Tabora: RC Paulo Chacha amsimamisha kazi Meneja GPSA kwa kutukana wateja

Tabora: RC Paulo Chacha amsimamisha kazi Meneja GPSA kwa kutukana wateja

Mindyou

JF-Expert Member
Joined
Sep 2, 2024
Posts
1,869
Reaction score
4,877
Wakuu,

Mkuu wa Mkoa wa Tabora, Paulo Chacha, amemwagiza Katibu Tawala wa Mkoa kumsimamisha kazi Meneja wa Wakala wa Huduma za Ununuzi Serikalini (GPSA) Mkoa wa Tabora, Mayala Mburi, kutokana na tuhuma za kumtukana matusi wateja waliokwenda kupata huduma za mafuta, akiwemo mtumishi kutoka ofisi ya Waziri Mkuu.

Maagizo hayo aliyatolea wakati alipotembelea ofisi za GPSA mkoani Tabora Jumanne, akiwa ameambatana na Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Mkoa.

RC Chacha alisema kuwa Meneja huyo alikubaliana kuwahudumia watumishi hao wa Waziri Mkuu kwa kuwapatia mafuta, lakini alivyowapokea usiku aliwatukana

Baada ya kudaiwa kutukanwa, watumishi hao walimpigia simu RC Chacha ambaye alimpigia simu meneja huyo. RC naye akatunwa matusi ya nguoni na meneja huyo.

Kwa upande wake Meneja wa GPSA mkoa wa Tabora, Mayala Mburi, akijibu tuhuma hizo ameeleza kilichomsibu mpaka kusababisha kutoa lugha za matusi kwa Mkuu wa Mkoa pamoja na wateja waliofika kituoni kupata huduma ya mafuta .

Katika hatua nyingine, RC Chacha ameagiza kusimamishwa kazi kwa watumishi wawili wa TANROADS Mkoa wa Tabora, Meshack Deogratius na Godfrey Gration, kwa tuhuma za kupokea rushwa kutoka kwa dereva wa gari lililozidisha uzito katika kituo cha kupima uzito cha Turi kilichopo mkoani Tabora.



 
Hivi MAYALA tuliambiwa maana yake nini tena?! 😄

Hapa Kimeumana! 😄 , km kweli ni pombe anapaswa ailaani! Iwe mwiko kwake Mayala! 😄

Ila hii ni fikra zangu tu! Sina mamlaka ya kumpangia! 🤣
 
Kibongo bongo wewe mkuu wa mkoa na watumishi wenzako wa umma kilichowatukana ni pombe alizokunywa Bw Mayala Mburi mtumishi mwenzenu na siyo yeye kama yeye.

Siyo nyie kila siku kila mwaka mnategemea kuongeza kodi zitokanazo na vilevi?sasa mkimtimua huyu akakosa kazi hela za pombe achangie uchumi wa taifa atazitoa wapi?sameheaeni tu mambo yaende.
 
Kibongo bongo wewe mkuu wa mkoa na watumishi wenzako wa umma kilichowatukana ni pombe alizokunywa Bw Mayala Mburi mtumishi mwenzenu na siyo yeye kama yeye.

Siyo nyie kila siku kila mwaka mnategemea kuongeza kodi zitokanazo na vilevi?sasa mkimtimua huyu akakosa kazi hela za pombe achangie uchumi wa taifa atazitoa wapi!
Unajua hii ni serious issue sio utani? Mpaka sasa huyo bwana ategemee kazi hana. Na chain of events ndio imeanza hivyo

Pili unywaji pombe wako usi athiri utendaji wa kazi, either unywe but uweze kutekeleza majukumu (wapo watu wenye uwezo huo)
Or usiguse kabisa

Otherwise taratibu za utumishi ziko wazi
 
Kibongo bongo wewe mkuu wa mkoa na watumishi wenzako wa umma kilichowatukana ni pombe alizokunywa Bw Mayala Mburi mtumishi mwenzenu na siyo yeye kama yeye.

Siyo nyie kila siku kila mwaka mnategemea kuongeza kodi zitokanazo na vilevi?sasa mkimtimua huyu akakosa kazi hela za pombe achangie uchumi wa taifa atazitoa wapi?sameheaeni tu mambo yaende.
Pombe inakupa confidence ya kufanya kile unachohofia kukifanya ukiwa normal.
 
Kibongo bongo wewe mkuu wa mkoa na watumishi wenzako wa umma kilichowatukana ni pombe alizokunywa Bw Mayala Mburi mtumishi mwenzenu na siyo yeye kama yeye.

Siyo nyie kila siku kila mwaka mnategemea kuongeza kodi zitokanazo na vilevi?sasa mkimtimua huyu akakosa kazi hela za pombe achangie uchumi wa taifa atazitoa wapi?sameheaeni tu mambo yaende.
Jamaaa alitamani sana amtukane Mkuu wa mkoa, sasa amemnywea pombe na kutimiza kusudio lake.

Kwake umekuwa mwaka wa kuforce amefunga hesabu mapema🤣🤣🤣
 
Kisa katukana watumishi ofisi ya waziri mkuu? Mbona wananchi tunatukanwa Kila siku.
 
Unajua hii ni serious issue sio utani? Mpaka sasa huyo bwana ategemee kazi hana. Na chain of events ndio imeanza hivyo

Pili unywaji pombe wako usi athiri utendaji wa kazi, either unywe but uweze kutekeleza majukumu (wapo watu wenye uwezo huo)
Or usiguse kabisa

Otherwise taratibu za utumishi ziko wazi
Taratibu za utumishi wa umma zinasemaje mtumishi anapokuwa amemaliza muda wa kazi kwa siku?tukumbuke hayo matusi hakuyatoa mchana muda wa kazi though siujui mkataba wake unasemaje ila kisheria mkuu wa mkoa ndiye ameingilia uhuru wa jamaa.

Kwa sababu simu amepigiwa (na mkuu wa mkoa anakiri) saa tano usiku na huo ni muda kila mtu anafanya yake anayoyajua,kutukana watu kweli ni kosa haipendezi silitetei hilo but waangalie na mazingira yenyewe tukio lilipotokea.
 
kwa bahati mbaya sana, pombe imegarimu wengi, haijawahi kumwacha mtu salama. ona sasa hapo amemtukana mkuu wa mkoa kuwa akome kumpigia akiwa kwenye starehe, kama alivyokoma kunyonya ziwa la mama yake.
 
Back
Top Bottom