Tafakuri ya FaizaFoxy 6: Dar Es Salaam na Tanzania ya zamani, tukumbushane...

Wengine tumekulia vijijini ninachokumbuka ni uwepo wa nyasi ndefu, miti kibao na vichaka vilivyohifadhi wanyama kama sungura na swala, mito yenye samaki wa kutosha, mazao tele shambani, maziwa tele tunakunywa.

Bila kusahau kuogelea mtoni ukirudi nyumbani uso umekakamaa huwezi hata kumzomea mwenzio😆.
 
Vichapizi bado hujaacha tu..

Basi la ghorofa lilienda mwisho ilala. .

Pia university of Dar es salaam walikuwa nalo
 
Kama mtu anakumbuka mahandaki ya ardhini Mmnazi mmoja..

Na ile sauti ya tindo ikitangaza muda majira ya saa ukipiga simu za kuzungusha
Nayakumbuka nadhani yapo ilipo ofisi za magazeti ya CCM kwa sasa. Au sijuwi waliyafukia yale. Karibu kabisa na nyumbani kwetu.
 
Vichapizi bado hujaacha tu..

Basi la ghorofa lilienda mwisho ilala. .

Pia university of Dar es salaam walikuwa nalo
Sim ipo kwenye fast charge na mie naitumia, inakuwa tatizo. Ntajirekebisha.
 
Eleza ya kwenu, hapa si jukwaa la siasa, jimwage tu.
Hahahaaa haya bana kwetu kuzuriii huwa naenda kila ifikapo December huku dar es salaam tumefuata rizki tu heleri laiti kama ile falsafa ya Hayati Nyerere apumzike kwa Amani ingeendelea ya viwanda kila mkoa hee huku dar ningekuja kufuata nini kwa mfano kama nikushangaa bahari ningeishia Tanga

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Miye ndiyo nimekuja Dar nimekosa Abood k'koo nkapanda zangu pale manzese msufini.
 
Nnakumbuka mtaa wa Zanaki na Libya kuna Daktari mwanamke wa.Kihindi tukienda kutibiwa, Akisha kupima tu pipi.

Hivi kwanini siku hizi madaktari hawatumii "stethoscope"? Sijawahi kwenda hospital enzi hizo bila kupimwa joto na "thermometer" na bila kupimwa kitua na "stethoscope".

Hivi madaktari wa siku hiz bado wanatumia "stethoscope" kila mkienda kupimwa au wanazinweka show tu shingoni?
 
Yeah ehe nakumbuka maisha ya pale mtaa wa Narung`ombe yalikuwa safi safi,magari ya city yanazoa taka kila baada ya siku mbili,wakati wa mfungo waisalaam kwa wakiristo hasa watoto wote tunafuturu pale msikiti wa Mahiwa(Cul de sac),namkumbukla mwl.Mama pale kinondoni shule ya Msingi!,mmm Mnazi mmoja Primary School mara mbili kwa wiki chakula kinatolewa shuleni(USAID),Azania,Tambaza,Jangwani,Kisutu top schools in Dar(mmmmm Forodhani sec nayo ndani ya list hii),mechi ya mpira kati ya Tambaza na Kinondoni sec,Dar inasimama kwa muda !!,nchi wakati ina heshima na adabu.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…