TAHADHARI: Wahafidhina wapo toka zamani, Kisa cha Abneli mwana wa Neri na Generali Yoabu

TAHADHARI: Wahafidhina wapo toka zamani, Kisa cha Abneli mwana wa Neri na Generali Yoabu

Kuna kosa la kiuongozi Daudi alifanya.
Hakuwahusisha watu muhimu kama Yoabu.
Yoabu alihatarisha sana uhai wake kwa ajili ya Daudi lakini Daudi hukukumbuka hayo.

Ni Yoabu ndiye aliyemuindolea Daudi aibu ya kumjaza mimba mke wa Uria ambaye Daudi aliagiza awekwe mstari wa mbele ili auawe na adui kupoteza ushahidi.

KUna funzo kubwa sana...kiongozi wa juu anapofanya mapatano au maridhiano ahakikishe ushiriki wa wasaidizi wake vinginevyo atasababisha migogoro kwenye uongozi wake.

Nina wasiwasi kama wana ccm muhimu wamehusishwa na kuridhia yanayoendelea ...muda utaongea
Nadhani sasa unaweza kuona link iliyopo kati ya Uzi huu na Kisa hiki😅😅

Mfalme Daudi alikuwa na mapungufu mengi na ndio maana alikuwa ana hestate kumuonya hata kumwadhibu Yoabu.

Yoabu alijua siri nyingi za maovu ya daudi kwa kupitia hilo Daudi alikuwa dhaifu sana kwa Yoabu.

Yoabu alikuwa hasikilizi mtu yeyote ispokuwa Daudi tu na pengine anakengeuka.

Rais( Mfalme) kwa kawaida hawezi kuanzisha movement ya maridhiano then akatokea mtu mmoja kuyaharibu. Huo ndio Uhafidhina.

Maelewano ya Abneri na Daudi yalikuwa kitisho kwa Yoabu ndio maana alijihami.

Hii ndio maana ya "Tahadhari"
 
Nadhani sasa unaweza kuona link iliyopo kati ya Uzi huu na Kisa hiki😅😅

Mfalme Daudi alikuwa na mapungufu mengi na ndio maana alikuwa ana hestate kumuonya hata kumwadhibu Yoabu.

Yoabu alijua siri nyingi za maovu ya daudi kwa kupitia hilo Daudi alikuwa dhaifu sana kwa Yoabu.

Yoabu alikuwa hasikilizi mtu yeyote ispokuwa Daudi tu na pengine anakengeuka.

Rais( Mfalme) kwa kawaida hawezi kuanzisha movement ya maridhiano then akatokea mtu mmoja kuyaharibu. Huo ndio Uhafidhina.

Maelewano ya Abneri na Daudi yalikuwa kitisho kwa Yoabu ndio maana alijihami.

Hii ndio maana ya "Tahadhari"
Kuna haja kuanzisha uzi kuhusu Daudi.

Huyu ana funzo kubwa sana kwetu;
1. Alikuwa mpiganaji hodari
2. Alikuwa msikivu...rejea kisa cha mke wa Nabali

3. Alikuwa na hofu ya Mungu..rejea alipopinduliwa na mwanae...kuna mtu alimzomea ...wasaidizi waliomba ruhusa ya Daudi wammalize yeye alisema...mwacheni huenda Mungu aliruhusu amzomee.

4. Kosa...kutamani mke wa mtu akioga

5. Kiburi...kuwahesabu Israel kwa kiburi akijua ni kosa.

6. Kisasi...alimkabidhi Sulemani watu kadhaa ahakikishe hawafi kwa amani isipokuwa anawamaliza.

.......DAUDI ANA MAMBO MENGI KUJIFUNZA...
 
Kwanza nitoe Pongezi zangu Nyingi kwa Viongozi wa Kitaifa akiwemo Mh Rais Samia Suluhu Hassan, rais wa Jamuhuri ya Muungano Tanzania.

Pongezi zingine ziwaendee viongozi wakuu wa vyama vya siasa Mh Freeman Mbowe na Mh Zitto Zuberi Kabwe. Bila kuwasahau na wananchi wote wenye Mapenzi Mema.

Tatu sitaweza kuwasahau pia viongozi hawa kwa upekee kabisa Askofu Emaus Mwamakula na Lecturer Dr Lwaitama kwa Nasaha zao za kila siku kuhusu Amani, umoja na haki ktk Taifa letu la Tanzania.

Hivi Karibuni niliandika kuhusu Generali mmoja wa Jeshi la Israeli anaitwa Yoabu. Huyu alikuwa kiongozi wa juu majeshi yote ya falme hiyo wakati wa Utawala wa Mfalme Daudi Kusini mwa Israeli yaani Hebroni.

Ktk makala ile ilikuwa kwa mfumo wa Swali, Je Tanzania kuna Yoabu? Pengine kutokana na uwasilishaji wangu( mimi sio mwandishi) kuna baadhi ya wasomaji hatukuelewana. Sio kosa!

Sisi wengine wenye imani nyingi za hapa na pale kila jambo huwa tunalipima na kulitazama kwa mujibu wa imani zetu. Elimu ya dini tunaitumia kama reference kwenye mazingira yetu ya sasa.

Juzi Tarehe 8 Machi Mh Rais Suluhu alihutubia Taifa akiwa kwenye Jukwaa la wanachama wa Chadema, baraza kuu la wanawake lenye heshima afrika mashariki na kati.

Ktk hotuba yake aligusia uwepo w watu conservatives yaani wenye misimamo isiyobadilika hata kwenye jambo lenye Maslahi ya Kitaifa. Hawa watu sometimes ni watu hatari. Alisema wapo CCM na Wapo Chadema.

Abneli Mwana wa Neli alikuwa ni Mkuu w Jeshi la Mfalme Sauli Yerusalem. Yeye alikuwa coordinator wa shughuli zote za ulinzi na maslahi ya ufalme wa Saul kipindi ambacho Mfalme Sauli alikuwa na migogoro ya kiutawala dhidi ya Mfalme Daudi.

Hofu ya Sauli ni kuhusu Daudi anayetaka kuchukua ufalme wa Israel yote yaani Hebroni na Yudea( Yerusalem).
Kulipiganwa vita mbali mbali kati ya Daudi na Sauli na kati ya Daudi na Wafilisti( waparestina).

Kutokana na uhasama kuwa mkubwa upande wa Sauli ulianza kushindwa kuhimili mapambano. Watu wa Sauli walikufa wengi, na wengine kubaki walemavu.

Jemedali Abneli mwana wa Neli akatumwa Mission kwenda kwa Mfalme Daudi kukaa kwa amani na kuridhiana ili suluhu ipatikane bila kuumiza wananchi wao.

Ugeni kwa upande mmoja ukiongozwa na Abneli na upande wa pili akiongozwa Mfalme Daudi Mwenyewe katika Ikulu yake.

Kitendo kile cha kufanya mazungumzo ya amani hakikumfurahisha General Yoabu. Alianza kuona Abneli anaweza kuwa Royal kwa Daudi na hivyo kuna uwezekano Abneli anaweza kuchukua nafasi ya Yoabu.

Ikawa walipomaliza maridhiano Daudi alisindikia msafara wa Abneli baadae akarudi Ikulu.

Wakati huo huo Mwanajeshi Katiri aoiyekuwa na roho mbaya kuwahi kutajwa katk Biblia Yoabu alikuwa ametoka kuongoza Vita huko Gathi kwa wafilisti na wa Amaleki.

Alipofika Ikulu akadokezwa kuwa muda mfupi uliopita Abneli alikiwa Ikulu akifanya mazungumzo na Mfalme.

Basi akapiga mbio kuwafata akina Abneli.

Kwa kuwa Abneli aliamini ni wakati wa amani na yakale yamekwisha si ndweli alisimamishwa na Yoabu akimwambia anataka wasalimiane na kukumbatiana.

2samweli 3: 24-25

Raraabii!! Abneli akaamini akamkumbatia Yoabu. Kumbe Yoabu alikuwa anaongozwa na Hila. Alikuwa ameficha kisu Mfukoni kwa nyuma. Wakati wakisalimia kwa amani Yoabu akamchoma Kisu tumboni. Abneli mwana wa Neli akafariki palepale.

Taarifa za Kifo cha Abneli zilisambaa kwa kasi sana. Nchi nzima ya Israel ikaingia kwenye majonzi makubwa. Hofu na vilio vikatawala. Nchi nzima wakafunga na kusali kwa siku Tatu wakiomboleza.

Mfalme Daudi alisikia habari zile zikamsikitisha sana. Akalia na kuomboleza mbele ya Raia wake. Hata ushindi waliopata kule Amaleki ukaingia doa.

Daudi analia mbele ya Kaburi la Abneli akisema imekuwaja Abneli umekufa kizembe hivyo? Kwani ulifungwa miguu na mikono?

Kosa la Daudi ni kusahau kukumbuka kuwa ndani ya Utawala wale kuna Wahafidhina wasiopenda utengamano. Wasiopenda amani kwa wengine. Yaani kwao bora vita na mateso kuliko umoja na mshikamano.

Yoabu alitumia vita na vurugu kujinufaisha na kupata umaarufu kwa kuwa alijua kupigana na siraha za kutosha aliweza kuzitumia vyema. Hivyo alibaki kuwa ni kipenzi cha Mfalme.

Kwa lugha nyingine nje ya vita na uhasama Yoabu alikuwa hana sifa nyingine. Hana cha kumuonesha Mfalme. Hana maana na hana kazi. Hivyo migogoro kwake ilikuwa na Advantage kubwa bila kujali Mfalme alikuwa akichukizwa na hali ile. Ilifikia hatua Yoabu akamuua Mtoto wa Daudi kwa kumchoma Mkuki moyoni na mfalme akabaki analia tu asimfanye kitu Yoabu kwa kuwa alijua bila Yoabu vita nyingi vya maaduni asingetoboa. Hivyo mfalme alibaki kufadhaika moyoni tu.

Kwa Upande wa Viongozi wetu wa Kitaifa wameligundua hilo. Ni muhimu sana kuongeza umakini dhidi ya wahafidhina wasije wakavuruga hii mipango mizuri.

Na Mwenyezi Mungu awasimamie na kuwabariki sana.

Nimesikia kuna vikao vinaendelea kwa maslahi ya Taifa. Mungu awajali mkafanikishe jambo hili mweze kuwatumikia Wana wa Mungu wa Tanzania kwa mafanikio makubwa.

Asalam Aleykum.

2Samwel3: 20-39.


Si "waparestina" ni "wa palestina" muandishi utakuwa wa kwetu kanda ya Ziwa si Bure,

Hongera kwa Makala yako
 
Mkuu umetoa mfano bora kabisa na ubarikiwe, ni kweli wako watu wasiotaka amani wala utangamano wala upendo na hao ndo wanamvuruga sana mama lakini Samia na Mbowe walianza na "MUNGU" watamaliza na "MUNGU".
CUF na NCCR walipoamua kufanya hayo mliwatukana sana. Ndio maana nasema chadema wengi akili hamna
 
Ndicho alichosema Mh Rais Samia.
Hao watu ndio husababisha hata mambo mabaya kutokea katika Nchi ! Wanaoitwa wahafidhina katika Nchi zilizoendelea hawako kama hawa wenzetu ambao wapo tayari kumterrorise either psychological au physically yeyote ambae watamuona haendani na fikra zao !!
 
Kuna haja kuanzisha uzi kuhusu Daudi.

Huyu ana funzo kubwa sana kwetu;
1. Alikuwa mpiganaji hodari
2. Alikuwa msikivu...rejea kisa cha mke wa Nabali

3. Alikuwa na hofu ya Mungu..rejea alipopinduliwa na mwanae...kuna mtu alimzomea ...wasaidizi waliomba ruhusa ya Daudi wammalize yeye alisema...mwacheni huenda Mungu aliruhusu amzomee.

4. Kosa...kutamani mke wa mtu akioga

5. Kiburi...kuwahesabu Israel kwa kiburi akijua ni kosa.

6. Kisasi...alimkabidhi Sulemani watu kadhaa ahakikishe hawafi kwa amani isipokuwa anawamaliza.

.......DAUDI ANA MAMBO MENGI KUJIFUNZA...
Hoja namba
1. Alikuwa na nguvu za ajabu( alipewa na Mungu) alikuwa anaweza kuua wafilisti kwa mikono yake. Wakati anamuoa Mikali alipewa sharti la kuleta govi 100. Huu ulikuwa mtego wa Sauli ili akafie vitani.
2. Daudi alikuwa na ubabe fulani. Kisa cha kutaka kumuua Nabali ni kwa sababu Nabali alikataa kuporwa mali zake na wanajeshi wa Daudi. Ndipo mke wake Abigaili akamuomba msamaha. Baadae Nabali alifariki Daudi akamuoa mjane.

3. Alimkata Ayoub asimwue mwanaye Absalomu hata kama absalom alitaka kumpindua. Hii ni huruma ya kiwango kikubwa. Lakini mwanaye angemfanya nini?

Uhafidhina wa Yoabu ulianza zamani.

Yoabu anajifanya ana huruma kwenda kumchukua Absalome mafichoni na kutumia njama za mwanamke mmoja kumpa methali Daudi kana kwamba Yoabu anamuombea msamaha Absalom lakini njama za Yoabu ilikuwa kumsogeza karibu aweze kumdhuru.

Daudi alilia sana kifo cha mateso cha mwanaye Yoabu
 
Nadhani sasa unaweza kuona link iliyopo kati ya Uzi huu na Kisa hiki😅😅

Mfalme Daudi alikuwa na mapungufu mengi na ndio maana alikuwa ana hestate kumuonya hata kumwadhibu Yoabu.

Yoabu alijua siri nyingi za maovu ya daudi kwa kupitia hilo Daudi alikuwa dhaifu sana kwa Yoabu.

Yoabu alikuwa hasikilizi mtu yeyote ispokuwa Daudi tu na pengine anakengeuka.

Rais( Mfalme) kwa kawaida hawezi kuanzisha movement ya maridhiano then akatokea mtu mmoja kuyaharibu. Huo ndio Uhafidhina.

Maelewano ya Abneri na Daudi yalikuwa kitisho kwa Yoabu ndio maana alijihami.

Hii ndio maana ya "Tahadhari"
FB_IMG_1678449428565.jpg
FB_IMG_1678449437294.jpg
FB_IMG_1678449442167.jpg
 
Mkuu ujumbe wako ni mzuri Ila Kwa kuongezea tu hapo kwenye nukuu ya biblia kama ilivyoandikwa. Imeandikwa kwamba Yoabu alimwua Abneli Kwa akili ya damu ya Asaheli ndugu yake, ambaye aliuwawa na Abneli.
2 Sam 3;27
Ndio ujue kwamba mleta mada haelewi hata anachojaribu kutuelezea.

Hakuna relevance yeyote ile ya andiko na uhafidhina.
 
Hao watu ndio husababisha hata mambo mabaya kutokea katika Nchi ! Wanaoitwa wahafidhina katika Nchi zilizoendelea hawako kama hawa wenzetu ambao wapo tayari kumterrorise either psychological au physically yeyote ambae watamuona haendani na fikra zao !!
😅😅😅
 
Hiyo story ya bible umeichanganya changanya sana hadi imekosa ladha
 
Unaongelea huyu anayeimba?

Kama ndivyo, huyo ni Mwimbaji wa Injili Bahati Bukuku.
Anaelezea namna ya kupambana na matatizo ya kijamii kwa kutumia busara badala ya nguvu nyingi.

Anasema usitumie nyundo kumuua Nzi aliyetua kichwani mwa mtu maana utaacha jeraha kubwa kwa mtu huyo.
Kumbe ndio bahati bukuku huyo? Maana zaman hakua mwarabu ivo mpaka nimemsahau asee!!
 
Back
Top Bottom