Taifa Stars waenda Cape Verde bila Dreamliner

Jiweeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeee njoo usikie wanavyomsema mtoto wako! Hawana adabu
Hili linalotokea ni sawa na babu kakaa na mjukuu, babu kajamba mjukuu ndio anakula kofi kuwa mbona anajamba hovyo? Ila waungwana wanajua nani hasa!
Inaitwa heshima kwa wakubwa. Mwakyembe vumilia tuu
 
Meli yetu ile? Acha masihara wewe! Kwa ule mwendo wake sii itafika Cape Verde mwezi February 2019?
 
kwa maana hiyo nikwamba viwanja vya Mwanza na Kilimanjaro ni vikubwa kuliko Uwanja wa Taifa wa Cape Verde?????
 
Mkuu tuliaa basiii... Usiwaseme hadharan Hawa wazeee.... Hahahahahahah aibu yao
 
MKUU KWA KUONGEZEA NDEGE ZOTE ZA ENGINE MBIL ZINAZOPITA ATLANTIC OCEAN FLIGHT PLAN YAO LAST PONT NI PALE, LAZIMA ZINATUMIA CAPE VERDE INCASE YA EMERGENCY HATA NASA WAMEWEKEZA SPACE SHUTTLE KUTUA KWA DHARURA
HII INATOKANA NA ETOPS REQUIREMENTS HIVYO HATA TAG ANGOLA YA RIO DE JENEIRO INAPITIA PALE
 

Ukigoogle utaona kabisa uwanja wa Praia Nelson Mandela una urefu wa 2.1KM inabidi ugoogle tena kuangalia minimum length ya uwanja wa Dreamliner kutua ukipata majibu uje sasa kupingana na hoja ya Mhe.Waziri.Dreamliners zinatua Cape Verde lakini si uwanja huo wa Nelson Mandela Praia.Kuna kisiwa kingine kina uwanja mrefu kwa ajili ya dreamliner ambapo wangetua huko wangetakiwa kusafiri (kwa boti? Au Charter) kuja Praia ambako ndiko Mchezo utafanyika wakaona ni usumbufu bora wakatue hapo hapo Praia(Nimemsikia vizuri Mhe.Waziri).Comments nyingi humu ni za kishabiki suala hapa ni je hizo sababu ni za msingi??Nakubaliana na wanaotoa hoja ya kwamba abiria 200+ hawakuweza kupatikana na hii ni kwa sababu pamoja na mambo mengine ya kiuchumi lakini pia muda ulikuwa mfupi mno tangu tangazo hilo litolewe.
 
Mkuu Vyamavingi Acha porojo na siasa za mwakyembe, weka vipimo vya uwanja wa Praia. Hizo ndege mnazoonyeshwa hakuna B787 naona ni A220 za Cote d'void na B737. Mie nahisi sababu kubwa ni TFF kushindwa kufika bei na ATCL wakachomoa which is right. Mengine ni siasa. Cape Verde in visiwa viwili vikubwa. Sal na huko Praia. Kisiwa cha utalii ni Sal na ndiko kwenye uwanja mkubwa kwa ajili ya madege makubwa unayoyasena. Praia ni makao makuu na mpira utachezwa huko.

QUOTE="Vyamavingi, post: 28710099, member: 251105"]Nimejisikia aibu sana kana Mtanzania pale Dk. Mwakyembe alipowadanganya Watanzania ati Dreamliner yetu haiwezi kutua uwanja wa ndege wa Cape Verde! Mwakyembe inaoneka ama haifahamu Cape Verde au ni mwanasiasa anayetumia ghiliba.

Kama umo humu Dk. Mwakyembe, nakufahamisha kuwa Cape Verde uchumi wake unategemea utalii, Watalii wanakwenda Cape Verde kwa maelfu na hawatumii charter na bombadier kufika huko, wanashuka kwa madege makubwa kuliko hiyo dreamliner.

Vv[/QUOTE]
 
Watu hawakugundua tangu mwanzo kuwa ilikuwa danganya toto kwasababu hiyo nauli ni kubwa mno. Walijua kabisa hakuna wataolipa hiyo nauli hivyo ndege haitakwenda. Na jiwe lazima alikuwa anaangalia tu pembeni anasema hiiiiii. Ndege ingejaa lazima jiwe angewachunguza hao watu.

Kuwaambia watu kuwa uwanja wa Praia ni mdogo kwa ndege yetu ilikuwa ni dharau tu ya kawaida ya viongozi kwa wananchi wao ambao wanawajua ni wajinga na wanadanganyika kirahisi, na siyo ishu kabisa.
 
Kwani lazima watue Praia, mbona wana uwanja mkubwa kimataifa unaitwa "Amílcar Cabral International Airport" urefu 3272m ktk kisiwa cha Sai
 
Inalinda kibarua chake, angesema ukweli ingethibitisha kua tuna hali ngumu kifedha jambo ambalo wakubwa hawataki tuseme
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…