Heshima Comrades.
Nimefuatilia kwa umakini mpana sana uzi huu. Nilichojifunza ni kwamba "Tumekosa Utamaduni Uhuru. Tunaelekea kuuzima kabisa utamaduni wetu", sababu ni nini lakini?. Usomi, utumwa mamboleo, ulimbukeni na maisha au nini?.
Yaani hatuguswi kabisa kuuenzi utamaduni wetu kupitia majina?. Majina ya kizunugu, kiarabu, kijerumani ya nini?.
Kuanzia Wachina, Waarabu, Wajapani, Wakorea, Wayahudi, Wafini, Waswedi na orodha inaendelea wana Majina yao ya asili. Kwanini sisi Afrika ndiyo wenye kasumba ya kuazima majina yao?.
Halafu eti mtu ana-comment {Fuata mambo yako, si uyataje na wewe jina unalolipenda} ?, serious?. N'nani alisema kuwa mtu mmoja mmoja ana uwezo wa kuwa mjenzi wa maaadili?. Na kwanini tu wepesi wa muendelezo wa falasafa ya kila
mtu na lkwake badala ya kuwa sauti moja, utamaduni mmoja na kadhalika?. Shabaha yetu kama Taifa ni ipi katika Utamaduni, sanaa na michezo?.
Jina kama Francis, Errard, Dickson, Ekhart, Nasrat, Yvonne ya nini haswa wakati hata kuyatamka na uandishi wake hatuuwezi?.
Mbona tuna majina mengi mazuri ya kiswahili?. Ni kwanini tusijivunie hayo?. Tutafakari...
Tuguswe na kuendeleza utamaduni wa Mwafrika kupitia majina, mavazi, vyakula, nywele, rangi ya ngozi na kadhalika.
Wapo Wamarikani wengi wa Kaskazini wenye majina ya Kiswahili ambao nimewapenda mno kwa kuuenzi utamaduni wa Kitanzania. Kwa uchache tu ni kama wafuatao;
Talib Kweli (mwanamuziki wa Rap),
Amiri Baraka (mwandishi, mwanaharakati, na mshairi),
Haki Madhubuti (mshairi),
Maulana Karenga (mwanzilishi wa sikukuu ya Wamarekani Weusi yenye jina la Kiswahili, Kwanzaa na Mkurugenzi wa Idara ya Masomo ya Waafrika katika Chuo Kikuu cha California, Berkley) na mke wake Tiamoyo Karenga, Maisha Ongoza, Mapinduzi Leo, Rafiki Mtumishi, Malaika Jabali (mcheza sinema), Fani Adili, Harambee Afrika, Ujamaa Muhammad, Akili Mali, Sheria Haki, Mtoto Wa Afrika, n.k.
Elimu ya kweli ni kujielewa, kuielewa jamii na kuuelewa ulimwengu. Usipoijua historia yako unakuwa sawa na mti usio na mizizi-Marcus Garvey (Yohana Mbatizaji wa watu weusi)
USHAURI.
Tuachane na Utumwa Mamboleo. Tuuenzi utamaduni wetu kwa kuwapa Wenetu majina ya Asili yetu na Utanzania. Tuachane na majina ya Kiarabu, Kiyahudi na Kizungu. Tuchague majina yetu yenye tafasiri nzuri na Kuwapa wenetu.
Ruhuksa kunikosoa na Kunielimisha.
Hekima Ni Uhuru.