Selous
JF-Expert Member
- Jan 13, 2008
- 1,325
- 145
Tatizo watanzania wengi tunaanza kulizoea hili bonde na kuliona kama makao yetu ya kudumu. Ndiyo, na aliyetupeleka bondeni anajua fika kuwa nje ya bonde atapoteza nguvu kwa kuwa huko kuna hewa safi isiyoruhusu ustawi wa uvundo. Bunge limegeuzwa kuwa baraza la kutunga sheria kudhibiti na kuzima mawazo yoyote ya kuhama bondeni. Serikali inalinda huu uvundo kwa nguvu zake zote kwa kisingizio cha amani na utulivu bila kujua inatafuna watu wake pole pole kama kansa. Wengi baada ya kuathirika na uvundo wamepoteza kabisa uwezo wa kunusa, kusikia wala kuona na wanachapa usingizi bila wasiwasi. Wachache ambao hawajaathirika sana wamefungwa kamba miguuni na kuzibwa midomo wasije wakawakosesha wenzao usingizi.
Pamoja na Utawala bora umesahau mkuu.