Taasisi ya elimu ya juu imeanzisha chama cha kusaidiana kufuata dini ndani ya Ofisi ya serikali

Taasisi ya elimu ya juu imeanzisha chama cha kusaidiana kufuata dini ndani ya Ofisi ya serikali

Zygot

JF-Expert Member
Joined
Apr 14, 2016
Posts
2,265
Reaction score
2,919
Kuna taasisi ya elimu ya juu imeruhusu umoja wa kusaidiana kwa misingi ya dini. Tafsiri yangu ni kwamba, kwa kuunda umoja huo, na kuhamasishwa na viongozi wa taasisi ni ishara ya kuwatenga watu wa dini zingine.

Nimeona ushahidi kupitia kumbukumbu ya malipo ya mishahara (salary slip) ya mmoja wa wanachama hao ikionesha michango ya umoja huo inakatwa moja kwa moja toka hazina ya serikali. Bado 'nabembeleza' kupata nakara ya malipo hayo, nitaileta hapa jamvini.

Ni vema kutoa tahadhari kwa viongozi hawa dhaifu wanaofikia hatua ya kuhamasisha umoja wa kusaidiana kwa misingi ya dini ndani ya ofisi za serikali. Mbaya zaidi ni taasisi ya elimu ya juu! Kwa maana nyingine hata elimu itatolewa kwa misingi ya kidini.
 
Hilo jambo kama ni la kweli, basi litakuwa halina kabisa afya mahali pa kazi. Na uzuri hujataja ni dini gani!
 
Kuna taasisi ya elimu ya juu imeruhusu umoja wa kusaidiana kwa misingi ya dini. Tafsiri yangu ni kwamba, kwa kuunda umoja huo, na kuhamasishwa na viongozi wa taasisi ni ishara ya kuwatenga watu wa dini zingine.

Nimeona ushahidi kupitia kumbukumbu ya malipo ya mishahara (salary slip) ya mmoja wa wanachama hao ikionesha michango ya umoja huo inakatwa moja kwa moja toka hazina ya serikali. Bado 'nabembeleza' kupata nakara ya malipo hayo, nitaileta hapa jamvini.

Ni vema kutoa tahadhari kwa viongozi hawa dhaifu wanaofikia hatua ya kuhamasisha umoja wa kusaidiana kwa misingi ya dini ndani ya ofisi za serikali. Mbaya zaidi ni taasisi ya elimu ya juu! Kwa maana nyingine hata elimu itatolewa kwa misingi ya kidini.
Itaje hiyo taasisi, unaficha ficha nini??
 
Kuna taasisi ya elimu ya juu imeruhusu umoja wa kusaidiana kwa misingi ya dini. Tafsiri yangu ni kwamba, kwa kuunda umoja huo, na kuhamasishwa na viongozi wa taasisi ni ishara ya kuwatenga watu wa dini zingine.

Nimeona ushahidi kupitia kumbukumbu ya malipo ya mishahara (salary slip) ya mmoja wa wanachama hao ikionesha michango ya umoja huo inakatwa moja kwa moja toka hazina ya serikali. Bado 'nabembeleza' kupata nakara ya malipo hayo, nitaileta hapa jamvini.

Ni vema kutoa tahadhari kwa viongozi hawa dhaifu wanaofikia hatua ya kuhamasisha umoja wa kusaidiana kwa misingi ya dini ndani ya ofisi za serikali. Mbaya zaidi ni taasisi ya elimu ya juu! Kwa maana nyingine hata elimu itatolewa kwa misingi ya kidini.
Tanzania yangu ni salama sana ikiwa tu, ikiachwa na misingi ileile tuliyorithishwa na waasisi wetu, hasa hasa kwenye mambo ya Imani

Ni ujinga kuanza kupuuza misingi hiyo kwa lengo lolote lile dhidi ya dini moja ama vinginevyo

Kwa miaka mingi sasa tongu tuwe huru, inatosha kusema, mambo ya kijinga yenye lengo la kututenganisha hasa hasa ya kidini yangelikuwa yamekoma kabisa na zaidi tukawa Taifa lenye kulenga kutatua shida za wananchi tu na siyo brabraa@

Hii huwa ni mihemko ya hovyo sana kwa wanasiasa hasa kunapokaribia uchaguzi

Dini ingebaki kwa wananchi na serikali na ama taadisi zozote za kiserikali zikaendelea na mipango ya kusukuma maendeleo kwa wananchi

Hili tutaliimba mpaka lini?

Shetani wa Tanzania huwa hatulii kwa nini?

Anayekuwa anamtumia iko siku moja atamla nyama

Tanzania bila udini na ufitini inawezekana
 
Hii awamu kila kukicha mambo yanaenda vibaya sana..
1. Udini unazalisha chuki,
2. Udini utazalisha UGAIDI 😕😕😕
 
Akchuari mimi niliisikia siku nyingi. Ingawa haijatajwa lakini nilisikia mazungumzo ya aina hii yakiwahusu Sokoine University pale Morogoro.

Source ya taarifa yangu ni mke wa rafiki yangu ambaye naye alifuatwa kwa lengo la kuruhusu mshahara wake ukatwe. Ikabidi mume atoe ushauri. Watakuwa ni SUA tu! Mambo tu ya kishenzi maeneo ya kazi.
 
Akchuari mimi niliisikia siku nyingi. Ingawa haijatajwa lakini nilisikia mazungumzo ya aina hii yakiwahusu Sokoine University pale Morogoro.

Source ya taarifa yangu ni mke wa rafiki yangu ambaye naye alifuatwa kwa lengo la kuruhusu mshahara wake ukatwe. Ikabidi mume atoe ushauri. Watakuwa ni SUA tu! Mambo tu ya kishenzi maeneo ya kazi.
Itaje hiyo taasisi, unaficha ficha nini??
Chuo kilichoweka mfumo huu kwa muda mrefu ni UDOM. Wana umoja wa kusaidiana kwa misingi ya kidini ndani ya ofisi za serikali. Baada ya kuona mtu akitaja SUA, nimefuatilia na kuthibitisha bila shaka kwamba hata wao wameanzisha mfumo huo, tena unachochewa na mmoja wa viongozi wa chuo!

Bahati mbaya dini inayoanzisha mtindo huu ni ya aina moja. Yaonekana kuna 'movement' ya ktk ofisi za serikali na wanaambizana. Hawa UDOM na SUA pamoja na usomi wao, uelewa ni bado.
 
Back
Top Bottom