TAARUKI MSIMBAZI (Huko kwa mikia fc aka mbumbumbu fc wazee wa spray kumewaka moto)

Hao wanaosemekana wana bifu wamekodi ndege binafsi kwenda Congo. Kweli ujinga wa wapuuzi umevuka mpaka. Wachezaji wao wanakula kwenye sinia ili chakula kitoshe. Feisal Toto aliliweka hilo wazi baada ya kulinganisha kambi ya timu ya Taifa na Vyura.Wachezaji wana njaa wao hawafikiri kazi kuwa obsessed na Simba.
Simba sasa hivi sio level yenu.Saizi yenu ni Ndanda na Singida United.
 
Kakolanya, Ajibu wamekimbia njaa. Kula kwenye sinia watano ,watano kama hitima kumewachosha.
 
Hili suala liko wazi ,simba waliingia mkataba wa kijinga sana. Sasa hvi zile ngojera za ujenzi wa uwanja wa kisasa zmekufa.
Tangu lini mshabiki wa makwasukwasu a.k.a ombaomba fc atupangie sisi namna ya kuingia mikataba....sawa sisi tuliingia mkataba wa kijinga nyie ingieni mkataba wenye akili na kina mzee akilimali
 
Hawa wafanya biashara kama wakina Dewji, kama kweli wanania nzuri ya kuendeleza soka la Tanzania ni vizuri wakanunua timu waendeshe wenyewe wanavyotaka. Haya mambo ya kung'ang'ania Yanga na Simba sijaona bado mafanikio yoyote zaidi ya migogoro miaka inakwenda timu zimebaki hapo hapo tu.

Kama nia kuendesha timu kibiashara watafute timu kama alivyofanya Azam waendeshe kibiashara. Waendeleze vipaji kutoka utotoni mpaka mafanikio yatapatikana.

Watanzania hatupendi maendeleo na ni waoga wa mabadiliko, kila kitu tunataka tufanye kwa mazoea bila kuingiza mbinu mpya hili tusonge mbele.
 
Mkuu huu ushauri ungempa manji kipindi kile alivyokuwa anaimiliki timu yenu kwa sasa hatudanganyiki.....sisi washabiki wa simba tupo tayari kumpa moodewji timu yote aichukue iwe yake kabisa nyie yanga hayawahusu...kwanini mnateseka???sahivi ndo mnajifanya akili zimewarudi mmekuwa watoa ushauri...huo ushauri peaneni hukohuko kwenu na kina mzee akilimali
 
Kwa taarifa yako mimi Simba damu na nimetoa maoni kama mshabiki wa mpira na sio kama mshabiki wa klabu ya mpira.

Tatizo letu ndio hapo, kila kitu mnaweka ushabiki wa timu mbele kuliko muelekeo wa soka la Tanzania kwa ujumla. Ni ngumu kutoa maoni mazuri kama unaweka ushabiki wa timu mbele. Tunaweka chuki binafsi kwenye kila jambo; ndio maana juzi ukaona wale wanaomchukia Bashite wali omba timu ya Taaifa ifungwe wakati timu ya Taifa inawakilisha wa Tanzania wote na sio mtu mmoja (bashite).

Sasa swala la Mo kama nia kumpa timu, apewe timu ili aanze kutimiza malengo yake badala ya makundi kuanzisha migogoro ambayo inaweza kukwamisha maendeleo ya timu.
 
SI RAHISI KAMA MNAVYOWAZA! SIO WOTE WANAOFURAHI MAFANIKIO YA DEWJI!,, WAMEACHIWA 51% MBONA HAMJITOKEZI KUWEKEZA HATA KUSEMA NA NUNUA 29% AU 15%? KAMA HAO WAZEE WATASEMA WANAVUNJA MKATABA UNAWEZA MLIPA BILIONI 6!
 
Huwezi kuwa mshabiki wa simba wewe..mshabiki gani usijejua kuwa kilichopo ni simba tumebadilisha mfumo wa uendeshaji wa timu...maswala ya kusema moodewji akanunue timu yake yanatoka wapi umeambiwa sisi tunataka kuiuza timu...kilichopo tumebadilisha mfumo wa uendeshaji wa timu...na mfumo huyo ndo unatumiwa hata ulaya na vilabu vikubwa tena karibu vyote...simba hata wewe unaweza kuwa sehemu ya umiliki ni pesa yako tu...leo hata wewe ukienda na mabilioni yako ukitaka kumtoa moodewji nenda tunakupa timu...hizi kelele za baadhi ya mashabiki hatuzipi nafasi tena...kwani wa avyosema mo sjui anataka nini hii simba tangu imeanza mpaka lei ina nini zaidi ya kile kijengo kariakoo...inasikitisha timu kama simba haina hata uwanja wa mazoezi...leo hii tumepata mwekezaji anatujengea uwanja...ananunua wachezaji kwa bei kubwa kuna watu wanaanza kelele kelele sababu wanaona wameshindwa kupiga dili na kula hela za zimba...simba we are in a right track
 
Reactions: Tui
Wew Wewe unazo hisa ngapi kwenye hiyo club yenu? Au unajifurahisha tu. Bora sisi tunaochangia kuliko nyie. Hiyo timu ni Mali ya MTU, mtake mistake habari ndiyo hiyo. Povu ruksa
 
Imepenya hiyooo na kukuna pale penyewe.
Kama kichwa cha Kagere. NAONA tokea kile kichwa kiingie mnaweweseka sana.Na bado safari ndio kwanza imeanza. Mkitoa droo fanyeni maandamano.
 
Wew
Wewe unazo hisa ngapi kwenye hiyo club yenu? Au unajifurahisha tu. Bora sisi tunaochangia kuliko nyie. Hiyo timu ni Mali ya MTU, mtake mistake habari ndiyo hiyo. Povu ruksa
Hata ikiwa mali ya mtu nyi yanawahusu nini....ndiyo ni mali ya mtu tumeamua kumpa moodewji....na tumempa sasa tena tumemuuzia kimojamoja milele na milele....inauma eeeeh???..toa namba ya ombaomba fc mnayochangishia hela kuna buku hapa nataka niwape nasikia wachezaji wanakufa njaa huko
 
Reactions: Tui
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…