenga zaidi kisiasa
 

viongozi wote walisema kua ule ulikua ni ugaidi. Mbona huyo mtuhumiwa hakushitakiwa kwa kosa la ugaidi?. Au kwa sababu si muislamu.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…