Tabia hii kwenye vituo vya kutoa huduma za afya haipo sawa

Tabia hii kwenye vituo vya kutoa huduma za afya haipo sawa

vibertz

JF-Expert Member
Joined
Mar 15, 2022
Posts
2,474
Reaction score
4,726
Habarini,

Kuna tabia imejengeka kwenye vituo vya kutolea huduma ya afya (hospitali, zahanati, vituo vya afya) ambapo mteja baada ya kumaliza kuhudumiwa, analazimika kuacha karatasi ambayo ina taarifa za msingi kuhusu mgonjwa husika.

Karatasi hiyo inakuwa na taarifa za aina ya vipimo na majibu ya vipimo lakini unalazimishwa kuacha wanakwambia ni mali yao. Ukiandikiwa dawa basi hospitali zingine wanakulazimisha ununue hapo hapo dawa, hawakupi karatasi ya dawa ili ukanunue kwengine.

Hili jambo ni kumnyima haki mgonjwa kwasababu yeye ana haki ya kununua dawa popote pale anapoona pana unafuu kwake. Msifikirie kibiashara tu bali angalie na utu kwa mgonjwa.

Kwa upande wa karatasi yenye vipimo na majibu ya vipimo pia ni haki ya mgonjwa kupewa kwasababu ataitumia siku nyingine kama reference pindi akienda hospitali nyingine kupata matibabu kuwa kuna huduma ilishawahi kufanyika. Na pia ni muhimu kwa mgonjwa kuweka kumbu kumbu.
 
Hili tatizo lipo kwenye maabara nyingi kama sio zote. Hata ukisema ununue dawa kwao utakuta garama zao ni kubwa kuliko kwingine.... Kuna siku niliandikiwa dawa maabara fulani dodoma nikanunua...ile dawa wao waliuza 15000 ....kumbe nje ya pale ni 6000 tu!
 
Nadhani ni sababu ya kuhakikisha dawa unazopewa na huduma unayopewa ni sawasawa

Ingawa siku hizi kuna visystem kwenye mahospitali yaani tangu umeenda hadi unaondoka hugusi karatasi..

Mm napenda hii mifumo ya kisasa ila mwisho wa siku angalau mgojwa unapaswa kupewa health records zako km kumbukumbu.
 
Japo kila mahali kuna ytaratibu wake lakini ni hako yako kupewa details za matibabu uliyopewa. hvyo unawezaa kumuomba dokta akupe summary ya vipimo na tiba aliyokupa na ukapewa, mfano kwa waliolazwa wakiruhusiwa wanapewa "discharge summary" lakini pia kuna vituo wana utaratibu wa daftari la mgonjwa ambalo linaandikwa kila kitu na unaondoka nalo, kama hawana huo utaratibu basi huweka taarifa zako kwenye file lako na ukiomba wakupe wanatoa.
 
Watanzania kwa asilimia kubwa wanafanana kama watoto wa familia moja, baba, mama mmoja.

Unafiki, majizi, rushwa, dhulma, ujanja ujanja, upumbavu na mengine mabaya.

Hata kama walopewa dhamana ya kuongoza wanaiba watz wanaona sawa tu sababu majizi hayawezi kukemeana.
 
Back
Top Bottom