Tabia 7 za watu waliokulia katika umasikini uliokithiri kisha wakafanikiwa ghafla

Tabia 7 za watu waliokulia katika umasikini uliokithiri kisha wakafanikiwa ghafla

matunduizi

JF-Expert Member
Joined
Aug 20, 2018
Posts
7,968
Reaction score
19,368
Moja kwa moja tuokoe muda maana zamani hizi watu wako bize sana na breaking nyuzzz.

1: Wanadhani utajiri ni kunyenyekewa na kila mtu.
Hawa utakuta bila kupiga Magoti Ndugu, kanisa, msikiti, masikini hapewi msaada.

2: Hofu ya kupoteza ni kubwa kuliko hamasa ya kupata zaidi.
Hii ilimkuta msanii Jack Chein alipoingia Hollywood. Wenzake wakitumia nguo hawazirudii zinachukuliwa kwa ajili ya kusaidia watu. Yeye alikuwa anatunza hadi Nguo za ndani. Kumbuka alitokea China ambako hali ilikuwa mbovu kwa Sera mbovu za babu Yao Mao.

3: Wengi hawawezi kudumu katika hali ya utajiri. Watapambana kutumia hovyo hadi warudi katika umasikini bila kujua. Kumbuka Tyson alikuwa na msafara wa Magari na anasa za kila Aina. Ila ndani ya muda mfupi tu akawa masikini wa kutupwa, madeni anadaiwa kuliko mama wa uswahilini ambaye anadaiwa upatu na vikoba hadi anauziwa madera na wenzake.

4: wanaulimbukeni ambao haujali updates. Gari kwa sababu alinunua Benzi enzi zile nchi nzima wakiwa Wawili tu wenye benzi, basi hata leo ambapo kuna latest version ya Benzi atakomaa tu wakati watu wanamshangaa. Hii tabia alikuwa nayo Prof mmoja UDSM. Anaipenda pijoti yake balaa hadi foronya za siti zimeisha lakini haambiliki.

Kama alinunua suti milioni moja mwaka 90, hadi Leo atakomaa nayo tu hata kama ni bwaga kama zile suruali za ngongoti.

5: Wanaamini utajiri ni wake na sio yeye na familia. Utamkuta anazunguka kwenye mahoteli makubwa anakula vyakula vya thamani, wakati mkewe na watoto huko ni ugali mchicha. Nimewahi kwenda kwa bosi mmoja Mkubwa sana wakati wa msosi tunakula ugali sembe na dagaa zimechanganywa na mchicha. Hakuna matunda, juice wala jamaa halijali balanced diet. Tulikula wote yeye, mkewe, watoto na mfanyakazi. Ila jamaa lilikuwa linazuga tu, huko kazini limeshapakia mavitu ya maana .

6: Huwa ni malimbukeni. Kama alikuwa anasali/swali ataacha, kama alikuwa anapenda kusalimia washkaji anawapiga chini wote. Muda wote wanahisi kulogwalogwa tu.

7: hawana skills za kutafuta watu ambao watakuwa msaada siku wakiishiwa. Wanakuwa wamezungukwa na watu ambao wao wanadhani wanawandesha. Au wanawategemea. Ndio wale ambao wakifulia kila mtu anawakimbia. Anabaki na wale ambao hata akiomba 500 ya kununua dagaa Gengeni hawana. Watu wa maana huwa na connection na watu wa kila kada . hata wakiishiwa bado kuna watu wanaweza kumpa Mawazo,mtaji, njia ili asidhalilike.

Ni hayo tu.
Nimekaa sehemu nimetafakari nikasema ngoja nisikae na haya Maneno Kichwani niwatupie watu wanaofikiri nao wachakate
 
Mwalimu wangu Marehemu Dr. Masumbuko Lamwai, aliwahi kunambia katika kosa kubwa mtu anaweza kufanya ni "KUMPA UONGOZI MTU ALIETOKA KATIKA HALI DUNI KIMAISHA NA AMEPATA ELIMU YEYE PEKE YAKE KATIKA FAMILIA YAKE". Aliseongeza nyama katika sentesi yake baada ya kuona kaniacha njia panda kwasababu ya umri wangu kuwa mdogo, akanambia;

1) Mara nyingi watu hao hujijengea "KIBURI NA JEURI" katika maisha yao.

2) Huwa wanajiona kama "MUNGU WATU" na "KUJISAHAU SANA".

3) Huwa wanajiona "HAWAKOSEI" na wanachukizwa sana "KUKOSOLEWA".

4) Huwa wana "HULKA YA ROHO MBAYA", na kutopendezwa na maendeleo ya wenzao na watu wanaowazidi maarifa na elimu.

5) Huwa wana "UADUI KWA WATU NA KUTOKUAMINI WATU WENGINE".

6) Huongoza taasisi kama vile wanaongoza familia zao wanakotoka.

NB: Hii athari yote hutokana na "KUHESHIMIWA KUPITA KIASI, KUOGOPWA, KUSIKILIZWA SANA HATA WANAPOKOSEA NA KUTUKUZWA" katika familia masikini zao walizotoka.

Nlimwona labda anaongea kwasababu alikua amelewa (alikua mpenzi wa pombe kali). Ila kadri miaka inavyokwenda, naamini maneno yale.
 
Mwalimu wangu Marehemu Dr. Masumbuko Lamwai, aliwahi kunambia katika kosa kubwa mtu anaweza kufanya ni "KUMPA UONGOZI MTU ALIETOKA KATIKA HALI DUNI KIMAISHA NA AMEPATA ELIMU YEYE PEKE YAKE KATIKA FAMILIA YAKE". Aliseongeza

Nlimwona labda anaongea kwasababu alikua amelewa (alikua mpenzi wa pombe kali). Ila kadri miaka inavyokwenda, naamini maneno yale.
Wenzetu waliliona hilo thus ukitoka kwenye umasikini upewi lesseni ya udereva.,utaangusha gari
 
Tusipangiane Maisha Wwe Jamaa!!

Ilisikika kauli ya mlevi mmoja hiv!! Toka Bar!!!!!
 
Kama mother mmoja Anaitwa Martha anahizi tabia zote
 
Tabia ni kama nguo ama rangi zake -- huvaliwa na watu wote. It means, tajiri ama maskini, ilimradi hana HOFU ya Mungu, ni tunda lilelile bovu, bila kujali background. Aiseeee kuna matajiri waliokulia utajirini -- yaani WENGIIIII TUUU -- ni majahili usiseme!!!!
 
Ndo maana kuna mambo nikisikia yule mtoto wa Nyange kayafanya fikra zangu zinahamia kwenye background yake.
 
Aliyekua maskini Kisha akaukwaa utajiri Ni sawa na juha aliyepewa madaraka.

Mifano Ni mingi, kwanza anatafuta imaginary enemy halafu anatesa ukoo au kabila zima la huyo adui wa kuhisi.

Kupenda kukomoa watu na kua haambiliki kisa anahisi ana akili sana. Hata Kama taaluma yake Ni uhasibu utamuona anatoa maelekezo the ma engineer wabobezi. (Sasa wewe usifuate hayo maelekezo )
 
Aisee hao jamaa wa Rombo ndo walivyo wanapokunywa pombe akili zao zinatowa madini makali sana.RIP Masumbuko Lamwai
 
Back
Top Bottom