Taifa Stars yafa kiume Kampala, yatoka 1-1 na Uganda

Taifa Stars yafa kiume Kampala, yatoka 1-1 na Uganda

bemg

JF-Expert Member
Joined
Apr 25, 2010
Posts
2,799
Reaction score
643
Kwaheri Tanzania michuano ya CHAN tujipange upya kwa kuwekeza soka la vijana
 
Acha unyanyapaa kufa kiume kitu gani, imesaidia nini. Sisi ni wahapahapa
 
Acha unyanyapaa kufa kiume kitu gani, imesaidia nini. Sisi ni wahapahapa

Wamejitahidi kama tulichapwa home 3-0 lakini Leo Bocco kafunga dk59 na wao kusawazisha dk85.Ndo maana nimesema tuwekeze kwenye soka la vijana ili tusiwe wahapahapa
 
Kufa kiume ndio nini?
Kwani kuna kufa kike?
Kufa ni kufa tu
Mpira hatujui
Kazi hatufanyi
Uchumi hatukuzi
Elimu duni
Siasa hatujui
Tumebaki kupiga makofi ya kinafiki na fitna tu ndio zetu
 
Siku zote tukijitahidi ni draw tu
hata mechi ya kushinda tunatoa draw

Tazama mshahara wa makocha ...wa Uganda na wa TZ,,,
 
Ni kweli taifa limekuwa haliendi mbele' mifumo yetu inatakiwa kuhuishwa na kuondoa upenzi wa kinafiki
 
Siku zote tukijitahidi ni draw tu
hata mechi ya kushinda tunatoa draw

Tazama mshahara wa makocha ...wa Uganda na wa TZ,,,

Siasa imeingia kila eneo ,tuliowapa dhamana ya kusimami mchezo wanaendeleza siasa tu.Timu ya vijana copa coca-cola iliyoenda Brazil ilitakiwa kuendelezwa lakini wapi tunang'ang'ana na wachenzaji walewale
 
Tanzania tuhamishiwe ule ukanda wa Tuvalu, Tahiti, Sao Tome And Principle, Republic of Nauru. Huko tutashiriki Word Cup kila siku.
 
Tanzania tuhamishiwe ule ukanda wa Tuvalu, Tahiti, Sao Tome And Principle, Republic of Nauru. Huko tutashiriki Word Cup kila siku.

Kwa team hii na siasa za TFF hatuwezi hata huko
 
Mkwasa atimuliwe fasta tumpe Julio,Nae akiharibu tunampa Tegete wote wafaidi huo mshahara
 
Imefika kipind cha kuwekeza katika soka.la sivyo tuache soka tufanye mambo mengine.inakera saana.
 
Wale Wa Toto walio chukua kombe Brazil wako wap?afu mbona mitaani kuna vijana wazuri zaid ya hawa wanao itwa taifa......z.kweli bola tufunge soka mpaka tutakapo pata m4c mijitu iko bizy na ten percent inakelaaa sana MPA kchwa knaenda upande kilakola tunafeli hakuna chakujivunia pamba......vuu kabisa.
 
Mimi lilishaachaga kuzinguliwa na hawa TAIF STRESS. Nashabikia timu nyingine siyo hii maana haitabiriki kama maji ya ziwa victoria.
 
Wale Wa Toto walio chukua kombe Brazil wako wap?afu mbona mitaani kuna vijana wazuri zaid ya hawa wanao itwa taifa......z.kweli bola tufunge soka mpaka tutakapo pata m4c mijitu iko bizy na ten percent inakelaaa sana MPA kchwa knaenda upande kilakola tunafeli hakuna chakujivunia pamba......vuu kabisa.

mmoja wao yuko serengeti anacheza timu ya kijiji
 
Hadi naikumbuka tfa ya akina ndolanga huyu malinzi tulimpa kichwa sana humu.
 
Kufa ni kufa tu, hamna kike wala kiume. Lakini ni mwanzo mzuri kwa mkwasa ukiangalia mda aliokaa na timu
 
Back
Top Bottom