Tafadhali wadau naomba mnisaidie 5m Tshs nikakomboe hazina

Tafadhali wadau naomba mnisaidie 5m Tshs nikakomboe hazina

Status
Not open for further replies.
Hahahahahaaaa. Ndugu CORAL unajifanya mteule kama wana Israel? Kuokota mana kila siku asubuhi? Usilogwe kutuma pesa huko ndugu. Hata senti moja. Utalia vibaya. Kuna tajiri mmoja huko Tukuyu alilizwa vibaya na watu waliojifanya wako Uingereza. Sasa karudi kijijini analima ndizi na kahawa.
 
Last edited by a moderator:
Ndg mi naweza fanya hii biashara na wewe...kama unaweza ni pm ili tuonane mapema dar es salaama tujue utanilipaje
 
Wewe ni tapeli uliyebobea kwan wanajf wakikuliza swali we ni pm.hizo siyo deal kutaka kuwaibia wenzako,Fanya kazi ili upate kipato halali . Kila kitu unaficha. Mwizi mkubwa we we,tena kama kuna wachungaji tumuombee ana pepo kali
 
Walewale kwenye e mail mtu kafa nitakuhamishia pesa leta acc no ukitoa tu umekwisha katafute vijijini waliolala hupati mtu kana ni wewe pole umeliwa mjomba amka
 
Jamani hii kitu haina utapeli wowote wale nilioongea nao ana kwa ana wamenielewa na hawakuwa na shaka yoyote. Ila walishindwa tu uwezo wa kunisaidia. Nyote mnaokandia kama tungewasiliana nikawapa details mgeweza kuelewa. Hakuna utapeli hapa na mimi sijatapeliwa Wanaijeria hawahusiki kabisa. Labda suala la collateral hilo naona laweza kuwa ndio kikwazo lakini mchakato mzima ni wa halali kabisa. Kuhusu kulipa mara 2 kwani kuna tatizo gani? Sihitaji mkopo wa biashara bali ni kama nilivyoeleza juu. Kwa hiyo tusikokotoe kibiashara. Whoever is interested ani pm I am serious.

Komaa mkuu utadaka hata mmoja humu. Huwezi kuwa na hela kibao huko uingereza halafu 5m inakuzingua hapa bongo. Huko ulaya hiyo pesa uliitengeneza vipi na ukaondoka bila kufanya process yoyote halafu uje ufanyie Mbeya huko. Huyo mwanasheria wako unamlipa nini kama siyo uongo huu.
Siku hizi watu wajanja bana labda wewe ndio umebaki.
 
Huyu mnamuonea bure jamani, yeye si tapeli ila ameingia mikononi mwa 'wapopo'. Atakuwa ameshaliwa kidogo kidogo sasa wazee wa kazi wanataka kumpiga ya ukweli, Bro achana na hiyo mambo, maisha sio mepesi hivyo, fanya kazi kwa bidii achana na hayo mambo sijui mtu alikufa ana hela nyingi bank wanatafuta mrithi, shtuka na uachane nayo

yaaaaani unajua kufikiria wewe......dah....
huyu ndo wa zile email zinazotumwaaaa....halafu katumiwa na wanazidi kumchanganya zaidi......ngoja tusikilizie...
 
Dah!Nimecheka sana, mtu analiwa kichwa hivi hivi!!
 
Aisee huu mchapo nilishapata na walitaka dola 300 ilikutransfer doc kuja kwangu. Alafu kila doc sample ilikuwa original kutoka kwao. Nusu niingie mkenge ila nikashtuka. Nikaomba passport na kuwaambia nitume pesa kwa western union ndio nikagundua mchezo. Sitaki hata sikia hiyo makitu.
Mazee kimbia wasije kukufilisi uanze moja.
Hakuna pesa ya bure....!!😇

Sent from my Samsung Note III using Tapatalk
 
mkuu ungefunguka vizuri kusema kweli maelezo yako yamekaa kama zile barua za wapopo ambazo watu wanazipata kila siku pesa bwana acha kabisa ni kitu kingine kama wadau wanavyosema , pengine ukituma hizo hela we ndo unapigwa jieleze vizuri hapa jf kuna watu wana info za ajabu utasaidiwa tu ...ila pia kama una dhamana inaweza saidia hayo tu
 
hahahaha huyu kakutana nascammer anaambiwa babake aliuawa sijui yuko kambi gani dakar senegal au wale sijui kafariki hahahaha.
atakua ameshaliwa na ametumiwa mi docs anadhan ni halisi eti amewasiliana na lawyer wa mhusika hahaha pole mkui
 
Tatizo hapa mleta mada hataki kufunguka Khs huo mkasa! Ndg km umeamua kuja jukwaani LIVE hebu fafanua hiyo ishu ikoje changamoto utakazopata hapa huenda zikakusaidia! Unasema wee ni mfanyakazi wa Serikali imekuwaje ukawa na mapesa huko uGHAIBUNI kisha ukose 5m yakuyahamisha namna hiyo ndomana watu wanatilia mashaka! Kukutaka useme hapa itakusaidia km umepigwa ili ucpigwe zaidi lkn kwa nmna hii yakutaka PM or CM cdhani km utampata m2 Serious kukusaidia bt kila la heri ndg,,,!
 
Hizi ni issue za Matapeli wa Africa Magharibi na huko imewekwa mitego wanakamatwa hovyo.

Sasa Jamaa hapo juu na njaa zake na kukosa akili ya kufikiria maisha na kuamka na akili za utapeli pori ndio matokeo yake hayo.
Mwenyewe kajipanga kaona ndio njia ya kheir katika maisha na kuona humu wote simple minded people.
Fanyakazi acha ubwete.

Tamaa hizo ndio wengine wanaliwa Tigo huku Pwani kwa kutaka maisha ya urahisi.
Na baadhi ya watu kama nyie ndio mnaingia kwenye mambo yaleee,ukiambiwa Zini na mama yako mnafanya ili mpate pesa kirahisi.


Na kama umeajiriwa Serikalini basi wewe ni Kanjanja,na Ngoja ni trace hii number yako ya VODA nitaanika hapa unaitwa nani na upo wapi,na pia nita trace kwa watu wenye kontacts zako ili kujua hadi kazi unayofanya,then watu wataamua humuhumu Shenzi

Life is how you think in God`s right ways
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom