Fred Mwakitundu
JF-Expert Member
- Dec 31, 2018
- 227
- 382
Ni tahadhari tu kwa wale mnaotumia magari binafsi kwenda kuwaona wagonjwa ama kwa shughuli nyingine katika Hospital ya Rufaa ya Kanda ya KCMC mjini Moshi kwamba muwe makini sana kuna mtandao mkubwa wa vijana wanaotumia funguo bandia kufungua milango ya magari na kuiba vitu vilivyomo ndani ya gari na kufunga vizuri na kisha kuondoka pasipo kutiwa nguvuni.
Hiki kimekuwa kilio cha siku nyingi kwa watu wenye magari kiasi cha kupaona KCMC kama si mahala salama kwa usalama wa mali zao na kinachoshangaza zaidi eneo lote la maegesho wanapoegesha watu kunamulikwa na camera za usalama lakini wizi ndo kwanza unashika kasi
Hivi karibuni kinara wa mtandao huo alitiwa nguvuni tena kwa juhudi binafsi ya mtu aliyeibiwa vitu vyake ndani ya gari baada ya kuanzisha uchunguzi usio rasmi kwa kufuatilia nyendo za kijana huyo mdogomdogo na siku ya siku akambamba akiiba vitu ndani ya gari ya mtu mwingine na kuziarifu mamlaka za KCMC na hatimaye kumtia nguvuni
Kijana huyo alishitakiwa mahakamani na kutiwa hatiani na hadi sasa bado anatumikia kifungo chake lakini huku nyuma ameacha mizizi inayoendelea kutambaa bila kukatwa
Hii ni taarifa ya awali taarifa kamili ni hapo baadae
Wenye magari mkae chonjo, kama una kitu cha thamani ndani ya gari usikiache unaweza ukalia pasipo kuchapwa makola
Hiki kimekuwa kilio cha siku nyingi kwa watu wenye magari kiasi cha kupaona KCMC kama si mahala salama kwa usalama wa mali zao na kinachoshangaza zaidi eneo lote la maegesho wanapoegesha watu kunamulikwa na camera za usalama lakini wizi ndo kwanza unashika kasi
Hivi karibuni kinara wa mtandao huo alitiwa nguvuni tena kwa juhudi binafsi ya mtu aliyeibiwa vitu vyake ndani ya gari baada ya kuanzisha uchunguzi usio rasmi kwa kufuatilia nyendo za kijana huyo mdogomdogo na siku ya siku akambamba akiiba vitu ndani ya gari ya mtu mwingine na kuziarifu mamlaka za KCMC na hatimaye kumtia nguvuni
Kijana huyo alishitakiwa mahakamani na kutiwa hatiani na hadi sasa bado anatumikia kifungo chake lakini huku nyuma ameacha mizizi inayoendelea kutambaa bila kukatwa
Hii ni taarifa ya awali taarifa kamili ni hapo baadae
Wenye magari mkae chonjo, kama una kitu cha thamani ndani ya gari usikiache unaweza ukalia pasipo kuchapwa makola