Tafadhali kwa watanzania wanaoishi Marekani pita hapa

Status
Not open for further replies.
Mara nyingi, watu hupenda kuiremba Marekani na barabara safi na majumba makubwa.

Marekani kuna maisha ya kitajiri na kuna maisha duni kama ya Afrika.

Hatuwezi kuifananisha Marekani na Tanzania. Maisha ni tofauti sana kutegemea na elimu ya mtu.

Mtoa mada, kama unategemea kuajiriwa, uwe na elimu inayohitajika na waajiri. Hata kama ni daktari Tanzania, huwezi kuanza kazi bila ya ukaguzi wa vyeti vyako na kama umesona nje ya Marekani, digrii yako huenda isiwe sawa na ya Marekani mpaka ufanye course kadhaa. Hii huchukua muda.

Nakushauri uende peke yako kwanza. Nakushauri usiende Michigan, nenda majimbo ambayo yana kazi zaidi na tajiri zaidi. Michigan ipo hoi kiuchumi. Kwa kuanza, New York, California, Texas.

Nakushauri utafute kazi katika mtandao au usome kazi ziliopo katika mtandao kabla ya kwenda na usome gharama za maisha katika majimbo tofauti yanayolingana na elimu na ujuzi wako.

Tafuta kazi ambazo ni nyingi na rahisi kupata kwa elimu yako. Jisomee mwenyewe.

Maisha kokote ni magumu lakini utafanikiwa mwisho.

Kila la kheri.

Hii pia ni Marekani.





 
Kazi Marekani zipo, as long as una kibali cha kazi, ambacho wewe tayari unacho. Wanaohangaika sana ni wale wasio na vibali. Wee kama mchapa kazi, marekani uta-survive bila tatizo. Unaweza usiishi maisha ya juu kwanza, lakini baadae utakua sawa tuu. Tena una bahati una mwenyeji, you will be fine. Mie nakushauri uende tuu. Vikishindikana, unarudi nyumbani ni nyumbani tuu. Tena huko hata mkeo anaweza pata kazi bila shida. Msichague kazi kwanza.
 
Ulichoongea ni kweli, lakini mie bado sijaona mbongo alieenda Marekani anaeishi kwenye hayo maeneo kwenye picha. Wanaweza kuwa kwenye proverty category, lakini poverty ya Marekani huwezi linganisha na Tanzania. Na masikini wa huko wana misaada ya kila aina, they are very spoiled.
 
yeah hata mbinguni kwa mwenyezimungu kuta matabaka kuna moto,kuna heaven ambazo zinazidiana ubora,kila mtu anakula kulingana na urefu wa mkono wake
 
yeah hata mbinguni kwa mwenyezimungu kuta matabaka kuna moto,kuna heaven ambazo zinazidiana ubora,kila mtu anakula kulingana na urefu wa mkono wake

Nakubaliana na wewe sana tu.

Natajiribu kutoa picha ya ukweli zaidi ya maisha ya nchi za "dunia ya kwanza".

Kuna udanganyifu sana.

The more realistic you are in your expectations, the better you are in preparing your new life.

America ain't the land of milk and honey for everyone, especially the unprepared one. You gotta be prepared to hustle!
 
Mkuu hamuwezi kuwaomba wazazi wako ama wa missus muwaachie mtoto? Yaani mtoto mdogo ni kimbembe kingine with zero income i.e. Matunzo, Medical, sitter wa kumuangalia. Plus despite the good intentions ya huyo mwenyeji wako supporting a family of 3 in principle vs. reality it's two different things. All in all my advice is still the same ideally tangulia wewe then ndio wengine waje. Goodluck! Usisahau kuleta marejesho.
 
Shukrani mkuu
 

Missy,

Nilishaandika huko nyuma kuwa hatuwezi kulinganisha maisha ya nchi tajiri na masikini.

Masikini wa Marekani ni tofauti na wa kwetu.

Mimi siongelei kwa kuangalia CNN. Nimeishi na kusoma Marekani.

Kuna ule msemo wa kuishi "paycheck to paycheck". Yaani ukipokea mshahara, umetumia wote, hamna savings.

Wewe umeshaishi huko? Msaada unategegemea na mshahara na hali ya nyumbani. Marekani siyo Europe, unapewa foodstamps na sehemu ya kulala ukiwa na watoto na usitegemee kuishi upendavyo. Kuna mitaa kila siku ni kupigana risasi. Serikali inakuchunguza sana na unasaidiwa kutokana na shida yako na uwezo wa Serikali. Mambo ya kuzalisha watoto ili ulipwe imeisha na Clinton. Sasa lazima usome ili usaidiwe. Na Msaada ni limited. Kuona daktari inategemea na insurance ya kazini. Vizee vitasaidiwa lakini hospitali ni luxury sio kama Kanada. Wewe kama ni kijana, kupata tiba ya bure sahau unless ni ya dharura au una insurance nzuri kazini.

Masikini wa Marekani are definately NOT spoiled. Ukiniambia wa Kanada au U.K. / Scandinavia, sawa, sio kwa Trump.

Kwa vyoyote, Mimi naamini kuwa kama mtu ni mchapa kazi, atafanikiwa Marekani.

Sijui wewe lakini Mimi nimeshapigwa mizinga na wabongo wengi tu USA. Kuna jamaa namjua anaishi chumba cha bure lakini mlo miwili ni bahati. Ni raia wa Marekani sasa lakini hana kazi ya maana baada ya kuachishwa kazi na kiwanda kuhama China.

Ndiyo maana Trump anasema atatoza kodi kubwa katika bidhaa zao ili viwanda visihame nje.

Marekani huna uhakika kama kesho una ajira au mshahara uliopokea mwezi Jana utaupata mwezi ujao. You need to be flexible and update your resume 24/7.
 
Yeah ni kweli watu sio wa kweli hasa sisi watanzania,ni wabinafsi sana
 
Pamoja sana,
 


Mkuu, you will make it.

Jirani yangu walikuwa na elimu ya sekondari tu. Mke akashinda lottery.

Japokuwa hawana uwezo mkubwa lakini wamefanikiwa kununua nyumba (kwa mkopo) na Wazazi wanafanya kazi walmart na katika gereji ya magari. Wameweza kusoma jioni ili wapate elimu zaidi ya kuwasaidia kupata kazi. Wapo New York.

Watoto wote wamefaulu kusoma Chuo Kikuu.

Utafanikiwa tu. Jipange na jitayarishe kubadilika kimaisha.

Just do your homework.
 
Nimeshriki kama single vipi kuna ugumu hapo na uki apply ya family? Ya na issue iko pale kwenye picha wanaihitaji uipige na jinsi utakavyoonekana kwenye pic kusiwe na makosa
 
Na kuna wabongo walitoka marekani ambako waliishi miaka 13,wakafika bongo na mbwembwe kibao kupanga nyumba mbezi beach dola 1500 kwa mwezi,na nyumba yao ilikuwa hatua za mwisho kuisha,
Baada ya mwaka walifulia ile nyumba walishindwa kulipa kodi,nyumba yao haikuisha na biashara walizoanzisha zilikufa, na ndoa yao ikavunjika...
 
Yeah ni kweli watu sio wa kweli hasa sisi watanzania,ni wabinafsi sana

Mkuu, utamaduni wa watu ni tofauti.

Marekani huwezi kumgongea jirani kuomba chumvi au Msaada wowote. Kila kitu ni kwa appointment. Huwezi kuja kunitembelea bila ya kunijulisha siku kadhaa kabla. Hii sio tabia mbaya bali ni tabia ya wenzetu. Jinsi unavyoishi huwezi kuwa na muda mwingi wa kupiga story. Hamna mwajuma wa kukusaidia kazi za nyumbani. Muda ni pesa huko.

Maisha ni mazuri lakini sio rahisi kama unavyoona katika picha za Hollywood.

Ila naamini kuwa ukijipanga, ukiwa mchapa kazi, ukiwa na elimu bora, utafanikiwa.
 
Life style. Mbwebwe zinataka uwezo. Wee kama mchapa kazi, na mtu simple tuu, you will be more than okay.
 
Status
Not open for further replies.
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…