Taarifa za Usajili wa vilabu vya Soka, msimu wa 2015/2016

Taarifa za Usajili wa vilabu vya Soka, msimu wa 2015/2016

Kocha Carlo Ancelotti amesema atafurahi akipata mtonyo wa kuifundisha Liverpool.
 
Kinda anayetisha midfield Paul Pogba (22) anakaribia kutua Mancity kwa dau la £45m.
 
chanongo alishindwa kwenda tp mazembe kufanya majaribio baada ya kupata majeraha ya mguu kwenye mechi ya yanga vs stand united uwanja wa taifa.
kwahiyo kaambiwa yanga ndio tmj hospt
 
Rafael Benitez ameaga rasmi Napoli akiwa njiani kutua Real Madrid
 
ManUtd imeziambia Bayern na PSG kwamba anayemtaka Angel Di Maria itabidi aumie kama walivyoumia wao kumwaga dau nene la £59.7m.
 
Baada ya kumalizika kwa msimu wa soka 2014/2015 katika ligi mbalimbali barani Ulaya na kila timu kuvuna ilichopanda,sasa ni nafasi nyingine kwa timu kutumia pesa zilizovuna baada ya ligi kwa kusaka wachezaji ambao zinadhani ni bora kwa ajili ya kuimarisha vikosi vyao na kuleta ushindani mkubwa ili kutetea au kushinda vikombe.

Ikiwa ni juma la kwanza baada ya dirisha la usajili kufunguliwa kuna tetesi nyingi kuhusiana na baadhi ya wachezaji wenye majina makubwa na wale wasiokuwa na majina makubwa kuwa na uwezekano wa kuhama vilabu vyao na kujiunga na vilabu vingine aidha kwenye ligi ya awali au kwenye ligi tofauti

Vilabu vikubwa na tajiri kama Real Madrid,Chelsea,Man united,Barcelona,Arsenal,Man City,Juventus,Liverpool,Bayern Munich,AC Milan na vingingine vimeanza kupigana vikumbo kwa ajili kunasa saini ya wachezaji na hata makocha.

Baadhi ya wanasoka mahiri ambao inasemekana kuna uwezekano mkubwa wa kuhama vilabu vyao na kwenda vilabu vingine kwa ajili ya aidha maslahi au changamoto ni pamoja na:-

1.Gareth Bale
2.David de Gea
3.Paul Pogba
4.Karim Benzema
5.Raheem Sterling
6.Nathaniel Clyne
7.Yaya Toure
8.James Milner
9.Hugo Lorris
10.Gonzalo Higuain
11.Ikey Gundogon
12.Peter Chech
13.Mario Gotze
14.Antonio Guerzman
15.Ortamendi
16.Carlos Tevez
17.Cuadrado Juan
18.Dany Ings
19.Angel Dimaria
20.Radamel Falcao
19.Nicolas Gaitan
20.Sami Khedira
21.Theo Walcot
22.Christian Benteke
23.Dany Alves
24.Lucas Poldoski
25.Robin Van Persie
26. Drogba Didier
27.Oscar
28.Jackson Martnez
29.Diabara
30.Morgan Shirnderlin

Hao ni sehemu tu ya wengi wanaotarajiwa kuhama kwenye vilabu vyao

Nani ataenda wapi,nani kaenda wapi,tupia taarifa!!!!!!!!!!!
 
Vidal na Peter Chech kutua arsenal, hili chama msimu ujao lisipokuwa double winner uefa na EPL sijui.
 
Vidal hana nafasi ya kucheza arsenal! Wenger kashakanusha juu ya huu uvumi
 
Arsenal inammendea kiungo mkabaji Geoffrey Kondogbia (22) wa Monaco kwa dau la £25m.
 
Paulo Dybala toka Parlemo nae tayari amejiunga Vibibi vizee vya Turin -Juventus kwa ada ya uhamisho inayokadiriwa kufikia €32
 
Man City wapo tayari kutoa kitita cha €50 kwa aijili ya kupata saini ya Raheem Sterling toka Liverpool

Chanzo: CAUGHTOFFSIDE
 
Club ya Liverpool karibuni itamtangaza James Milner kama mchezaji wao mpya kutoka Man city.....
 
Tom Cleverly amesajiliwa rasmi Everton

Source: CAUGHTOFFSIDE
 
by kichwat;
ManUtd imeziambia Bayern na PSG kwamba anayemtaka Angel Di Maria itabidi aumie kama walivyoumia wao kumwaga dau nene la £59.7m.



Mkuu kichwat, nani anunue hayo masikio kwa hiyo bei? wabaki nayo hamna mtu wa kuyanunua!
 
Last edited by a moderator:
Arsenal imemwaga dau la £29m kumchukua straika wa Napoli Gonzalo Higuain (27). Napoli wanasema hatoki mtu bila £36m kuwekwa mezani.
 
Arsenal imemwaga dau la £29m kumchukua straika wa Napoli Gonzalo Higuain (27). Napoli wanasema hatoki mtu bila £36m kuwekwa mezani.
Higuain gani wakununuliwa kwa pesa ndefu yote hiyo!!! Labda awe yule ambae alikuwa moto wa kuotea mbali akiwa pale Real Madrid, Ila kama ni huyu wa Napoli hana thaman ya hela zote hizo....
 
Real Madrid wanatarajia kukutana na wakala wa David De Gea leo kwaajili ya mazungumzo ya kumnasa mlinda mlango huyo anaekipiga Manchester United kwasasa
 
Back
Top Bottom