Tahadhari kwa Waislam waliofunga

mende 2014

JF-Expert Member
Joined
Apr 13, 2014
Posts
763
Reaction score
131
Dokta Adeeb wa Hospitali ya Karachi, ambaye ni mtaalamu wa figo, ametoa tamko kwa kila mtu kutokunywa vinywaji vya baridi kama Pepsi, Cocacola,7up na nyinginezo wakati wa kufungua SWAUMU kutokana na kwamba kufunga kwa muda mrefu kunasababisha kukauka maji kwenye figo.

Hivyo kunywa vinywaji vya baridi na vyenye kemikali vinasababisha matatizo ya figo. Kwahiyo usinywe kinywaji chochote cha baridi wakati wa kufungua. Tumia maji au fresh juice.

Tafadhali sambaza ujumbe huu kwa ndugu, jamaa na marafiki.
 
Aisee, Je kuna uthibitisho wowote wa kitaalam au....
 
Kuna uhusiano gani kati ya post na hiyo attachment yako?
 
Nilijua Ataelezea Vipi Unaweza Ukapata Hayo Magonjwa Ya Figo Ili Hata Angeogopa Na Kuacha Mara Moja
 
Pamoja na kuwa huenda hakukuwa na tafiti za kisayansi. Ndio maana ufunguaji wao huanza kwa uji kma sikosei. Kwa hiyo hilo automatically limezingatiwa lakini si vibaya kukumbushwa.
 
Aisee, Je kuna uthibitisho wowote wa kitaalam au....

Mtume Muhammad(S.A.W) ameshatuambia tufungue na nini,wakati wa kufunga
Imepokewa kutoka kwa Anas-Allah amuie radhi-amesema:"Mtume wa Allah- Rehema na Amani zimshukie-alikuwa akifuturu kwa tende mbichi (zisizo kavu)kabla ya kuswali.Kama hakupata tende mbichi (hufuturu kwa) tende kavu na kama hazipo hizo tende kavu (hufuturu)kwa mafunda ya maji. Imam Ahmad-Allah amrehem.

Katika hadithi nyingine: Amesema;
"Atakapofuturu mmoja wenu,basi na afuturu kwa tende,kwani hizo ni baraka na asiyezipata basi na afuturu kwa (kunywa) maji twahara.
Elimu za sayansi leo zimethibitisha kuwa katika tunda,tende kunapatikana viinilishe na vitamin A,VitaminC,Thiamine (B1),Riboflavin (B2),Niacin,Folic Acid,Iron,Zinc,Protein,Sodium,Calcium na Phosphorous ambavyo vyote hivi vina manufaa makubwa katika mwili wa binadamu
 
Hii mkuu hata ikiwa bila kufungua huwezi kuanza ku breakfast kwa vinywaji hivyo.Maana vinakuta vigo lipo active sana na sensitive sana muda huo.

Figo ni Janga,ungetaka kujua ungeenda siku ya Figo duniani,ndio ungejua hali inavyotisha,maana pale walienda watu wanaojiona wapo fiti sana kupima hivi wanaambia ngoma moja haipo sawa.Na wapo walioenda wakiwa wanaumwa kwa kuangalia kama ni Figo wengine wakaambiwa wapo sawa.

Hali ya Tatizo la igo inatisha,na idadi ya watu kutokupenda kunywa maji nayo pia inatisha..
 
Umejibu mleta post vizuri sana.
JazakAllah Khair

Ni makosa makubwa kufungua kwa kuingiza sumu mwilini,kama vile kufungua kwa kuvuta sigara,kula mishikaki au vyakula vingine vilivyopikwa na mafuta mengi.Aidha,mtu anayefunga anatakiwa,si tu kula vyakula vya asili,bali pia kula kwa kiasi na sio kula kupita kiasi kwa lengo la kufidia mlo wa mchana kutwa.

Moja ya matunda bora kwa kufungulia ni tende,tumia tende kufungulia kwani zina faida lukuki kama nilivyoeleza huko nyuma.

Nimetumia jina lako spice(nikijiwa wazi unaujuwa uislamu vizuri) kuwaafahamisha wasiojuwa uislamu ni mfumo kamili wa maisha,Tumeletewa funga,na maelekezo ya kufunga,sio tumeambiwa tufunge tu,funga ina maelekezo yake.
 
Nakushukuru mtoa mada lkn kufunga si ni kila mtu anafunga?,iwe kwasababu za kiimani au kwasababu binafsi,basi utaratibu huo ni mzuri kiafya.
 
..Nashuudia kwamba huu Uislam wenu ni dini ya haki kabisa

Wanaotaka kuufahamu uislamu wasome vyanzo vya habari vya kiislamu sio vya wababaishaji wasiojuwa uislamu au wanapotosha makusudi,kila ibada inayofanyika ndani ya uislamu ina maelekezo yake,na faida zake,

1.Swala kwa waislamu,ni tendo la mazoezi kwa viungo kwa siku mara tano,maskini,tajiri,mfalme,rangi tofauti wote wanaswali pamoja na kugusana.,.(Yapo maelezo yake kwa urefu)

2. Kufunga ni tendo la Afya, Mtume Muhammad (S.A.W) asema Fungeni mpate Afya. (Yapo maelezo kwa urefu).

3. Kuhiji ni tendo la kukutana waislamu wa dunia nzima mwaka Mara moja,imejumuisha mazoezi,afya,semina,makongamano,kubadilishana mawazo, kusaidia maskini, kuangalia neema za uumbaji wa Allah,kwa kukutana watu,makabila,rangi tofauti,matajiri,maskini, Wenye
Vyeo,wasio na vyeo nk(Yapo maelezo kwa urefu).

4. Maziko ya kiislamu
a. Tajiri na maskini wanazikwa kisawasawa
b. Tajiri,maskini,mfalme wote wanazikwa na kuvalishwa sanda aina moja.
c. Wote wanazikwa kwenye kaburi na kuguswa na michanga bila kujali utajiri,rangi,cheo,umaskini wa maiti.
 
Kikwajuni One

Mtume alikuwa anafuturu kwa sababu ya hizo vitamini au kwa sababu kulikuwapo tu na tende?
 
Last edited by a moderator:
Mtume alikuwa anafuturu kwa sababu ya hizo vitamini au kwa sababu kulikuwapo tu na tende?
Kama ingekuwa ni tende tu ndio iliyokuwapo asingesema wafunguwe kwa tende,lakini yaonyesha wazi mpaka akasema wafunguwe kwa tende,kulikuwapo na vingine.
 
Kikwajuni One

Mtume alikuwa anafuturu kwa sababu ya hizo vitamini au kwa sababu kulikuwapo tu na tende?

Alisema hivyo kutokana na mazingira yake zilikua nyingi na ndipo zilimwapo sanaa,sasa cha ajabu umkaririshe mtanzania eti afungulie tende ,tumia vinavyokuzunguka cha msingi zingatia afya ya mwili
 
Last edited by a moderator:
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…