Taji Apewe Mshindi wa Tatu

Taji Apewe Mshindi wa Tatu

Kwa kuwa ni wazi kuwa Dada Sitti Mtemvu atavuliwa taji kwa kudanganya umri na kuongoe kifaransa ili kukwepa maswali napendekeza Taji apewe yule mshindi wa tatu.

Nadhani yule ana sifa zote za kuwa Miss TZ.

NB
Ni hawa hawa kina Lundenga walimtema Miriam Odemba lakini leo ni maarufu Duniani.

http://en.m.wikipedia.org/wiki/Miriam_Odemba

Ww ndio utakua huyo mshindi wa tatu
 
Endapo akipewa mshindi wa tatu lazima yataibuka maneno pia...Mimi naona wale top 5 washindanishwe tena ili tumpate mrembo halali...


Litakuwa jambo la ajabu sana. Kinachozuia mshindi wa pili asipewe ni kitu gani? Nahisi hili suala halina mjadala, Sitti akijivua/akivuliwa, automatically wa pili anachukua nafasi yake.
 
Mbona mbowe alipopiga picha anakula denda mbele ya wanawe mlisema ni mambo ya kawaida!!! Au kunya anye kuku, akinya bata kaharisha? Acheni double standard bana. Mkiamua kukosoa toeni kwanza mahaba na chuki zenu ndio mtakua mnaeleweka.
Punguza mahaba kijana yule bibi bomba alikuwa amevaa nguo za juu tu.
 
Hivi baba wa Kiafrika kupiga picha na binti yako akiwa kwenye mavazi haya hii ni adabu ya wapi?

Tena muislam anayejua maadili yote ya dini, huyu mtemvu ni sheeeeda, kazi yake kupeleka wadogo zetu uarabuni tu, simpendi huyu mzee basi tu
 
Kwa nini mshindi wa pili arukwe? Na huyo mshindi wa tatu wa kuitwa Jihan anapigiwa chapuo sana. Ipo namna....
 
Sorry wanaJF.
Ninaomba mrejee kwenye mada nimefanya masahihisho.
Kuna makosa yaliyofanywa na baadhi ya blogs kuwa Lilian Kamazima ni mshindi wa tatu.
Nilimlenga Lilian kuwa anastahili kuwa miss Tz
 
Back
Top Bottom