TAHADHARI kwa mnaotaka kuanzisha biashara nchini Tanzania kwa sasa!

TAHADHARI kwa mnaotaka kuanzisha biashara nchini Tanzania kwa sasa!

Ungeongezea pia kwa kuwaonya wale wanaoenda kuchukua mkopo benki na kuweka dhamana nyumba... Wategemee kulala nje siku si nyingi...
 
Biashara mkuu hatuachi,, lazima tuendelee tu hata kama wakituua lazima tufanye, maana 2020 haiko mbali tushuhudie jamaa anavyorukaruka kichura chura!! Lazima betri zilegee safari hiyo!!
 
Habari za muda wanajamvi,
Wahenga walinena Tahadhari kabla ya hatari au vilevile Kinga ni bora kuliko tiba, basi nami naomba nianze kutoa tahadhari kama ifuatavyo.

Najua ni watanzania wengi wenye nia ya kuanzisha biashara ili kuweza kujikwamua kiuchumi, lakini pia kuna mambo ya kuzingatia kabla ya kuamua kuanzisha biashara yeyote ile ili iweze kuwa biashara yenye mafanikio.

Kwa hali ya nchi yetu ilivyo kwa sasa inamlazimu mtu anaetaka kuanzisha biashara kutafakari kwa kina zaidi juu ya changamoto zinazoikumba sekta ya biashara na uchumi kwa ujumla nchini.

Kwa ufupi tu nianze kwa kusema mzunguko wa pesa nchini umedhoofika kama si kupungua sana hadi kufikia kiwango ambacho kimeanza kutupa hofu wananchi mfano mzuri ni jinsi tunavyoona wafanyabiashara wanavyolalamika kwamba mauzo yamepungua sana kwa zaidi ya asilimia 50 yaani kama mwaka 2015 mtu alikuwa anaweza kuuza mpaka sh. ml 1 kwa siku basi sasa kupata tu laki 5 imekuwa ni kama ndoto. Msingi wa biashara yoyote ile ni wateja, sasa hivi wateja(wananchi) hawana pesa maana yake ni kwamba biashara lazima ife.

Kwa wewe unaepanga kufungua biashara kwa kipindi hiki embu jaribu kuanzisha biashara ambayo wateja watakuwa wana uhitaji wa bidhaa yako iwe ni kwa hiari au lazima. mfano Biashara ya chakula, mtu hawezi kuacha kula hata uchumi ushuke kufikia zero. n.k

Sina nia ya kumkatisha mtu tamaa ila nimejaribu kueleza kile nikionacho mm, nakaribisha maoni na sikatai kukosolewa, Ahsanteni.
exactly.umepigilia yani
 
Usisahau na maduka ya dawa maana kuumwa kupo pale pale tena yawezekana awamu hii watu wakaumwa zaidi[emoji5][emoji5]
Duuuuu.......INAWEZA KUWA AWAMU YA KUUMWA....Mungu aepushie mbali kwa kweli
 
Mkuu nikwel anachoongea jamaa me mwenyewe ni mfanya Biashara nakuhakishia sasa hivi mauzo yamepungua kwa zaidi ya 60% mkuu
Achana na huyo inawezekana katika maisha yake hajawahi kufanya biashara halafu anaanza kupiga porojo


Watu wanashauriana yeye anakuja na bla bla zake

Mimi mwenyewe nilikuwa na mpango wa kuanzisha biashara lakini nimesita nafikiria kwa umakini
 
Zimbabwe yenyewe ambayo uchumi wake ushakufa lakini watu bado wanafanya biashara, sembuse nchi bikra kama bongo, miporojo kibao tena iliyojaa mihemko ya kibavicha
Uvivu unamsumbua, ukosefu wa ubunifu!
 
Zimbabwe yenyewe ambayo uchumi wake ushakufa lakini watu bado wanafanya biashara, sembuse nchi bikra kama bongo, miporojo kibao tena iliyojaa mihemko ya kibavicha
Ila kuheshimu mawazo yake ni vizuri pia,kumbuka ilala biashara nyingi zimekufa.
 
Ila kuheshimu mawazo yake ni vizuri pia,kumbuka ilala biashara nyingi zimekufa.
Pia,jana nimepita katikati ya mji wa Morogoro na kuuliza bidhaa moja maduka yote na sikupata,Mhindi mmoja akaniambia Biashara ni mbaya sana,haamini kama huyu Rais na mfumo wake vitadumu muda gani.Mimi mwenyewe nikamwambia usiseme makazini ni kwema,Kuna shida isiyo ya kawaida Rais ni kama anongoza wanyama Serengeti wanapohama kwenda Kenya.
 
Ila kuheshimu mawazo yake ni vizuri pia,kumbuka ilala biashara nyingi zimekufa.
Ila ILALA ni halmashauri zake zinaongozwa na upinzani kwanini wasiwawekee watu unafuu wa ushuru maana tunaaminishwa ndio wakombozi wa shida zote
 
Nlivoona heading nkajua kuna point ztaongelewa apa, wakati huu ndo ule mda watu wanasema matatizo ni mengi kwahio opportunities nazo ni nyingi, wakati unaendelea kuwaambia sio wakati mzuri wa kuanzisha biashara watu walishawaza jinsi ya kutengeneza ela nyingi sana tena naona saahv hadi betting wana branch karibia kila kona, CRDB waliotangaza hasara ndio kwanza wanaongeza matawi na kuajiri watu wengi zaidi, juzi apa mwananchi kama ulisoma kuna benki wametangaza faida ya mabilion inaonyesha jinsi gan hujawahi shika bishara yoyote, USISHAURI WATU UJINGA
 
Habari za muda wanajamvi,
Wahenga walinena Tahadhari kabla ya hatari au vilevile Kinga ni bora kuliko tiba, basi nami naomba nianze kutoa tahadhari kama ifuatavyo.

Najua ni watanzania wengi wenye nia ya kuanzisha biashara ili kuweza kujikwamua kiuchumi, lakini pia kuna mambo ya kuzingatia kabla ya kuamua kuanzisha biashara yeyote ile ili iweze kuwa biashara yenye mafanikio.

Kwa hali ya nchi yetu ilivyo kwa sasa inamlazimu mtu anaetaka kuanzisha biashara kutafakari kwa kina zaidi juu ya changamoto zinazoikumba sekta ya biashara na uchumi kwa ujumla nchini.

Kwa ufupi tu nianze kwa kusema mzunguko wa pesa nchini umedhoofika kama si kupungua sana hadi kufikia kiwango ambacho kimeanza kutupa hofu wananchi mfano mzuri ni jinsi tunavyoona wafanyabiashara wanavyolalamika kwamba mauzo yamepungua sana kwa zaidi ya asilimia 50 yaani kama mwaka 2015 mtu alikuwa anaweza kuuza mpaka sh. ml 1 kwa siku basi sasa kupata tu laki 5 imekuwa ni kama ndoto. Msingi wa biashara yoyote ile ni wateja, sasa hivi wateja(wananchi) hawana pesa maana yake ni kwamba biashara lazima ife.

Kwa wewe unaepanga kufungua biashara kwa kipindi hiki embu jaribu kuanzisha biashara ambayo wateja watakuwa wana uhitaji wa bidhaa yako iwe ni kwa hiari au lazima. mfano Biashara ya chakula, mtu hawezi kuacha kula hata uchumi ushuke kufikia zero. n.k

Sina nia ya kumkatisha mtu tamaa ila nimejaribu kueleza kile nikionacho mm, nakaribisha maoni na sikatai kukosolewa, Ahsanteni.
Ushauri ni mzuri
 
Back
Top Bottom