Taasisi Mbalimbali zatoa vifaa vya Tehama Kukabiliana na uhalifu Arusha

Taasisi Mbalimbali zatoa vifaa vya Tehama Kukabiliana na uhalifu Arusha

Roving Journalist

JF Roving Journalist
Joined
Apr 18, 2017
Posts
3,984
Reaction score
13,760
WhatsApp Image 2024-11-20 at 17.45.11_d1d5d150.jpg


Taasisi na Idara mbalimbali Mkoani Arusha zimeendelea kushirikiana na Jeshi la Polisi Mkoani humo katika kupambana na uhalifu ambapo Idara ya maji na Benki ya Crdb wametoa vifaa vya Tehama katika kituo kikuu cha Polisi Arusha.

Akiongea mara baada ya kukabidhi vifaa hivyo Mkurungenzi wa mamlaka ya Maji Safi na Maji taka Mkoa wa Arusha Mhandisi Justine Rujomba amesema kuwa lengo la kutoa vifaa hivyo ni kuboresha na kuongeza ufanisi wa utendaji wa Jeshi la Polisi katika kutoa huduma bora kwa wananchi.
WhatsApp Image 2024-11-20 at 17.43.12_b5c293af.jpg
WhatsApp Image 2024-11-20 at 17.45.13_123ed37f.jpg
Ameongeza kuwa anatambua mchango wa Jeshi la Polisi katika ulinzi wa raia na mali zao ambapo ameweka wazi kuwa mamlaka ya maji jijini Arusha imekuwa mnufaika wa huduma zinazotolewa na Jeshi hilo.

Kwa upanda wake Meneja wa Benki ya Crdb tawi la Arusha Bi Mary Kimasa amesema kuwa ujio wao ni kuendelea kushirikiana na Jeshi la Polisi huku akiweka kuwa vifaa hivyo anaamini vitakwenda kusaidia Jeshi hilo ambalo linategemewa na wananchi katika ulinzi wao na mali zao.

Nae Mkuu wa Polisi Wilaya ya Arusha Mrakibu Mwandamizi wa Polisi SSP Georgina Matagi amezishukuru taasisi hizo ambazo zimetoa vifaa hivyo huku akiwasihi wengine kuendelea kushirikiana na Jeshi la Polisi wilayani humo katika mapambano dhidi ya uhalifu.

Mwilikiwa Masawe ambaye ni Mjumbe wa bodi ya maji Salama Mkoa wa Arusha amesema waliamua kuleta vifaa vya Tehama wakitambua mchango na mapambano ya uhalifu yanayofanywa na Polisi Wilaya ya Arusha ili kuwasaidia katika mapambano hayo.
 
Watakuja watu hapa kumuulizia huyo WP
Maswali ni muhimu kwanini Ar chuga imejaa uhalifu,wasimamizi wasaidizi wana vimelea vya uhalifu na wasimamiwa wasaidiwa vimelea vya uhalifu vipo,baya zaidi tiba ya vimelea vyote vya uhalifu havijapata dawa wala tiba mujarabu.
 
Back
Top Bottom