Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
😉 utalala wap kwamfano!?!! Mkuu tulime bangi tu polis wakitudaka yatazungumzika,ila sio huyo kiumbeHa ha ha kweli kabisa yani usipomkuta bandani hata hautalala usiku huo
Mijoka hii hii ambayo ikionekana tu tunakimbiana?Bei ya sumu hutofautiana kulingana na nyoka.mfano
1.Gram ya puff adder venom ni $202
2.Boomslang bei yake ipo juu kuliko nyoka yeyote yule $4800
3.koboko $500
Hivyo bei ya venom hutofautiana na aina ya nyoka,sasa kazi ni wewe kupata license na kuchagua aina ya nyoka unaowahitaji au kuona watakuletea faida kubwa.
Aidha kuhusu namna ya kutoa sumu ,nyoka hukamatwa kwa ustadi kupitia kifaa special ,fimbo special yenye kibanio na pia nyingine iliyochepuka ambayo husaidia kumbana nyoka shingoni karibu na kichwa ,ukishamkamata nyoka kichwa hatua inayofuata ni kutafuta chombo special cha kuwekea sumu hiyo.mfano umechukua bakuli dogo,au chombo chochote kile unafunga plastic juu yake kama vile mfuniko huku ukiwa umemshika nyoka kichwa na wakati huo mdomo wa nyoka utakuwa wazi usiokuwa na madhara kwako wewe kisha unamuinamisha kwenye chombo husika na fangs za nyoka zitagonga au kuchoma plastic uliyoiweka juu na kumwaga sumu ndani,njia zipo nyingi tu
![]()
![]()
Soko ya venom ipo USA ,India ,China ,S.Africa
Lakini wengi hupeleka China sababu huko wengi ndio wanahitaji kwa wingi.
Unapeleka na ufuate utaratibu na sheria mfano December 2016 India waliwakamata smugglers 5 waliokuwa na venom yenye thamani ya $30Million ,walikuwa wanasafirisha kimagendo na walikuwa wanawauzia druglords ambao pia hutumia venom kutengenezea drugs
![]()
Lipo mbeya nashukuru Mungu mambo yanakwenda vizuri,nawashukuru watu wa Mali asili kwa ushirikiano na ushauri wanaonipatia
🙂 🙂 🙂 🙂 🙂Hii ni zaidi ya Kilimo kwanza!Hii inaitwa Kifo Kwanza