Tafuta pesa mpaka akifa mbwa wako watu wakupe salamu za pole na kukutumia rambirambi

TheDreamer Thebeliever

JF-Expert Member
Joined
Feb 26, 2018
Posts
2,490
Reaction score
3,584
Habari wadau!

Maisha sio fair, watu pia hawapo fair.
Inabidi kutafuta pesa mpaka akifa mbwa wako watu wakupe salamu za pole na kukutumia rambirambi.

Leo hii kuna watu walipata ajari kwenye gari moja au ndege moja na watu maarufu lakini vifo vyao havikutangazwa.

Mwaka 2020 unaisha na mimi nakubali hakuna nililofanya zaidi ya ku comment R.I.P kwenye post za matajiri waliokufa kama R.Mengi, Ruge, Patel n.k.


Lakini 2021 naahidi kupambana mpaka siku mbwa wangu akifa nitumiwe salamu za pole.

Uzi teyari
πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚
 
Wenye pesa pia wanatamani vitu vingine
Ambavyo masikini wanavyo lakini havipatikan Kwa pesa..

Afya
Time..
Kupendwa na watu..
Usingizi stress free..
Watu kutokuwa na expectations kubwa na wewe
Wasiwasi WA kuibiwa na kutapeliwa.
Kutopewa heshima bandia..
Mapenzi bandia..n.k n.k
 
Wenye pesa pia wanatamani vitu vingine
Ambavyo masikini wanavyo lakini havipatikan Kwa pesa..

Afya
Time..
Kupendwa na watu..
Usingizi stress free..
Watu kutokuwa na expectations kubwa na wewe
Wasiwasi WA kuibiwa na kutapeliwa.
Kutopewa heshima bandia..
Mapenzi bandia..n.k n.k
 
Pesa ndio kila kitu baba inanunua hivyo vyote
 
Huwa nikiona comment yako, najua ni busara na hekima tupu, hujawahi kukosea.
 
Uzi wa kiboya sana
 
Dahh ila huenda ina ukweli maana Lewis Hamilton yule dereva wa formula 1 ana mbwa wake anaitwa Roscoe.Nilisoma gazeti moja kamfungulia page yake instagram sijui wapi mbwa peke yake ana wafuasi laki 3. Sasa mbwa ana wafuasi laki na kitu kwenye page yake ana nini hasa cha maana umfuate yote ni pesa tu kwa sababu bwana wake ni mtu mkubwa na ana pesa ataposti chochote watu watashare na wata like.Ni kama kile kisa cha yule tajiri kule Misri mbwa wake kafa akaandaa shughuli watu wakala akamnunulia jeneza la kioo akamzika, wananchi wakakasirika wakaenda kumshitaki kwa mkuu wa mji huyu bwana anafanya vibaya anachezea pesa kisa mbwa wake kafa,mkuu wa kijiji akasema haiwezekani lazima nikamtie adabu huyo mtu akachukua bakora yake anataka ampige tajiri.Tajiri akamtuliza mkuu wa kijiji akamwambia mkuu sikiliza mbwa wangu aliniambia akifa hizi pesa nifanye shughuli na nyengine nikupe wewe sasa unakuja na bakora unataka unichape si utazikosa?,mkuu wa kjjiji kusikia pesa halafu ilikuwa karibu kama dola milioni hivi akauliza marehemu kasemaje?[emoji16][emoji16][emoji16][emoji16].pesa acha tutafute pesa ona sasa mkuu wa kijiji bado kidogo asema Mungu amlaze marehemu mahala pema peponi.
 
Mkuu umewaza mbali sana.
Huwa nawaangaliaga Directors/Owners wa makampuni maisha wanayoishi hadi nawaoneaga huruma yaani.
Hawanaga muda wa kurelax yaani masaa 24 vichwa vyao viko bize wanawaza jinsi ya kulinda utajiri,usalama wao na ushindani wa kibiashara.
Yaani kiufupi hawapati usingizi kama sisi,unakuta nyumba yake mwenyewe anaiogopa kulala mpaka anabuni mbinu za kubadili sehemu za kulala kila siku mara lodge,mara aache gari yake nyumbani akodi taxi ili mradi kuwazubaisha wabaya.
 
Watu wamekufa 2019 wewe unaitumia 2020 kuandika R.i.p, wewe si chapati ya dengu wewe
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…