Satu, naomba nikuulize swali moja tu...je muungano unaweza kudumu Wazanzibari wakiinyima kura CCM?Mtoa mada acha unafiki. Unahoji 'unyeti' wa Muungano wetu, wakati huo huo unajifanya kusema huna lengo la kuuvunja bali unataka 'kuuimarisha'. Unaweza kuimarisha kitu ambacho hata hujui 'unyeti' wake? Au hujui maana ya neno 'unyeti'?
Satu, naomba nikuulize swali moja tu...je muungano unaweza kudumu Wazanzibari wakiinyima kura CCM?
Mtazamo wa kizamani huo usio na uhalisia. vipi mipaka ya nchi sehemu zingine, mbona kwa upande Kenya Mombasa imepakana na Pemba? Au mbona hatukauungana na Burundi au rwandaKwa inavyoonekana huu Muungano uliundwa kwasababu za kimaslahi ya usalama wa Tanganyika, maana Zanzibar iko karibu mno na Tanganyika hvyo Kama kusingekua na Muungano basi ingekua njia rahisi mno ya adui zetu kuingia Tanganyika...
Mbona uingereza imejitoa EU?Mtoa mada acha unafiki. Unahoji 'unyeti' wa Muungano wetu, wakati huo huo unajifanya kusema huna lengo la kuuvunja bali unataka 'kuuimarisha'. Unaweza kuimarisha kitu ambacho hata hujui 'unyeti' wake? Au hujui maana ya neno 'unyeti'?...
Zanzibar na Kenya au Uganda ni ipi iko karibu? Zanzibar mapka upande boti lakini Kenya, Uganda etc unavuka kwa miguu. Hili suala la kusema adui ataitumia Zanzibar ni porojo tu. BTW siku hizi adui akitaka kukuvamia ni rahisi sana na siyo lazima ategemee kakisiwa kadogo kama Zanzibar.Kwa inavyoonekana huu Muungano uliundwa kwasababu za kimaslahi ya usalama wa Tanganyika, maana Zanzibar iko karibu mno na Tanganyika hvyo Kama kusingekua na Muungano basi ingekua njia rahisi mno ya adui zetu kuingia Tanganyika...
Satu, Muungano kama ulivyo sasa ni wa kilaghai, ni wa hila na haupo kwa maslahi ya Watanzania wote bali kwa maslahi ya CCM. Kwa jinsi ulivyo, kama CCM haipo, muungano haupo, umekufa.Kabla sijakujibu, onesha kwanza rangi yako halisi. Unapenda Muungano uwepo na udumu? Kama unapenda Muungano uwepo, kwa nini unahoji 'unyeti' wake kama si mnafiki wewe?
Mimi napenda Muungano wetu na nataka udumu kwa sababu najua 'unyeti' wake.
UK ipoje? Prime Minister wa UK ni nani?? Na wa England ni nani?? Na Bunge la UK ni Lipi na la England ni lipi ? Vs lile is Scotland , Ireland na Wales?Nchi mbili zikiungana na kuwa nchi moja ni kwamba ama serikali inakuwa moja au zinakuwa tatu. Haijawahi kutokea nchi mbili zikaungana na kuwa nchi moja halafu serikali zikabaki mbili kama ilivyokuwa awali. Hivyo hivyo haijawahi kutokea nchi moja ikawa na Rais wawili, huu ni ulaghai na ni mpango uliobuniwa na CCM ili kuhakikisha inabaku madarakani hata kama inashindwa uchaguzi..
Nini unyeti wa Muungano wa UK, USA n.k ukiujua huo utaujua unyeti wa Muungano wetuKwa ukumbusho tu:
- Tuanze kwa kukiri kwamba zilizoungana zilikuwa ni nchi mbili, Tanganyika na Zanzibar.
- Tukiri pia kuwa wakati zinaungana tulikuwa na vyama tawala viwili, TANU na Afro-Shirazi Party (ASP)
- Pia tukumbushane kwamba wakati zinaungana 1964 bado tulikuwa katika mfumo wa vyama vingi...
Mkuu, fikiria sasa, ndiyo Sieph kashinda uraisi, na wazanzibari wakavunja muungano,Tunashukuru Mh Tundu Lissu ameweka wazi kila kitu.
Satu, Muungano kama ulivyo sasa ni wa kilaghai, ni wa hila na haupo kwa maslahi ya Watanzania wote bali kwa maslahi ya CCM. Kwa jinsi ulivyo, kama CCM haipo, muungano haupo, umekufa.
Satu, utakuwa na akili fupi sana kama hata hili unashindwa kuliona. Unajua kwa nini jeshi linapelekwa Unguja? Inapelekwa kwa sababu Wazanzibari hawaitaki CCM na dalili zipo za kushindwa.
Satu unaniita mnafiki kwa kutaka Muungano uimarishwe na nyufa zilizojitokeza zishughulikiwe. Unaponiita mnafiki sikushangai kwani hata kaswali kadogo sana umeshindwa kujibu, pole.
Satu, huu mjadala unakuzidi kimo.
Kabla sijakujibu, onesha kwanza rangi yako halisi. Unapenda Muungano uwepo na udumu? Kama unapenda Muungano uwepo, kwa nini unahoji 'unyeti' wake kama si mnafiki wewe?
Mimi napenda Muungano wetu na nataka udumu kwa sababu najua 'unyeti' wake.
UK ipoje? Prime Minister wa UK ni nani?? Na wa England ni nani?? Na Bunge la UK ni Lipi na la England ni lipi ? Vs lile is Scotland , Ireland na Wales?
Ndugu yangu August, kwa kweli sikutegema hoja dhaifu kama hizi kutolewa na mtu kama wewe ambaye niliamini unao uelewa wa mambo kwa kiwango cha juu kuliko idadi kubwa ya vijana wa Lumumba walioko humu ndani...au nakosea? Katika utetezi wako unataja UK na unataja USA, are you serious kweli? UK haina Rais, kweli si kweli? USA ina Rais moja kweli si kweli? Tanzania inao Rais wawili, Makamu wa Rais wawili, Waziri wakuu wawili (kumbuka Zanzibar ina Waziri Kiongozi).Nini unyeti wa Muungano wa UK, USA n.k ukiujua huo utaujua unyeti wa Muungano wetu
Sultani hajawahi kuwa na serikali. Iliyovamiwa na kuangushwa ni serikali iliyokuwa ikiongozwa na Muhammed Shamte wa chama cha ZPPP. Mpemba wa Ole huyoBila muungano hakuna Chama cha Mapinduzi.
Chama cha Mapinduzi hutumika kuyaenzi mapinduzi ya serikali ya Sultani. No Zanzibar in the picture No CCM
Sultani alikuwa kiongozi wa nchiSultani hajawahi kuwa na serikali. Iliyovamiwa na kuangushwa ni serikali iliyokuwa ikiongozwa na Muhammed Shamte wa chama cha ZPPP. Mpemba wa Ole huyo
Siku ukivunjika ndo utajua km una umuhimu au laaa!Kwa ukumbusho tu:
Nchi moja, Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
- Tuanze kwa kukiri kwamba zilizoungana zilikuwa ni nchi mbili, Tanganyika na Zanzibar.
- Tukiri pia kuwa wakati zinaungana tulikuwa na vyama tawala viwili, TANU na Afro-Shirazi Party (ASP)
- Pia tukumbushane kwamba wakati zinaungana 1964 bado tulikuwa katika mfumo wa vyama vingi
- Awali nchini Tanganyika Tume ilikuwa imeundwa kuangalia uwezekano kufuta mfumo wa vyama vingi
- Baada ya Muungano hiyo Tume iliimarishwa kwa kuongezewa wajumbe kutoka Zanzibar nao washiriki
- Tume ilitoa ripoti yake tarehe 22/3/1965 na kuikabidhi katika vikao vya vyama viwili tawala, TANU na ASP
- Miezi minne baadaye muswada ukawasilishwa bungeni na sheria mpya ya chama kimoja ikapitishwa rasmi
- Katiba ya muda ndiyo ikatumika katika Uchaguzi Mkuu wa kwanza chini ya mfumo wa chama kimoja 1965
Rais wawili, Rais wa Muungano na Rais wa Zanzibar!
Serikali mbili, Serikali ya Muungano na Serikali ya Zanzibar
Vyombo vya uwakilishi viwili, Bunge na Baraza la Wawakilishi
Bendera mbili, Bendera ya Muungano na Bendera ya Zanzibar
Nyimbo za Taifa mbili, Wimbo wa Taifa na Wimbo wa Zanzibar
Kuna unyeti gani hapa?
Kitu gani kinafichwa hapa?
Kwenye Katiba hakuna kipengele chochote kinachozungumzia nchi itaendeshwaje kama vyama tofauti vitashinda bara na visiwani. Kwa hiyo ni dhahiri chama chochote nje ya CCM hakiwezi kutangazwa mshindi hata kikipata asilimia 95% za kura. Labda ni wakati muafaka wa kujiliza, je kwa nini tunahangaika na kupoteza pesa kugharamia uchaguzi usio huru?
Uchaguzi ambao matokeo yake hayana maana wala umuhimu wowote? Hii ni kwa sababu, kama chama chochote kingine kingekuwa na nafasi ya kutangazwa mshindi, Katiba ilitakiwa itamke wazi kabisa namna vyama tofauti vinavyoweza kuunda serikali na kuliongoza taifa. Bila hivyo ni ulaghai, hila na njama za kuwahadaa Watanzania kwamba nasi eti tuna uhuru!
Labda sasa ni wakati wa kujiuliza, hii CCM imewekeza nini hapa nchini hadi ionekani kwamba Tanzania haiwezekani bila CCM. Kwa sasa tunaona viongozi wanavyoshindana kurithiana vyeo kana kwamba wao peke yao ndio wenye haki zaidi nchini. Kwa mwendo huu hatufiki na ni lazima tubadilike, lazima tutazame mbele na kuachana na mazoea yasiyo na tija kwa taifa.
Mathalani kunaanza tabia ya kutoheshimu hata kanuni na sheria tulizojiwekea kama binadamu, tunaanza kuiona Katiba kama kipande tu cha karatasi kisicho na maana na bila kumung'unya maneno tunaanza kuwa na tabia za wanyama wa mwituni. Wanyama hawana sheria, hawana katiba, hawana ustaarabu...kama una nguvu, kama ni mbabe, kama ni mkatili, yote rukhsa.
Anayehoji unyeti wa Muungano na anayehoji tunakoelekea, si adui hafanyi hivyo kwa kutaka kuuvunja Muungano, hapana, anataka kuuimarisha Muungano kwa sababu anaona hitilafu ambazo zisiposhughulikiwa, Muungano wetu uko hatarini na kuna siku tutasambaratika na kila moja kubeba mbao zake. Amkeni Watanzania, tumedanganywa vya kutosha.
Hao maadui ambao wataweza kuitumia Zanzibar kuivamia Tanganyika ni kina nani? Mbona hawatajwi?Kwa inavyoonekana huu Muungano uliundwa kwasababu za kimaslahi ya usalama wa Tanganyika, maana Zanzibar iko karibu mno na Tanganyika hvyo Kama kusingekua na Muungano basi ingekua njia rahisi mno ya adui zetu kuingia Tanganyika.
Aliyeuhimiza huu Muungano alijua Kama kusipokua na jeshi moja la kulinda kule Zanzibar na Tanganyika, siku tukiingia katika sintofahamu nao basi inaweza kuruhusu adui kuweka kambi pale na kujaribu kuingia kwa urahisi katika viunga vya Tanganyika.
Sina hakika ila naona lilikua Ni swala la kiusalama zaidi na ndio maana wakaipa kibali kua na Rais ama kiongozi wake ila jeshi liwe moja tu!!!