Tafakuri: Ni upi hasa unyeti wa Muungano wa Tanganyika na Zanzibar?

Tafakuri: Ni upi hasa unyeti wa Muungano wa Tanganyika na Zanzibar?

Mtoa mada acha unafiki. Unahoji 'unyeti' wa Muungano wetu, wakati huo huo unajifanya kusema huna lengo la kuuvunja bali unataka 'kuuimarisha'. Unaweza kuimarisha kitu ambacho hata hujui 'unyeti' wake? Au hujui maana ya neno 'unyeti'?
Satu, naomba nikuulize swali moja tu...je muungano unaweza kudumu Wazanzibari wakiinyima kura CCM?
 
Satu, naomba nikuulize swali moja tu...je muungano unaweza kudumu Wazanzibari wakiinyima kura CCM?

Kabla sijakujibu, onesha kwanza rangi yako halisi. Unapenda Muungano uwepo na udumu? Kama unapenda Muungano uwepo, kwa nini unahoji 'unyeti' wake kama si mnafiki wewe?

Mimi napenda Muungano wetu na nataka udumu kwa sababu najua 'unyeti' wake.
 
Kwa inavyoonekana huu Muungano uliundwa kwasababu za kimaslahi ya usalama wa Tanganyika, maana Zanzibar iko karibu mno na Tanganyika hvyo Kama kusingekua na Muungano basi ingekua njia rahisi mno ya adui zetu kuingia Tanganyika...
Mtazamo wa kizamani huo usio na uhalisia. vipi mipaka ya nchi sehemu zingine, mbona kwa upande Kenya Mombasa imepakana na Pemba? Au mbona hatukauungana na Burundi au rwanda
 
Mtoa mada acha unafiki. Unahoji 'unyeti' wa Muungano wetu, wakati huo huo unajifanya kusema huna lengo la kuuvunja bali unataka 'kuuimarisha'. Unaweza kuimarisha kitu ambacho hata hujui 'unyeti' wake? Au hujui maana ya neno 'unyeti'?...
Mbona uingereza imejitoa EU?
 
Kwa inavyoonekana huu Muungano uliundwa kwasababu za kimaslahi ya usalama wa Tanganyika, maana Zanzibar iko karibu mno na Tanganyika hvyo Kama kusingekua na Muungano basi ingekua njia rahisi mno ya adui zetu kuingia Tanganyika...
Zanzibar na Kenya au Uganda ni ipi iko karibu? Zanzibar mapka upande boti lakini Kenya, Uganda etc unavuka kwa miguu. Hili suala la kusema adui ataitumia Zanzibar ni porojo tu. BTW siku hizi adui akitaka kukuvamia ni rahisi sana na siyo lazima ategemee kakisiwa kadogo kama Zanzibar.
 
Aliyeanzisha mchakato wa katiba mpya aliliona mapema hili. Lengo mojawapo liikuwa ni kuunusuru Muungano wenyewe hasa baada ya Maalim na Karume kukutana kule Zanzibar na kuunda katiba inayosema Zanzibar ni nchi wakadefine hadi mipaka ya nchi hiyo!

Lakini Magufuli alipoingia madarakani akagoma kuendelea na mchakato wa katiba mpya, matokeo yake Zimwi la kutoukubali Muungano limepewa nguvu mpya!

Serikali itambue tu kuwa Katiba ya mwaka 1977 hasa katika masuala ya muungano haitokidhi matakwa ya Wazanzibari, Na wataendelea kuukataa kwa maneno mpaka hapo watakapoamua kuukataa kwa vitendo!.

Kama tunautaka muungano, basi tuje na katibya mpya sasa hivi, tukijifanya tunafumba macho kisha tukadhani wale tunaowapandikiza Zanzibar tukitokea Dodoma wataulinda muungano kwa niaba yetu ipo siku tutaamka na kukuta maelfu ya Wazanzibar mitaani hawautaki huo muungano, utawafanya nini, utawapiga risasi? —Na muungano utaishia hapo!
 
Kabla sijakujibu, onesha kwanza rangi yako halisi. Unapenda Muungano uwepo na udumu? Kama unapenda Muungano uwepo, kwa nini unahoji 'unyeti' wake kama si mnafiki wewe?

Mimi napenda Muungano wetu na nataka udumu kwa sababu najua 'unyeti' wake.
Satu, Muungano kama ulivyo sasa ni wa kilaghai, ni wa hila na haupo kwa maslahi ya Watanzania wote bali kwa maslahi ya CCM. Kwa jinsi ulivyo, kama CCM haipo, muungano haupo, umekufa.

Satu, utakuwa na akili fupi sana kama hata hili unashindwa kuliona. Unajua kwa nini jeshi linapelekwa Unguja? Inapelekwa kwa sababu Wazanzibari hawaitaki CCM na dalili zipo za kushindwa.

Satu unaniita mnafiki kwa kutaka Muungano uimarishwe na nyufa zilizojitokeza zishughulikiwe. Unaponiita mnafiki sikushangai kwani hata kaswali kadogo sana umeshindwa kujibu, pole.

Satu, huu mjadala unakuzidi kimo.
 
Ngoja nikachukue jembe nikalime mihogo, hata siwaelewi
 
Nchi mbili zikiungana na kuwa nchi moja ni kwamba ama serikali inakuwa moja au zinakuwa tatu. Haijawahi kutokea nchi mbili zikaungana na kuwa nchi moja halafu serikali zikabaki mbili kama ilivyokuwa awali. Hivyo hivyo haijawahi kutokea nchi moja ikawa na Rais wawili, huu ni ulaghai na ni mpango uliobuniwa na CCM ili kuhakikisha inabaku madarakani hata kama inashindwa uchaguzi..
UK ipoje? Prime Minister wa UK ni nani?? Na wa England ni nani?? Na Bunge la UK ni Lipi na la England ni lipi ? Vs lile is Scotland , Ireland na Wales?
 
Chadema wametuletea mgombea wa Urais
 
Kwa ukumbusho tu:
  • Tuanze kwa kukiri kwamba zilizoungana zilikuwa ni nchi mbili, Tanganyika na Zanzibar.
  • Tukiri pia kuwa wakati zinaungana tulikuwa na vyama tawala viwili, TANU na Afro-Shirazi Party (ASP)
  • Pia tukumbushane kwamba wakati zinaungana 1964 bado tulikuwa katika mfumo wa vyama vingi...
Nini unyeti wa Muungano wa UK, USA n.k ukiujua huo utaujua unyeti wa Muungano wetu
 
Tunashukuru Mh Tundu Lissu ameweka wazi kila kitu.
Mkuu, fikiria sasa, ndiyo Sieph kashinda uraisi, na wazanzibari wakavunja muungano,
Nitajie faida moja tu ya Lisu atakayoipata kutokana na kuvunjika muungano,

Nitajie pia faida ya ACT itakayopata kutoka Zanzibar kuja huku bara ikiwa muungano utavunjwa

Na kisha unitajie manufaa ya Chadema yatayapatikana huku bara Baada ya kuvunjika muungano
 
Satu, Muungano kama ulivyo sasa ni wa kilaghai, ni wa hila na haupo kwa maslahi ya Watanzania wote bali kwa maslahi ya CCM. Kwa jinsi ulivyo, kama CCM haipo, muungano haupo, umekufa.

Satu, utakuwa na akili fupi sana kama hata hili unashindwa kuliona. Unajua kwa nini jeshi linapelekwa Unguja? Inapelekwa kwa sababu Wazanzibari hawaitaki CCM na dalili zipo za kushindwa.

Satu unaniita mnafiki kwa kutaka Muungano uimarishwe na nyufa zilizojitokeza zishughulikiwe. Unaponiita mnafiki sikushangai kwani hata kaswali kadogo sana umeshindwa kujibu, pole.

Satu, huu mjadala unakuzidi kimo.

Duuh, umepiga nyundo ya kisogo huyu ndugu...

Niliisoma comment yake hii 👇 👇
Kabla sijakujibu, onesha kwanza rangi yako halisi. Unapenda Muungano uwepo na udumu? Kama unapenda Muungano uwepo, kwa nini unahoji 'unyeti' wake kama si mnafiki wewe?

Mimi napenda Muungano wetu na nataka udumu kwa sababu najua 'unyeti' wake.

Kabla sijaijibu nikaamua kuona watu wengine watamjibu nini. Thank God kuwa, umemjibu vizuri sana na ni kweli kabisa mjadala huu hauwezi, umemzidi kimo kwa mbali sana huyu ndugu...

Kwanza hata hajui hata mahali pa kulitumia neno "mnafiki" au "unafiki". Anadhani linaweza kutumika popote wakati wowote...

Wewe unajaribu kueleza kasoro za muungano na namna ya kuzirekebisha, jamaa anakurupuka kutoka huko alikokuwa bila hata kusoma kwa makini ili kujua logic ya mjadala ndipo aseme/aandike lakini anaishia kusema tu;

" .....acha unafiki" something which is out of the context kabisa....!!

Duuh, MATAGA ni tatizo kwelikweli, wengi zaidi ya 99% ufahamu wao ni below standards....
 
Katiba ya Zanzibar inaruhu kura ya maoni kwa jambo kubwa kama hili ..siku akitangazwa Maalim Seif ajenda kuu ni hio. Nyinyi endeleeni kufuta chaguzi, muibe kura, muikalie Zanzibar kwa mtutu wa bunduki, muwachagulie rais Dodoma lakini siku mkijichanganya tu huu Muungano tunauvunja. HATUUTAKI HATA KUUSIKIA.
 
UK ipoje? Prime Minister wa UK ni nani?? Na wa England ni nani?? Na Bunge la UK ni Lipi na la England ni lipi ? Vs lile is Scotland , Ireland na Wales?

Nini unyeti wa Muungano wa UK, USA n.k ukiujua huo utaujua unyeti wa Muungano wetu
Ndugu yangu August, kwa kweli sikutegema hoja dhaifu kama hizi kutolewa na mtu kama wewe ambaye niliamini unao uelewa wa mambo kwa kiwango cha juu kuliko idadi kubwa ya vijana wa Lumumba walioko humu ndani...au nakosea? Katika utetezi wako unataja UK na unataja USA, are you serious kweli? UK haina Rais, kweli si kweli? USA ina Rais moja kweli si kweli? Tanzania inao Rais wawili, Makamu wa Rais wawili, Waziri wakuu wawili (kumbuka Zanzibar ina Waziri Kiongozi).

Je ndugu yangu August, umewahi kuzipitia Katiba za hizo nchi mbili unazozilinganisha na Tanzania? Hebu kuwa mkweli ndugu yangu, niliuliza swali sijapewa jibu lake hivyo nakupa nafasi unijibu, Je CCM ikikataliwa na kushindwa uchaguzi upande moja wa muungano, huo muungano utaendelea kuwepo? Katika hizo nchi ulizozitolea mfano, je kushindwa kwa chama kilicho madarakani kuna athari gani kwa muungano wao mpaka vyombo vya dola vitumike kulazimisha ushindi kwa chama tawala?
 
Bila muungano hakuna Chama cha Mapinduzi.

Chama cha Mapinduzi hutumika kuyaenzi mapinduzi ya serikali ya Sultani. No Zanzibar in the picture No CCM
Sultani hajawahi kuwa na serikali. Iliyovamiwa na kuangushwa ni serikali iliyokuwa ikiongozwa na Muhammed Shamte wa chama cha ZPPP. Mpemba wa Ole huyo
 
Sultani hajawahi kuwa na serikali. Iliyovamiwa na kuangushwa ni serikali iliyokuwa ikiongozwa na Muhammed Shamte wa chama cha ZPPP. Mpemba wa Ole huyo
Sultani alikuwa kiongozi wa nchi
Mohammed Shamte alikuwa kiongozi wa serikali.
 
Kwa ukumbusho tu:
  • Tuanze kwa kukiri kwamba zilizoungana zilikuwa ni nchi mbili, Tanganyika na Zanzibar.
  • Tukiri pia kuwa wakati zinaungana tulikuwa na vyama tawala viwili, TANU na Afro-Shirazi Party (ASP)
  • Pia tukumbushane kwamba wakati zinaungana 1964 bado tulikuwa katika mfumo wa vyama vingi
  • Awali nchini Tanganyika Tume ilikuwa imeundwa kuangalia uwezekano kufuta mfumo wa vyama vingi
  • Baada ya Muungano hiyo Tume iliimarishwa kwa kuongezewa wajumbe kutoka Zanzibar nao washiriki
  • Tume ilitoa ripoti yake tarehe 22/3/1965 na kuikabidhi katika vikao vya vyama viwili tawala, TANU na ASP
  • Miezi minne baadaye muswada ukawasilishwa bungeni na sheria mpya ya chama kimoja ikapitishwa rasmi
  • Katiba ya muda ndiyo ikatumika katika Uchaguzi Mkuu wa kwanza chini ya mfumo wa chama kimoja 1965
Nchi moja, Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Rais wawili, Rais wa Muungano na Rais wa Zanzibar!
Serikali mbili, Serikali ya Muungano na Serikali ya Zanzibar
Vyombo vya uwakilishi viwili, Bunge na Baraza la Wawakilishi
Bendera mbili, Bendera ya Muungano na Bendera ya Zanzibar
Nyimbo za Taifa mbili, Wimbo wa Taifa na Wimbo wa Zanzibar

Kuna unyeti gani hapa?
Kitu gani kinafichwa hapa?

Kwenye Katiba hakuna kipengele chochote kinachozungumzia nchi itaendeshwaje kama vyama tofauti vitashinda bara na visiwani. Kwa hiyo ni dhahiri chama chochote nje ya CCM hakiwezi kutangazwa mshindi hata kikipata asilimia 95% za kura. Labda ni wakati muafaka wa kujiliza, je kwa nini tunahangaika na kupoteza pesa kugharamia uchaguzi usio huru?

Uchaguzi ambao matokeo yake hayana maana wala umuhimu wowote? Hii ni kwa sababu, kama chama chochote kingine kingekuwa na nafasi ya kutangazwa mshindi, Katiba ilitakiwa itamke wazi kabisa namna vyama tofauti vinavyoweza kuunda serikali na kuliongoza taifa. Bila hivyo ni ulaghai, hila na njama za kuwahadaa Watanzania kwamba nasi eti tuna uhuru!

Labda sasa ni wakati wa kujiuliza, hii CCM imewekeza nini hapa nchini hadi ionekani kwamba Tanzania haiwezekani bila CCM. Kwa sasa tunaona viongozi wanavyoshindana kurithiana vyeo kana kwamba wao peke yao ndio wenye haki zaidi nchini. Kwa mwendo huu hatufiki na ni lazima tubadilike, lazima tutazame mbele na kuachana na mazoea yasiyo na tija kwa taifa.

Mathalani kunaanza tabia ya kutoheshimu hata kanuni na sheria tulizojiwekea kama binadamu, tunaanza kuiona Katiba kama kipande tu cha karatasi kisicho na maana na bila kumung'unya maneno tunaanza kuwa na tabia za wanyama wa mwituni. Wanyama hawana sheria, hawana katiba, hawana ustaarabu...kama una nguvu, kama ni mbabe, kama ni mkatili, yote rukhsa.

Anayehoji unyeti wa Muungano na anayehoji tunakoelekea, si adui hafanyi hivyo kwa kutaka kuuvunja Muungano, hapana, anataka kuuimarisha Muungano kwa sababu anaona hitilafu ambazo zisiposhughulikiwa, Muungano wetu uko hatarini na kuna siku tutasambaratika na kila moja kubeba mbao zake. Amkeni Watanzania, tumedanganywa vya kutosha.
Siku ukivunjika ndo utajua km una umuhimu au laaa!
 
Kwa inavyoonekana huu Muungano uliundwa kwasababu za kimaslahi ya usalama wa Tanganyika, maana Zanzibar iko karibu mno na Tanganyika hvyo Kama kusingekua na Muungano basi ingekua njia rahisi mno ya adui zetu kuingia Tanganyika.

Aliyeuhimiza huu Muungano alijua Kama kusipokua na jeshi moja la kulinda kule Zanzibar na Tanganyika, siku tukiingia katika sintofahamu nao basi inaweza kuruhusu adui kuweka kambi pale na kujaribu kuingia kwa urahisi katika viunga vya Tanganyika.

Sina hakika ila naona lilikua Ni swala la kiusalama zaidi na ndio maana wakaipa kibali kua na Rais ama kiongozi wake ila jeshi liwe moja tu!!!
Hao maadui ambao wataweza kuitumia Zanzibar kuivamia Tanganyika ni kina nani? Mbona hawatajwi?
 
Back
Top Bottom