DOKEZO Tabora: Wanafunzi wafukuzwa kwa kujirekodi picha za utupu na kuzisambaza

Hili ni dokezo maalum toka kwa mwananchi mtumiaji wa JF mwenye nia ya kuusaidia umma kuwa na taarifa 'maalum'
Malezi hayawezi kuishia Kwa wazazi tutqjidanganya tu
Mtoto ni WA jamii nzima
 
Huo udaktari ataupata kwa kukirekodi picha za uchi ?
Kwani hao watoto wangekuwa wa kwangu ninge ukataza uongozi wa shule isiwafukuze?
Kwanza mtoto wa miaka 14 unamnunulia smartphone ili iweje hasa zaidi ya ushamba na ulimbukeni?

Kama kazi ya kulea mtoto sio ya mzazi pekee mbona mnashinda humu mnawaponda waalimu pale wanapo wapiga bakora watoto kwalengo la kuwarekebisha tabia zao mbaya?
Shule zinaongozwa kwa miongozo ya wizara ya elimu na sio kwa utashi wa mtu binafisi hivyo usilirazimishe mawazo yako ndo yaonekane ni sahihi.
Ww kama unaona hizo sheria sio sahihi mwambie mbunge wako apeleke mswada bungeni ili sheria zibadilishwe.
 
Inabidi wawe na shule zao ili sumu isisambae Kwa watoto wengine
 
Wewe kwenye simu umeona mabaya tu
Hujui Kuna mazuri mengi ya simu,
Kwanini mnaamini mtoto kuwa na simu ni dhambi?

Haki ya misingi ni mtoto apate elimu hata iweje, awe mlemavu, awe Malaya, mlevi n.k
Hakuna sheria ya kutengua mtoto asipate elemu
 
Wewe bibi huyu mama Gwajima kakukosea nn mbona unapenda kumuandama sana
 
Malezi hayawezi kuishia Kwa wazazi tutqjidanganya tu
Mtoto ni WA jamii nzima
Soma uelewe mkuu.
Malezi huanzia nyumbani nikimaanisha maadili ya mtoto huanzia kufundishwa na wazazi wake mzee.
Huko kwenye jamii wataendeleza maadili ambayo mtoto ametoka nayo nyumbani kwa wazazi/walezi wake
 
Kama watarejeshwa Hamuoni kuwa italeta ushawishi Kwa vijana wengine kuweza kufanya Hicho kitendo bila hofu ya kuchukuliwa hatua zozote za kisheria ??

Maana wataona Agghh kumbe ukijirekodi Na video ikivuja basi utaishia kusemwa Tu na kuhamishwa shule
 
Na nyimbo zinazohamasisha ngono wanaziachilia wao wako busy kufungia nyimbo zenye ushawishi harakati za kisiasa?

Pia kutotaja hiyo shule ndio suluhu ya kumaliza tatizo.?
Unataka ukaopoe bebi mapema?
Maana nahisi umeshaona hiyo shule wanavipaji kwenye mambo ya ngono....
 
Hivi huu Ustawi wa Jamii unaona hili Bomu la Kesho au wapo kufanya Now bila kuangalia Kesho....

 
Nikisema ccm ni inyaaa💩 muwe mnaelewa ..

Yani anaejirekodi afukuzwe alaf anaepata na mimba na kuzaa wasamehewe warudi shulen.....hao watoto wamefanya tukio dogo la utoto tu awakustaili hata kupigwa konzi ni kuwaelewesha tu
 
Huu upuuzi wa adhabu za namna hii sijawahi kuelewa mantiki yake, maamuzi ya namna hii yamejaa roho mbaya na mihemuko tu, mtoto mdogo unaona adhabu ya kumfukuza shule???? Kwa maana anapewa adhabu ya kunyimwa haki yake ya elimu???? Hii haina tofauti na adhabu ya kifo. Hii ni kumkomoa kabisaaa kwamba hapewi second chance ya kujirkebisha.
Aliwahi kufanyiwa hvi shemeji yangu akiwa form five kisa tu wamekamatwa usiku walikuwa wametoroka wameenda kuangalia mpira UEFA champions league and the guy was very bright , sasa hvi yupo tu mtaani anaendelea na mishe zingine.

Narudia tena huu ni upuuzi na roho mbayaa
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…