Taifa maskini linaloongozwa na Sheria zisizofaa. Inaingia akilini kumjengea nyumba aliyehudumu Serikalini miaka zaidi ya 20?

Pole mkuu,taifa lipo chini ya mashetani,yanabadilika rangi na jinsia tu
 
... unapoona the ruling class are fighting to remain in power sio mchezo Chief; wanajua wanachopata. Kwa maposho hayo nani atakubali kukabidhi madaraka kwa vikaratasi? Mtapigwa risasi wote muhimu chama kiendelee kutawala! Mbinu zote halali na haramu zitatumika kulinda madaraka.
 
Wanatia aibu sana hawa watu.
Huu ni unyonyaji wa Kiwango cha juu
Mwalimu aliuona katikati mwa miaka ya 60 ndo akapreempt azimio la Arusha na kuwafunga breki viongozi wa kisiasa la sivyo ukiwaachia hawa ni wanyonyaji wasio na kikomo!
 
Mkikumbushwa habari ya sheria na taratibu mpya (Katiba Mpya), mnapinga. Vumilieni tu!! Sehemu kubwa sana ya mapato ya serikali inatumika kuhudumia maisha ya viongozi wa serikali kuliko hata mataifa makubwa yaliyoendelea.

Umeme, maji, usafiri, nyumba ndio gharama halisi za maisha. Na nchi hii masikini bado inatoa huduma hizo kuanzia ngazi za chini kabisa wilayani!! Pesa za kuleta maendeleo zitaendelea kuwa kiduchu aka “kasungura kadogo”!

Vumilieni - hamtaki mambo haya yawe tofauti!
 
Kweli Nchi ya Hovyo kabisa licha ya kuwa mimi namkubali mama yetu SSH lakini kama hizi sheria zetu za hovyo zilizoasisiwa na umoja wa Sukuma Gang na Jiwe,AG kilangi,Speaker Bwana Yobu Ndugai na Jaji Mkuu Ismail Juma ni za hovyo Zikiwapa Kinga Kuanzia RAIS,WAZIR MKUU, MAKAMU WA RAIS,SPIKA NA NAIBU WAKE,AG NA JAJI MKUU(CJ)kutokushtakiwa na mhimili wowote ule iwe ni kabla na baada y kutoka kwenye madaraka zisipoondolewa kwa kutokufufua mchakato wa katiba mpya for sure WE GONNA DIE IN COCKROACH DEATH
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…