Tahadhari kwa wanaotaka kuingia kwenye biashara ya kilimo

Tahadhari kwa wanaotaka kuingia kwenye biashara ya kilimo

Mleta mada umetoa ushauri mzuri; achana na huyo mpuuzi analeta matusi kwenye mada muhimu kama hii. Ushauri wako nimeukubali sana. In fact, hata tafiti nyingi zilizofanywa kuhusu changamoto za kilimo Africa zipo consistent na ushauri wako. Nashukuru kupata hii taarifa moja kwa moja kutoka kwa mkulima.
Unashukuru kupata taarifa kutoka kwa mkulima alieshindwa ? huyo hakuwa mkulima, alijaribu kilimo kwamaana alisikia kuwa kilimo kina lipa akaona tofauti akapanic. hakufanya research kabla ya kilimo, aliingia kichwa kichwa kwa kutumia kilimo kwanza ( kilimo cha kizamani). Alafu unadai kakupa ushauri mzuri.
 
aliyeandika huu uzi si mjasiriamali. Alikurupuka tu kwa kuiga akaangukia pua. Sasa anawashauri wenziwe ambao si wajasiriamlai wasikurupuke kama yeye. Ila wajasiriamli msisikilize ushauri wake. Nu ushauri kautoa kwa losers wenziwe wenye mitizamo hasi kama yeye. Hiyo ndo observation yangu
hapo umenena kiukweli. YATOSHA
 
Unashukuru kupata taarifa kutoka kwa mkulima alieshindwa ? huyo hakuwa mkulima, alijaribu kilimo kwamaana alisikia kuwa kilimo kina lipa akaona tofauti akapanic. hakufanya research kabla ya kilimo, aliingia kichwa kichwa kwa kutumia kilimo kwanza ( kilimo cha kizamani). Alafu unadai kakupa ushauri mzuri.

Mtu mwenye akili utoa ushauri, unapoteza muda kuponda lakini utoi ushauri. Mimi ni kweli nilikurupuka ndio maana nikaandika kuwa watu wawe na taadhari, maana kuna vijana wengi wanaingia kwenye kilimo kwa kukurupuka. Nashindwa kuelewa point zako ni zipi?, au unaamini watu wote wako aware kama ulivyo wewe?.
 
Nilichokwambia, umetumia kushindwa kwako kutisha watu kuwa haiwezekani, swali ni je kweli haiwezekani au wewe ndo umeshindwa? Je walio weza wameweza vipi?, kwanini tutumie reference yako amabo ni dhaifu sana kuonyesha kuwa haiwezekani?

Ungeandika kuhusu kushindwa kwako kisha ukaomba ushauri, ukaonyeshwa ni wapi ulipokosea na nini ungefanya.
Biashara ya kilimo si ya kuingia kichwa kichwa, ni biashara inayotaka research, unalima nini ( Ubora wa mbegu, soko, unalima wapi (hali ya hewa), aina ya udogo, upatikanaji wa maji ya uhakika kwa ajili ya umwagiliaji na pia ubora wa maji. pia kuna uhifadhi wa mazao wakati unasubiri soko zuri ( high demand).

Mwisho, Kilimo ni Sayansi.

Haya maelezo ndio ulitakiwa uyatoe mwanzoni mkuu, hapakua na haja ya kutumia lugha kali kiasi kile, hata hivyo nafikiri Nkobe ametolea mfano huo kuonyesha kwamba watu wengi wanafanya hivyo na ni kweli wengi wanaofanya kilimo hawafanyi kilimokama biashara kama ambavyo umeelezea vizuri suala la umuhimu wa utafiti.

Unaona sasa mtu akisoma bandiko la mwanzo akichanganya na nyongeza yako anapata kitu kamili? Ni kujifunza kuvumiliana tu mkuu. Ahsante kwa mchango wako!
 
Last edited by a moderator:
Hata hivyo kuna kujifunza kwa njia mbili, ya kwanza ni kuangalia wengine wamekosea wapi kisha wewe ukafanya tofauti na kujihadhari usikosee. Njia ya pili ni wewe mwenyewe kukosea na kujifunza kutokana na makosa yako! Cha msingi kama maelezo yatasaidia wengi sioni kama kuna tatizo!
 
Unashukuru kupata taarifa kutoka kwa mkulima alieshindwa ? huyo hakuwa mkulima, alijaribu kilimo kwamaana alisikia kuwa kilimo kina lipa akaona tofauti akapanic. hakufanya research kabla ya kilimo, aliingia kichwa kichwa kwa kutumia kilimo kwanza ( kilimo cha kizamani). Alafu unadai kakupa ushauri mzuri.

We jamaa unaonekana ama hujawahi kulima ama huna uzoefu wa kutosha wa kilimo...ama unalima kama hobi tu.

Sioni sehemu uliyotoa maboresho.Unakazana mtoa mada kashindwa sasa wewe uliyefanikiwa boresha uzi watu wajifunze..Unaweka neno Research kujifanya unajua sana...Hata ufanye research ya aina gani bado kilimo cha bongo kina changamoto nyingi mpya zinazoibuka kila siku.Mfano mimi nililima sehemu mwaka huo wadudu wakaingia sikuvuna kitu.

Umejaa majivuno kujifanya unalima kisasa huku huweki chochote cha kujifunza kwa wengine.Eti research si tungekusikia Unamuuzia Mahindi Bakhressa..
 
Mtu mwenye akili utoa ushauri, unapoteza muda kuponda lakini utoi ushauri. Mimi ni kweli nilikurupuka ndio maana nikaandika kuwa watu wawe na taadhari, maana kuna vijana wengi wanaingia kwenye kilimo kwa kukurupuka. Nashindwa kuelewa point zako ni zipi?, au unaamini watu wote wako aware kama ulivyo wewe?.

Mkuu umetimiza Wajibu wako wa kushauri..wenye kusoma wamekuelewa..Kilimo kina changamoto mpya zinaibuka kila siku ni jukumu kuyasema ili wanaoingia wajue...
 
Haya maelezo ndio ulitakiwa uyatoe mwanzoni mkuu, hapakua na haja ya kutumia lugha kali kiasi kile, hata hivyo nafikiri Nkobe ametolea mfano huo kuonyesha kwamba watu wengi wanafanya hivyo na ni kweli wengi wanaofanya kilimo hawafanyi kilimokama biashara kama ambavyo umeelezea vizuri suala la umuhimu wa utafiti.

Unaona sasa mtu akisoma bandiko la mwanzo akichanganya na nyongeza yako anapata kitu kamili? Ni kujifunza kuvumiliana tu mkuu. Ahsante kwa mchango wako!
Thanks Samaritan
 
Last edited by a moderator:
We jamaa unaonekana ama hujawahi kulima ama huna uzoefu wa kutosha wa kilimo...ama unalima kama hobi tu.

Sioni sehemu uliyotoa maboresho.Unakazana mtoa mada kashindwa sasa wewe uliyefanikiwa boresha uzi watu wajifunze..Unaweka neno Research kujifanya unajua sana...Hata ufanye research ya aina gani bado kilimo cha bongo kina changamoto nyingi mpya zinazoibuka kila siku.Mfano mimi nililima sehemu mwaka huo wadudu wakaingia sikuvuna kitu.

Umejaa majivuno kujifanya unalima kisasa huku huweki chochote cha kujifunza kwa wengine.Eti research si tungekusikia Unamuuzia Mahindi Bakhressa..
Nchi hii hakuna mkulima au wakulima watakaoweza kujaza vihenge vyake.
OOOhh kilimo chanza ,sijui nini nini
Mahindi,ngano akiacha ku import.
Taznania tutakufa njaa,bei vitu vitaenda juu.
 
Tatizo lako kubwa ni hukufanya utafiti, changamoto ulizotaja ni za kawaida sana ambazo kama ungefanya critical analyzation usinge fail
 
Gunia la mahindi mikoa ya kusini halijawah kushuka chini ya elfu tisini
Ukitaka kikulipe fanya tofauti na wenzio, hasa ni lazima umwagilie. Mikoa ya kusini ina mvua ya kutosha, uwezekano wa kuvuna ni mkubwa, tatizo la kule gunia la Mahindi linaweza kushuka hadi elfu 15 maana kila anaelima anapata. Ukiweza kuleta Dar sawa
 
Hebu ondoka huko, unatuonyesha kushindwa kwako na jinsi gani ulivyo mpumbavu. Kwa maelezo yako ulifanya kilimo cha kizamani sana( Kilimo kwanza) alafu kwenye N.B unajifanya wewe unauzoefu unataka kuwasaidia wasio na uzoefu.

Kama hujui afadhali ungeuliza kwa kuomba ushauri, kwenye pont yako namba mbili inatosha kuonyesha ulivyo .........
Mtu ambae hajawahi kulima na anahamasisha kulima kupitia mtandao utamjua tu, Tusi ulilomtukana mwenzio likurudie. Mimi nimelima zaidi ya miaka 30 na nimelima kilimo cha kila namna cha kutumia mvua cha kumwagilia kwa matone na kawaida.
Biashara ya kilimo ina changamoto lukuki. Unaweza kuwa na maji ukachambuliwa na magonjwa ambayo si rahisi kuyatibu. Unawaeza ukavuna kwa wingi ukapambana na changamoto ya soko ambayo ni kubwa kuliko changamoto zote kwenye nchi kama yetu hii ambayo Serikali ndiyo ina kauli wapi uuze mazao yako na si mkulima mwenyewe. Pia unazungumzia kumwagilia mazao je unajua kweli gharama za kukuwezesha kumwagilia mazao kweli?! unahitaji water source ambayo ni ya kuaminika, mashine za kusukuma maji na mafuta ya kupamp kila siku kwa siku si chini ya 100 na kuendelea kutokana na aina ya zao na hali ya hewa, matanki ya kutunza maji na pia infrastructure ya umwagiliaji matone ndo ghali sana, kwa uchache hapo mtu anahitaji si chini ya milion thelethini kwa miundo mbinu tu ya umwagiliaji. Ndugu yangu ngoja niachie hapo na kama una busara umwombe radhi mwenzio, Mara nyingi sisi wakulima halisi huwa tunapenda kuwahamasisha wengine waingie kwenye kilimo ili waonje joto ya jiwe. Nampongeza sana mleta mada aliyoandika ndo halisi kabisa, ukiingia kwenye kilimo usiende kichwa kichwa utakufa siku si zako.
 
Hebu ondoka huko, unatuonyesha kushindwa kwako na jinsi gani ulivyo mpumbavu. Kwa maelezo yako ulifanya kilimo cha kizamani sana( Kilimo kwanza) alafu kwenye N.B unajifanya wewe unauzoefu unataka kuwasaidia wasio na uzoefu.

Kama hujui afadhali ungeuliza kwa kuomba ushauri, kwenye pont yako namba mbili inatosha kuonyesha ulivyo .........
kwel kabisa, yaani jamaa ni mpumbavu plus
 
Hebu ondoka huko, unatuonyesha kushindwa kwako na jinsi gani ulivyo mpumbavu. Kwa maelezo yako ulifanya kilimo cha kizamani sana( Kilimo kwanza) alafu kwenye N.B unajifanya wewe unauzoefu unataka kuwasaidia wasio na uzoefu.

Kama hujui afadhali ungeuliza kwa kuomba ushauri, kwenye pont yako namba mbili inatosha kuonyesha ulivyo .........
Huyu jamaa amekula maharage ya wapi aisee!!
Hasira zako unakuja kumalizia huku .Hii mada ni nzuri tu inaonyesha changamoto katika sekta ya kilimo na jinsi ya kukabiliana nazo sasa wewe unakuja kutukana huku na kumlaumu mleta mada kama wewe ni mjuzi zaidi si ungefungua UZI wako uelimishe watu kuhusu kilimo unasubir watu wafungue uzi uje uwatukane na kuwaponda sii vizuri kabisa alafu pili pili usio ila inakuwashia nini.
 
Gunia la mahindi mikoa ya kusini halijawah kushuka chini ya elfu tisini
Acha matani mkuu , mimi ninavyoandika niko Sumbawanga na mwaka huu tumeuza gunia sh 12, 000 mpaka elfu 9,000 kwa sasa ndo bei imepanda na haijazidi 45,000 kwa bei ya reja reja, Ninalima pia mikoa ya Dodoma kanda ya ziwa na Morogoro. Kwa taarifa yako ni kanda ya ziwa pekee ambapo bei ya mahindi imefika 75,000 na hiyo ni bei ya rejareja
 
Back
Top Bottom