Taifa linahangaika na wasiojulikana waliomshambulia Tundu Lissu! Je, ni hawa?! Mhe. Mwigulu, IGP, anzieni hapa!

Huyu jamaa kwa kutamka hivyo tu alipaswa atuachie ofisi yetu ya Magogoni, kwa kuwa tayari ameabuse power tuliyompa ya kutuongiza bila kujali tofauti zetu itikadi za kisiasa.....

Na kama kweli Bunge letu lingekuwa STRONG kama la South Africa, siku nyingi tu huyu jamaa angekuwa tayari keshakuwa impeached!
 
Naomba kujuzwa zaidi, ina maana mtu akiiba kamera ndo ameiba clips ambazo zimerekodiwa? savers zinakaa katika CCTV cameras?
 

Kukiwa na Mlinzi basi ndiye suspect wa kwanza
 
Kama unajua hawapo sasa unataka wakina nani wafanye uchunguzi na upelelezi? Jua tu hawapo basi hawapo halafu fikiria namna ya kujisaidia mwenyewe!

Dah!Hata kama ni kada wewe mwisho.Pole.Nimekusikia kwa maana ukiwa Mpinzani automatically unapoteza haki zako zote za msingi ikiwemo na URAIA.Hongereni CCM
 
Dah!Hata kama ni kada wewe mwisho.Pole.Nimekusikia kwa maana ukiwa Mpinzani automatically unapoteza haki zako zote za msingi ikiwemo na URAIA.Hongereni CCM

Tatizo lako una imani badala ya maarifa. Ukiamini katika kitu huwezi kuona upungufu wake. Unajua impact ya kusema nchi haina IGP wala Waziri was Mambo ya Ndani?

Ungejua una haki ya uraia ungetimiza wajibu wako was kuheshimu mamlaka.

Huwezi kudai haki pasipo wajibu, unapata wapi uhalali wa kuiai huduma taasisi ambayo una amini haipo?

Tatizo la kuvamia vitu pasipo maarifa ndio hili. Viongozi wa juu kabisa wanaoheshimika wa upinzani wanaheshimu na kuzitambua mamlaka vilivyo Leo kajitu tu ambacho hata hakafahamu chochote kanajitokeza kusema IGP hayupo.!!!!!!

Jamani jamani siasa inahitaji ufahamu kwanza, hata kama una manoeuvre, you manoeuvre within the lines and NOT out of blue.
 
Polisi wanafanya kazi gani wasiwabaini? Ni ukweli wanashirikiana nao kwa karibu. Hili jitu letu la magogoni limejifunza kwa Kagame na M&
 
Walevi wa Madaraka huwa hawajui hayo!!
 
Mbona ufahamu unatia shaka ? Ebu soma ulichoandika, Watu wanatekwa, wanauawa, wao wanafanya uchunguzi usiokuwepo. Asiye na maarifa ni wewe
 

Kabla sijaiheshimu MAMLAKA,hiyo MAMLAKA inayotaka kuheshimiwa inatakiwa iheshimu si RAIA tu bali uhai wa kila RAIA.Baba anapobehave nyumbani usimlaumu mtoto kwa kumdharau.

Unayatetea sababu unafadhila unazipata toka huko na wanaouawa bila hatia hawakuhusu sababu ni wapinzani na specifically mnakaa chini nakusema ah liache lipinzani lile na life tu,huku mkidhani kwa vile nyie ni wanachama wa Chama tawala basi mnahaki.

Utamuona IGP au Waziri wa Mambo ya Ndani au Rais kwa matendo yake.Yanapotokea mauji ya kila mara na ya upande mmoja mwenye dhaman lazima ashtuke kama hashtuki maana yake hao watu hawapo.

Haingii akilini Waziri wa Mambo ya ndani yupo busy kwenye kampeni za Ubunge na udiwani anaifanya kazi yake muda gani?Mauaji yanatokea yuko busy anatweet yuko kwenye kampeni,hivi mpaka uovu gani au nani auawe ndiyo muone kuna shida?

Sipendi mauaji ya raia yoyote,na for your information HESHIMA ni kama msumeno unakata kotekote.Pole sana.Siku yatakapokukuta sidhani kama kuna mtu atakusikiliza sababu hupata hata nafasi ya kuwatetea walioumizwa.Kuna mayatima wangapi tunawatengeneza kwa mikono yetu?

Hakuna SIASA kwenye maisha ya bindamu yeyote.Hata awe jambazi kama itawezekana kumkamata bila kumua ni bora zaidi kuliko kumuua kuna sababu nyingi kwanini asiuawe kama uwezekano wa kumpata akiwa hai upo.

Kama Serikali ya JPM inaona kuua wapinzani ndiyo kuijenga CCM basi ajue anaimaliza na si kuijenga.Chaguo ni lenu wanachama wa CCM,ANC iliamua Taifa lao kwanza Jacob Zuma baadaye (Chama) baadaye.

Na Zuma amesema asingependa hata RAIA wake mmoja aumizwe au kupotea kwa sababu yake au Chama chake kuvurugika,huyu naye aliliona la Taifa kwanza na Chama chake baadaye.

Nyie wanywa Maji ya bendera endeleeni Chama kwanza Taifa Baadaye yatakapokuja kuwasibu mtatupa taarifa.

Lakini hakuna Heshima bila kuheshimu
 
Hujui majukumu ya FBI
nayajua majukumu ya green guards na zanzibar tu, ubalozi wa marekani ulisema upo tayari kusaidia issue ya upelelezi wa lissu,ccm wakakataa kwa madai kwamba polisi itaweza hiyo kazi?
sasa ulidhani wangeletwa CIA,au NSA?
 
Mbona ufahamu unatia shaka ? Ebu soma ulichoandika, Watu wanatekwa, wanauawa majinga yako yanafanya uchunguzi usiokuwepo. Asiye na maarifa ni wewe unatii mamlaka ya mapepo.

Kutii mamlaka ya mapepo kunakupa maarifa ambayo wengine hawana. Unafahamu kazi ya kila pepo na hivyo kufahamu pepo linalowahadaa binadamu huku wanaliamini wakidhani ni mjumbe wa Mungu kumbe ni malaika wa shetani. Kinachopasa kuwajulisha mnakosa maarifa na ndio maana mnaangamia in kutokubadilika kwa hali ya mateso yenu wakati malaika wa shetani wao wakiishi tofauti na ninyi, wakiyafurahia maisha wala hawahangaiki tena na wafu na waliopoteza viungo na kuwa walemavu.

Ukikosa maarifa lazima utaangamia. Imeandikwa.
 
Watanzania tatizo wengi hatujui kuwa tunataka nini?

CCM wao wanachotaka ni Madaraka basi.
CCM wakiona kuwa ufisadi unawasaidia kushinda wanaufanya.
Wakiona kuwa kuficha ufisadi usijulikane ili washinde basi watafanya hivyo.
Wakiona kuwa kuvunja haki za binadamu kutawasaidia kushinda basi watafanya hivyo.
CCM hawajali chochote iwe ni sheria za nchi, amri za Mungu, sharia za dini, mila za kitanzania , uhai wa mtu ; kamwe hawatajali alimradi watakachokifanya kitawapa ushindi tu kwenye uchaguzi.

Sasa kwa wananchi wengi na wapinzani hawajui wanachotaka ,wao wanaenda tu kama mazuzu.
Ndio maana unakuta leo wanakuambia tunataariifa za kupigwa ,kitekwa na kukatwa mapanga kwa viongozi wetu ,na wanatoa mpaka ushahidi na walipo watesi wao lakini cha ajabu hawatoi taarifa kituo cha polisi wala hawajilindi matokeo yake wanauawa kama kuku na watu wasiojulikana.

Chadema weshaona kuwa watu wao kuuawa au kupigwa ni sehemu ya kupata umaarufu na kunadi chama kwa huruma za wananchi. Ndio maana wanapata taarifa kabla halafu wanakimbilia online Tv kushitaki badala ya kwenda polisi au kuchukua maamuzi magumu ya kujilinda au kuweka mitego ya kuwakamata watesaji na wauaji.
Chama chenye wanachama wengi vijana kwenye miji yote haiwezekani kishindwe kuwanasa watekaji. Vinginevyo wanajiteka wenyewe kwa sababu wameshaona kuwa ni mbinu ya kupata umaarufu.
Wajifunze kwa CCM ambao wao wanatoa taarifa polisi kwa kila kitu wanachokishuku na wanakua bega kwa bega na polisi kuhakikisha taarifa yao imefanyiwa kazi.
Wapinzani wao wanabaki kulalamika wakati hawatoi taarifa.
Mfano tu wamebiwa mawakala wawe na vitambulisho badala ya kutafuta vitambulosho au kwenda mahakamani kupinga au kuzuia kanuni hiyo kutumika wao wanataka kutunishiana misuli na mkurugenzi kwa kusem kuwa wataingia kwa nguvu wakati hawana nguvu.
Hakika watatolewa kwa nguvu na kura zitapigwa na CCM watatangazwa mshindi na wapinzani uchwara watabaki kulalamika mazuzu.

CCM nao na serikali yake wazuie uvunjifu wa amani kwa kutenda haki na hasa uhalifu dhidi ya binadamu. Ni laana kubwa kuona damu za watu zinamwagwa tena baada ya watu kuteswa sana bila kuona nguvu za kulaani na kuchukua hatua zikitumika.


Nchi hii ni ya mfumo wa vyama vingi na ni wajibu wa chama kinachoshinda uchaguzi kusimamia uhai na haki na sheria za nchi zisivunjwe kwa sababu yoyote ile hata kama inapelekea wao kushindwa.
Huwezi kusema unalinda Twiga ,tembo na nyoka wa porini halafu unashindwa kulinda ndugu zako na wanasiasa wenzako ambao kwa miaka mingi mmekua mkiishi kirafiki halafu ujiite wewe ni binadamu mwenye akili timamu.
Tulinde watu zaidi kuliko vitu.

Viongozi wa dini nao wasikae kimya.
Kuna dini nyingine wanajifanya kuwa urafiki wa viongozi wao na wanasiasa unawafanya wawe salama.
Wanajidanganya. Historia ya nchi kujawa na watawala waroho wa madaraka kwa kuwagawa watu hua haiachagi salama dini .
Leo hakuna ubaguzi wa kidini kwa sababu nguvu za wabaguzi wezielekeza kwa wanasiasa lakini wakiwamaliza wanasiasa watageukia dini. Watasema dini fulani hawafai kutawala nchi hii. Na watawabughudhi wale wenye ndoto za kutawala siku moja.


Watanzania tupendane wakati huu wa mwezi wa toba ya Kwaresma.
Tukumbuke kuwa Yesu aliuawa na serikali ya Kirumi baada ya kusingiziwa na wale walioamini katika itikadi za Kiyahudi .
Huu ulikua ni mfano mbaya kabisa kwa watawala wa kidunia kuua watu wasio na hatia.
Tujifunze maneno ya Yesu Masihi kwa kusema na kuomba Ufalme wa Mungu uje nchini mwetu.Watawala watawale kwa kumheshimu Mungu aliyetuumba wote na kutupa uhai kwa neema yake na mapenzi yake. Hakika tutaishi salama.
Ni rahisi kuua lakini sio rahisi kufuta dhambi na kuipa amani dhamira ya mtu aliyeua mtu asiye na hatia kwake.

Hofu ya Mungu na kujishusha ndiko kunakotufanya tuwaheshimu wengine kuwa nao wameumbwa ili waishi hapa duniani kama tulivyo sisi.
Utawala wa mwanadamu kwenye biblia umepewa namba 666 , ni utawala wa kujikweza na kujiinua juu kama mungu.Ni utawala unaofanana sana na utawala wa wenye kujitanua. Hautofautiani sana na utawala wa shetani kama utamweka Mungu pembeni.
Ni utawala usiopenda mambo ya dini dini mana unajiona kuwa uko juu ya sheriz zote.
Kwa hiyo watanzania tuwausie viongozi wetu wamwogope Mungu mmoja tu. Na wajitambue kuwa wao ni wanadam tu.
Turejee wote kwenye imani zetu zilizotufanya tutendeane mema.
Kila mtu afanye lile ambalo angependa yeye naye afanyiwe .


Kama Wanasiasa wa vyama vya CCM na Chadema watakubaliana na hali ya kuvuruga umoja wetu basi tutaliangamiza taifa letu. Hasa pale ambapo viongozi wa dini, waandishi wa habari na wananchi wasio na vyama wanakosa nafasi kubwa ya kukemea.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…