Taja Jina zuri Kwa mtoto

Taja Jina zuri Kwa mtoto

Heshima Comrade?.

Umesema majina huwa yanaamua hatima (Fate) ya watu maishani?. Kivipi?, naomba ufafanuzi katika hili.

Hujawahi kuwaona kina Masumbuko, Taabu, Shida, Kabaya, Matatizo, na kadhalika wametoboa maishani?. Unaishi wapi uje nikuonyeshe hao watu unaowaita hawajawahi kutoboa?. Pia ulikokuita kutoboa ndiyo nini?. Ni kwa kutumia vigezo vipi vya kimantiki ndipo mtu awe ametoboa kwako?.

Pia n'nawafahamu kina David, Davy, Daud na kadhalika ambao wana maisha ya kawaida tu na hawana vigezo hivyo ulivyovitaja. Pia ulikokuita kupendwa na Mungu ndiyo jambo gani?. Unaweza kulithibitisha hili la Mungu kumpenda mtu?.

My Take,

Kama ni Majina tuwape wenetu majina ya Kiafrika na yenye tafsiri yenye kuzingatia mantiki na si nje ya hapo. Kukopa jina kwa namna yeyote ile kutoka ng'ambo ni kielelezo cha namna Fikra zetu zilivyo za hovyo (kumradhi).

Hekima Ni Uhuru.
Heshima kwako Mkuu.
Kwanza nakupongeza kwa msimamo wako wa kizalendo wa kulinda tamaduni za kwetu.
Pamoja na kukupongeza nakuomba utuorodheshee majina ya kiafrika yenye kufaa kuwaita watoto wetu.
 
Kwahio mzee unataka kunishurutisha niombe radhi? Hahahahaa afu utawaambiaa mods sioo.....Kazaa yeye au mimi? au kasaidiana na mods kuzaa??...kuzaa mzae nyiee keroo mtupe sisi Hahahaa

Lengo langu si ovu Comrade. Ni katika kusahihishana tu na si kudhalilishana.

Hukutumia uungwana kumuita member mwenzio mpuuzi. Si Lugha nzuri katika Forums, ungetumia uungwana mbona sina tatizo Mkuu?.

Iishi "signature" yako Comrade. Utakuwa philosopher mkubwa sana.

Kumradhi.
 
Heshima kwako Mkuu.
Kwanza nakupongeza kwa msimamo wako wa kizalendo wa kulinda tamaduni za kwetu.
Pamoja na kukupongeza nakuomba utuorodheshee majina ya kiafrika yenye kufaa kuwaita watoto wetu.
Mimi ni Mtanzania Comrade.

Kukutajia majina sina weledi sana katika hilo. Ninachoweza kukushauri ni hili "Mpe mwanao jina la Taifa lako lenye tafsiri bora". Usimpe mwanao jina la kukopa. Ni udunya na upeo mdogo wa uelewa wa mambo.

Majina ya Kiswahili kama Busara, Akili, Hekima, Faraja, Fanaka, Nuru, Tumaini, Baraka, Shangwe, Mzalendo, Bora, Huruma, Waridi, Furaha na kadhalika ni baadhi tu. Ni majina yenye maana nzuri na yenye kuonyesha uzalendo kwa Taifa lako kupitia majina.

Hekima ni Uhuru.
 
Ita mwanao jina la kiafrika Ashanti,Menelik,etc kuwapa watoto majina ya kiarabu na kizungu ni kuendeleza utumwa wa kifikra na kitamaduni.kwangu mimi Palamagamba ni bora zaidi kuliko Smith/Rob/Jackson/Whitney etc
 
Heshima Comrades.

Nimefuatilia kwa umakini mpana sana uzi huu. Nilichojifunza ni kwamba "Tumekosa Utamaduni Uhuru. Tunaelekea kuuzima kabisa utamaduni wetu", sababu ni nini lakini?. Usomi, utumwa mamboleo, ulimbukeni na maisha au nini?.

Yaani hatuguswi kabisa kuuenzi utamaduni wetu kupitia majina?. Majina ya kizunugu, kiarabu, kijerumani ya nini?.

Kuanzia Wachina, Waarabu, Wajapani, Wakorea, Wayahudi, Wafini, Waswedi na orodha inaendelea wana Majina yao ya asili. Kwanini sisi Afrika ndiyo wenye kasumba ya kuazima majina yao?.

Halafu eti mtu ana-comment {Fuata mambo yako, si uyataje na wewe jina unalolipenda} ?, serious?. N'nani alisema kuwa mtu mmoja mmoja ana uwezo wa kuwa mjenzi wa maaadili?. Na kwanini tu wepesi wa muendelezo wa falasafa ya kila mtu na lkwake badala ya kuwa sauti moja, utamaduni mmoja na kadhalika?. Shabaha yetu kama Taifa ni ipi katika Utamaduni, sanaa na michezo?.

Jina kama Francis, Errard, Dickson, Ekhart, Nasrat, Yvonne ya nini haswa wakati hata kuyatamka na uandishi wake hatuuwezi?.

Mbona tuna majina mengi mazuri ya kiswahili?. Ni kwanini tusijivunie hayo?. Tutafakari...

Tuguswe na kuendeleza utamaduni wa Mwafrika kupitia majina, mavazi, vyakula, nywele, rangi ya ngozi na kadhalika.

Wapo Wamarikani wengi wa Kaskazini wenye majina ya Kiswahili ambao nimewapenda mno kwa kuuenzi utamaduni wa Kitanzania. Kwa uchache tu ni kama wafuatao;

Talib Kweli (mwanamuziki wa Rap), Amiri Baraka (mwandishi, mwanaharakati, na mshairi), Haki Madhubuti (mshairi), Maulana Karenga (mwanzilishi wa sikukuu ya Wamarekani Weusi yenye jina la Kiswahili, Kwanzaa na Mkurugenzi wa Idara ya Masomo ya Waafrika katika Chuo Kikuu cha California, Berkley) na mke wake Tiamoyo Karenga, Maisha Ongoza, Mapinduzi Leo, Rafiki Mtumishi, Malaika Jabali (mcheza sinema), Fani Adili, Harambee Afrika, Ujamaa Muhammad, Akili Mali, Sheria Haki, Mtoto Wa Afrika, n.k.

Elimu ya kweli ni kujielewa, kuielewa jamii na kuuelewa ulimwengu. Usipoijua historia yako unakuwa sawa na mti usio na mizizi-Marcus Garvey (Yohana Mbatizaji wa watu weusi)

USHAURI.

Tuachane na Utumwa Mamboleo. Tuuenzi utamaduni wetu kwa kuwapa Wenetu majina ya Asili yetu na Utanzania. Tuachane na majina ya Kiarabu, Kiyahudi na Kizungu. Tuchague majina yetu yenye tafasiri nzuri na Kuwapa wenetu.

Ruhuksa kunikosoa na Kunielimisha.

Hekima Ni Uhuru.
We waitwa nani kwa jina la kibantu ( kiswahili??)
 
Mimi ni Mtanzania Comrade.

Kukutajia majina sina weledi sana katika hilo. Ninachoweza kukushauri ni hili "Mpe mwanao jina la Taifa lako lenye tafsiri bora". Usimpe mwanao jina la kukopa. Ni udunya na upeo mdogo wa uelewa wa mambo.

Majina ya Kiswahili kama Busara, Akili, Hekima, Faraja, Fanaka, Nuru, Tumaini, Baraka, Shangwe, Mzalendo, Bora, Huruma, Waridi, Furaha na kadhalika ni baadhi tu. Ni majina yenye maana nzuri na yenye kuonyesha uzalendo kwa Taifa lako kupitia majina.

Hekima ni Uhuru.
Busara ( wisdom) Akili ( Brain) Wema ( goodheart) Furaha ( happyness) Majina yanatafsirika kwa kila kabila.
 
We waitwa nani kwa jina la kibantu ( kiswahili??)
Heshima Comrade.

Ukisoma The Federalist Papers na kujua kwanini Publilius, Mark Twain, Voltaire, George Orwel, waliitwa hivyo kamwe usingejisumbua kujua jina langu halisi. Kimantiki, haitokusaidia lolote.

Kumradhi.
 
Lengo langu si ovu Comrade. Ni katika kusahihishana tu na si kudhalilishana.

Hukutumia uungwana kumuita member mwenzio mpuuzi. Si Lugha nzuri katika Forums, ungetumia uungwana mbona sina tatizo Mkuu?.

Iishi "signature" yako Comrade. Utakuwa philosopher mkubwa sana.

Kumradhi.
sawaa mkuu kumbe hukuwa na nia mbayaa sorry kwako na kwake pia
 
Back
Top Bottom