Taja rafiki ambaye alifariki dunia mapema sana na huwezi kumsahau!

Taja rafiki ambaye alifariki dunia mapema sana na huwezi kumsahau!

Najim jamaa hakuwahi kuwa ndugu yangu wala rafiki lakini alinisaidia bila hata ya kunijua zaidi ya kuonana tu eneo moja kila siku.

Kipindi ambacho nilikuwa ugenini na wale waliopaswa kuwa marafiki na ndugu wote walinitosa kama hawanijui.

Najim alikuwa anazuga kunialika kwake na mkewe mida ya chakula kuzuga tupige story kumbe alijua hata mlo wangu ulikuwa wa tabu.

Nilipokosa pa kukaa Najim alikwenda kulipia store na kuibadilisha kuwa chumba na kuniambia kuwa ana chumba hakitumii nijishikilize mpaka nikikaa sawa.

Jamaa akanifundisha mbinu za biashara yake na mwisho kunifanya partner kwenye biashara kiasi cha kugawana faida nusu kwa nusu bila ya kuchangia hata shilingi.

Ila ndio vile chema hakidumu. Ila usihofu bro, sikuwahi kwenda kinyume na ahadi yangu kwako. Binti yako mkubwa nimemuozesha mwaka jana. Nilisimama kama baba. Na ambayo hakuwahi kutimiza lakini ulitaka yatimie nakuhalkikishia yametimia na ziada juu.

Sijalipa hata robo ya fadhila zako kwangu ila sitoacha kukuombea daima Allah akupe pepo ya daraja la juu kabisa.
 
Huyu nashindwa nifupisheje.. any way

Katika Nesi maarufu LUDEWA ni wewe. Maana ulipata ajali mara nne au tano na mara nyingi ni wakati ukipigania maisha ya watu wa Ludewa. Wakati ule miundo mbinu ya Ludewa ilikuwa katiri sana. Ni nani angethubutu kufika ukisi milimani miaka ile kuwasaidia kina mama kujifungua?? Hukuwa unajali posho wewe.

Nyumbani kwako wanao uliwaondoa siku nyingi mkawa mnaishi na mumeo. Mmoja amelelewa na anti ake wa ludewa tangu utoto na mwingine alienda Ilembula. Nahisi majukumu yako ya unesi yalikutinga au ndo vile ulijua hauna maisha kutokana na maradhi ya kichwa yaliyosababishwa na maajali ya mara kwamara kazini.

Siji sahau siku umelazwa unaumwa kichwa umepigwa drip umezidiwa ulivyoambiwa mzee furani unaumwa uliwaambia manesi wenzio drip si kitu unaomba ukamtibu, waliposema maliza drip kwanza nakumbuka ulikunywa mbele yao ( Ulikuwa katiri kwa mwili wako) ukaenda kumtibu yule mzee baba mkwe wako.

Siku niliambiwa uliumwa ghafra na madaktari walishindwa kuokoa mwili wako shangazi yangu kijana wewe ambaye maana umezaliwa 70s na kutoweka 2013.

Niliangalia simu yangu sikuamini kwani simu yangu last call ni wewe na tuliongea sanaa last night ukanambia unaumwa kichwa kidogo kumbe haupo sawa.

Radio Ludewa ilipiga nyimbo za maombolezo na ludewa nzima waliomboleza. Umetuacha Nesi mpambanaji wanabaki hawa wasio jali.
RIP
 
Mimi vifo vyote huwa vinaniuma nimjue nisimjue huwa najua kwa kifo chake huyo marehemu yupo mama analia,baba analia mtoto analia mke au mume analia yeye mwenyewe marehemu mipango yake yote imepotea.

Wakati mwengine mtu simjui nikiona umri aliiondoka nao huwa natokwa machozi kabisa,hakuna anayekipenda kifo ila ndiyo hakuna namna kukwepa muhimu kuwaombea waliotangulia huku sisi tukijiandaa na yetu.
 
Ilikuwa siku ya juma 5 ya mwezi wa 3 mwaka 2018, asubuhi mapema najiandaa kwenda mishe mara simu inaita..

Ssuti upande wa pili: (Bila salamu),njoo kwa bro wako hapa Temeke fasta Kuna tatizo.(Simu ikakata Bila Mimi kujibu chochote).

Ilenimeshatoka home Huku nimepagawa naelekea uelekeo wa kwa bro,njiani nakutana na mtu ninayemjua. Kabla ya salamu jamaa ananiambia pole sana Satoh hirosh,Mimi naelekea kazini kuomba ruhusa kisha tutakuwa pamoja. Dah ile siku ilibaki kidogo nizimie mana mpaka hapo sijajua nini kimetokea ingawa hisia za kifo zilishaniingia. Mdomo mzito unaogopa kumuuliza jamaa,Kuna nini kwa kaka?

Nafika home kwa bradha napokelewa na vilio vya wanawake uani. Shemeji yangu ananiona akaongeza kulia na kuniambia kwa sauti ya uchungu "kakaako hatunae Tena nitaishi vipi Mimi na huyu mtoto mdogo pekeyangu shemeji"

Ile siku nililia kama mwanamke. Imekuwaje kaka amefariki ghafla wakati Jana usiku niliongea nae kwenye simu.

Wazee wakaniita waniambie kilichotokea.

"Kijana jikaze maana wewe ndiye unategemewa sasa hivi kuongoza shughuli ya msiba na kupokea wageni wa mikoani.

Kilichotokea ni kuwa;

Jana jioni kakaako alitembelewa na rafiki yake mkubwa ambaye ni askari pale ukonga. Leo asubuhi akamcheki bodaboda wake (bro alikuwa ana pikipiki akamkabidhi jamaa aendeshe kisha amletee pesa kwa wiki,yeye ana mishe zake zingine). So kwa heshima ya rafiki yake,ile Jana yake jioni akamcheki jamaa wa pikipiki aje kuilaza home(kwa bro) ili asubuhi bro mwenyewe awahi kumpeleka mshikaji wake kazini ukonga kisha akirudi anarudisha pikipiki kwa boda wake na yeye kuendelea na mambo yake.

Asubuhi ya umauti,wakajiandaa vizuri na safari ikaanza hadi ukonga. Wakati anarudi home .. Daah!!

Dereva wa Fuso akitokea kisarawe akamgonga Bradha kwa nyuma na kumrusha service road kifo kikamkuta hapo hapo na kisha gari ikaiburuza pikipiki mita kadhaa. Konda wa Fuso ndiyo alimstua dereva.

"Oya umemgonga mtu wa pikipiki mwanangu alafu pikipiki ipo chini ya gari unaiburuza"

kumbe dereva alikuwa anaendesha gari Huku amelala( inaonekana alikesha usiku). Akastuka na kufunga breki...

Inaita uchungu kusimulia. Ila nakumbuka Mimi na yule askari mshikaji wake tulilia kama watoto mana kifo cha ghafla kinauma asee!!

REST IN PEACE KAKA,mwanao D ulimwacha darasa la 6 ule mwaka 2018,juzi TU hapo matokeo ya form 4 yametoka. Hajafanya vizuri sana kutokana na changamoto za kulelewa na single mama,Mimi nikiwa kama baba ila baba mdogo,ila nakuahidi nitajitahidi kadili ya uwezo wangu aende chuo.
 
2pac classmate wangu,he died at the age of 25, lakini legacy ameacha ni kubwa.
 
Juma, hakika wewe ulikua na tabia njema.... pumzika kwa amani katika Nyumba ya Milele Rafiki yangu
 
Back
Top Bottom