Artifact Collector
JF-Expert Member
- Mar 7, 2019
- 6,617
- 10,205
Sio ofisin kwenu, ofisi karibia zote za kibongo ziko hivyo maboss wenyewe wanapenda kunyenyekewa na kupelekewa umbeyaYaan kama unanisemelea Mimi
Hiki ndo kipo ofisin kwetu, usipojipendekeza unapigwa chini
Its called pride, pia unajiamini hutaki kufa kinyonge hata kama huna kituMimi tabia yangu ya Kutopenda Unafiki, Ujinga, Utoto, Upuuzi, Upumbavu, Kujikomba na Kuongopa imenifanya nichukiwe sana kuliko hata Shetani.
Kuna wale mpaka wanafunga watu kamba za viatu. Wale jamaa wa kwenye daladala wanao chukua pesa. Wanajua sana kujipendekeza.Ila kujipendekeza ni kipaji.
Kama kawaida baada ya kumaliza chuo nikaingia mtaani kusota na maisha bahati nzuri nikapata intern kwenye moja ya taasisi za serikali zinazolipa vizuri.
Changamoto ikawa kumbe kwenye taasisi hizi za serikali inatakiwa ufanye kazi kwa bidii bila kusahau kujipendekeza kwa boss.Kwa jinsi nilivyo tabia yangu ya kutopenda kujipendekeza wala kufitini wafanyakazi wenzagu mm nikawa natimiza Majukumu kama kawaida.
Kumbe ilitakiwa niwe naenda hata kumuona boss personly angalau mara moja kwa wiki kumsalimia tu ambavyo wengine hufanya sasa mm nawaza nikamuone manager nimweleze nini Cha zaidi wakati meeting za Kila wiki tunakutana na kila mtu anawasilisha ripoti yake?.
Basi bwana boss akaanza kulalamika ooh sina msaada kwenye office ikabidi nifuatilie kujua ninakwama wapi bassi wadau wakanitonya jipendekeze nenda hata mara moja peleka umbea wowote ule atakukubali tu.
Asikwambie mtu hakuna kazi ngumu Kama kuwa mmbeya eneo la kazi Kama hauna tabia hiyo.
Mm nikasema potelea mbali ilimradi natimiza Majukumu yangu na nipo qualified siwezi kujipendekeza kwenye ofsi hii nitapata kazi hata kwingine.
Mkataba wa intern ukaisha boss Kama kawaida akaaniambia nitafute kazi sehemu nyingine.
Mwamba nikaona siyo kesi nikaingia mtaani nikapata kazi kampuni nyingine ya kibongo aisee kule ndo ikawa balaa bila kuwa mbeya humalizi mwezi unatimuliwa boss anataka kila siku mpishane na wafanyakazi ili apate taarifa mara huyu kapeleka fulani mwizi kaiba mafuta, kifusi.
Daah nikaona pia isiwe kesi nikaacha kazi.Sasa Nina mwaka nasota mtaani nimezunguka kinoma hamna kazi kila Kona patupu wadau wanashauri tafuta hata viongozi wa kisiasa ujipendekeze kazi siku hizi kujuana mm naona wananisumbua tu.
Natafuta kazi nikiamini qualifications zangu zitanibeba lakini patupu nimeapply sehemu nyingi hata kuitwa hakuna.
Nikatafuta mpaka sehemu za vibarua patupu. Sasa nawaza hii tabia ya kutojipendekeza nitaachaa vipi maana kubadili tabia ni ngumu kama kubadili ngozi.
Nakujuaga dada angu hutakagi makuu, ila sometimes uchangamke utakosa fursa, [emoji2][emoji2][emoji2][emoji2]Kujipendekeza kipaji Cha kipekee Sana..nilishashindwa na sitakuja kuweza kujipendekeza..never.
Hotel recommendationUpi huo my dear
🤣🤣🤣🤣🤣🤣🤣Nakujuaga dada angu hutakagi makuu, ila sometimes uchangamke utakosa fursa, [emoji2][emoji2][emoji2][emoji2]
Sent from my Infinix X652C using JamiiForums mobile app
Mkuu ukifika kazini fanya kilichokupeleka, habari za kusabahi ni nje huko baada ya muda wa kazi. Mambo ya kusabahi watu ofisini ndio kujipendekeza kwenyewe. Unashindwa kutulia sehemu yako ya kazi unazunguka kusalimia watu, kama sio kujipendekeza ni nini?
Mhh my memory is lost🤒Hotel recommendation
Kwahyo imebdi ujipendekeze...Yaan kama unanisemelea Mimi
Hiki ndo kipo ofisin kwetu, usipojipendekeza unapigwa chini
Ndio mkuu ila daah sijazoea[emoji16]Kwahyo imebdi ujipendekeze...
Mimi kuna kasehem nlikuwa nimejishkiza miez 3 tu wamenichongea baada ya kuwakarbisha geto walitaka kufaham nnapokaa nkaona haina shaka, wakakuta chupa kazaa za spirit kwenye cabin "ooh jamaa mlevi, jamaa anapenda madem ana boksi la ndom, jamaa atakuwa mpiga dili, jamaa kazini anapendeza zaid ya boss" nkapigwa chini unemployed and brokeNdio mkuu ila daah sijazoea[emoji16]
Iko hivi bosi anakua anapelekewa habari zako mbaya, ili upige counter attack inabidi nawewe uwe unajipendekeza kwa boss ndo wengi wanavyofanya hivyoUnajua nimekaa hapa natafakari ya mtoa mada, kwamba kutokujipendekeza kunaweza kuwa sababu ya mtu kukosa kazi, naona kama haliingii akilini, labda kama kuna lingine ambalo mtoa mada anatuficha.
Hakuna anaepinga ya kuwa makazini kuna fitina, ila hakuna watu wanao kubalika makazini kama watu wanao jikubali, wachapa kazi na wasio na tabia ya kuwalamba miguu wakubwa, hili mimi nina ushahidi nalo na mpaka leo kutokana na kujiamini kwangu linanipa ugali, sambamba na kupiga kazi, yaani kazi ya fani yangu ukinipa naipiga mpaka una unafurahi.
Hayo mengine anayo yasema mtoa mada ni sahihi, lakini hili la kujipendekeza kidogo napingana nalo kwa mtindo huo.
Kwa ufupi ajira ni ngumu na upatikanaji wake ni mgumu pia.