Tafakuri: Nahodha huyu anaungwa mkono na nani?

Tafakuri: Nahodha huyu anaungwa mkono na nani?

Sexless

JF-Expert Member
Joined
Mar 11, 2017
Posts
23,683
Reaction score
55,898
Yule wa kipindi kilee, aliyependa kusafiri kama Vasco da Gama aliungwa mkono na walioitwa wanamtandao.

Na yule aliyekuwa akipenda kazi na kuongea kwa kujiamini sana aliungwa mkono na abiria waliouchukia ufisadi. Japo baadaye huyu nahodha alibadilika na kuwa katili asiyeelezeka. Akachukiwa na watu wote wakiwemo wa boti yake mwenyewe.

Lakini huyu wa sasa anaungwa mkono na nani? Kwanza kaingia kwa bahati mbaya. Na siyo siri tena kwamba kundi kubwa ndani ya boti yake mwenyewe halikumtaka awe nahodha. Sababu zilizotolewa na kundi hili ni mbili...1. Udhaifu wa kijinsia 2. Anatoka upande wa wachache.

Salama yake ilikuwa ni kuungana na wale wengi waliokuwa wakikwazwa na ukatili na majivuno ya yule nahodha aliyetwaliwa. Lkn pia angepatana na manahodha wa boti shindani.

Haya yangemsaidi kuzima figisu za ndani ya boti yake. Na kumpa uimara ktk unahodha wake

Lakini kwa kuwa kaingia kwa bahati mbaya, hapendwi hata na wale wa boti yake mwenyewe na anarudia makosa ya nahodha aliyetwaliwa basi anajiweka kwenye hatari ya kushindwa kazi mapema sana.
 
Ameingia madarakani kwa mujibu wa katiba ya jamhuri ya muungano wa Tanzania..Katiba iko wazi katika hili....Rais aliyepo madarakani akifa basi makamu wa Rais anatakiwa kuapishwa haraka.....

JPM amekufa kwa mapenzi ya Mungu kama ambayo mimi na wewe tutakufa, Mama kwa mujibu wa katiba ametwaa kiti..
 
Yule wa kipindi kilee, aliyependa kusafiri kama Vasco da Gama aliungwa mkono na walioitwa wanamtandao.

Na yule aliyekuwa akipenda kazi na kuongea kwa kujiamini sana aliungwa mkono na abiria waliouchukia ufisadi. Japo baadaye huyu nahodha alibadilika na kuwa katili asiyeelezeka. Akachukiwa na watu wote wakiwemo wa boti yake mwenyewe.

Lakini huyu wa sasa anaungwa mkono na nani? Kwanza kaingia kwa bahati mbaya. Na siyo siri tena kwamba kundi kubwa ndani ya boti yake mwenyewe halikumtaka awe nahodha. Sababu zilizotolewa na kundi hili ni mbili...1. Udhaifu wa kijinsia 2. Anatoka upande wa wachache.

Salama yake ilikuwa ni kuungana na wale wengi waliokuwa wakikwazwa na ukatili na majivuno ya yule nahodha aliyetwaliwa. Lkn pia angepatana na manahodha wa boti shindani.

Haya yangemsaidi kuzima figisu za ndani ya boti yake. Na kumpa uimara ktk unahodha wake

Lkn kwa kuwa kaingia kwa bahati mbaya, hapendwi hata na wale wa boti yake mwenyewe na anarudia makosa ya nahodha aliyetwaliwa basi anajiweka kwenye hatari ya kushindwa kazi mapema sana.
Sema, wewe ndo ulimchukia Magu plus wafanyabiashara wakwepa kodi, wawekezaji wadanganyifu na baadhi ya wasomi wasio na ajira .....

Hakuna mtu anachukiwa na watu wote.
 
Ilifika kipindi hotuba za jiwe nikawa sizisikilizi kabisa. Nikiiona tu whatsapp naidelete upande wangu.
Sipendagi mtu mwonevu. Nilikuwa sipo tayari kusikiliza matamshi ya uonevu. Mama bado namsikiliza ila kidogo kanishtua baada ya kuamua kuvunja katiba hadharani kwa kuogopa kauri za kuwa anampinga jiwe. Hadi namwonea aibu ,,alivyo hafanani na ukatili.

Sent from my SM-A207F using JamiiForums mobile app
 
Unasemaje kuhusu JPM??

Ulimchukia wewe, sema hivyo!!!
JPM alisababisha mwenyewe achukiwe. Alikuwa mwonevu sana na bahati mbaya wasifuji wake walidhani wanaoudhika na mambo yake ni chadema au wapigaji. Nayeye aliamini hivyo. Basi chuki ikawa inakua siku hadi siku.

Sent from my SM-A207F using JamiiForums mobile app
 
Sema, wewe ndo ulimchukia Magu plus wafanyabiashara wakwepa kodi, wawekezaji wadanganyifu na baadhi ya wasomi wasio na ajira .....

Hakuna mtu anachukiwa na watu wote.
Hakuna mwenye akili timamu ambae alimpenda dikteta
 
Ilifika kipindi hotuba za jiwe nikawa sizisikilizi kabisa. Nikiiona tu whatsapp naidelete upande wangu.
Sipendagi mtu mwonevu. Nilikuwa sipo tayari kusikiliza matamshi ya uonevu. Mama bado namsikiliza ila kidogo kanishtua baada ya kuamua kuvunja katiba hadharani kwa kuogopa kauri za kuwa anampinga jiwe. Hadi namwonea aibu ,,alivyo hafanani na ukatili.

Sent from my SM-A207F using JamiiForums mobile app
Unaidanganya nafsi, haya bhana
 
Wanasema huyu nahodha haendeshi meli, ila meli inaendeshwa kutokea kule kunako mkataba wa mchina.....
 
Back
Top Bottom