TAKUKURU kuwahoji Wabunge 69 kuhusu matumizi ya pesa za CHADEMA

TAKUKURU kuwahoji Wabunge 69 kuhusu matumizi ya pesa za CHADEMA

Suley2019

JF-Expert Member
Joined
Oct 7, 2019
Posts
2,203
Reaction score
5,610


JUNI 10, 2020
TAKUKURU MAKAO MAKUU KUHOJI WABUNGE 69 MATUMIZI YA FEDHA ZA CHADEMA

Kwa taarifa hii, tunapenda kuuthibitishia umma kwamba ni kweli kuwa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa – TAKUKURU Makao Makuu, imewaita Waheshimiwa Wabunge wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo – CHADEMA na waliowahi kuwa wabunge wa chama hicho kwa ajili ya mahojiano.

Hatua hii inafanyika ikiwa ni mwendelezo wa uchunguzi unaoendeshwa na TAKUKURU Makao Makuu wa malalamiko dhidi ya matumizi ya fedha za Chama cha Demokrasia na Maendeleo – CHADEMA ambapo hatua iliyopo sasa ni ya kuwahoji Wabunge sitini na tisa (69) – wanachama na waliowahi kuwa wanachama wa chama hicho.

Fedha hizi ni zile ambazo zililalamikiwa na waliokuwa Wabunge wa chama hicho ambao walitangaza kukihama chama chao ambapo katika malalamiko yao walidai kwamba walikuwa wakikatwa fedha katika mishahara yao kila mwezi kuanzia mwezi Juni 2016.

Kwa mujibu wa malalamiko hayo kila mwezi – Wabunge wa Viti Maalum walikuwa wakikatwa kiasi cha shilingi 1,560,000 na Wabunge wa kuchaguliwa kwenye Majimbo walikuwa wakikatwa shilingi 520,000 na kwamba hawakuwa wakifahamu namna ambavyo fedha hizo zimekuwa zikitumika.

Kwahiyo, tunapenda kuujulisha umma kwamba, kama ambavyo Mkurugenzi Mkuu wa TAKUKURU Brigedia Jenerali John Mbungo alivyoviambia vyombo vya habari Mei 27, 2020 ni kwamba uchunguzi dhidi ya tuhuma hii tayari ulisha anzishwa na baadhi ya wahusika walishaanza kuhojiwa.

Tunafanya hivi kwakuwa yawezekana katika tuhuma hii kukapatikana makosa yafuatayo:

  • Ubadhirifu na ufujaji wa fedha za chama
  • Matumizi mabaya ya mamlaka
Makosa haya yote yanaangukia katika Sheria ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa Namba 11 ya Mwaka 2007 ambayo ndiyo inayoongoza chombo chetu.

Mpaka sasa tayari tumeshafanya mahojiano na:

  • Viongozi wa CHADEMA
  • Viongozi waliowahi kuwa CHADEMA
  • Wabunge waliotoa taarifa
  • Maafisa wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi
  • Viongozi wa Bodi ya Wadhamini wa CHADEMA na sasa tunawahoji
  • Wabunge wanachama wa CHADEMA pamoja na
  • Wabunge waliowahi kuwa wanachama wa CHADEMA.

Mahojiano haya ambayo yanafanyika katika Ofisi za TAKUKURU Makao Makuu – Dodoma kuanzia leo - yanatarajiwa kukamilika wiki ijayo.

IMETOLEWA NA:
Doreen J. Kapwani
AFISA UHUSIANO – TAKUKURU MAKAO MAKUU


1591767108851.png

1591767206773.png

1591767230957.png
 
Katiba ya Chadema ( a party legal document) iko bayana kuhusiana na suala la michango ya wabunge kwenye Chama na matumizi ya michango husika.

PCCB haihusiani na kupanga matumizi ya pesa za chama, isipokuwa vipaumbele vya chama husika kama viwekwavyo na kusimamiwa na maamuzi ya vikao vya chama husika.

Mzee Yusuph Makamba bado analalamikia CCM kumtolipa pensheni yake, kwa nini PCCB haijakwenda kuchunguza huko? Pengine PCCB inafahamu fika kuwa huko ni nje ya mipaka yake.

Wanachotaka kukifanya Chadema ni mchezo mchafu. Makosa anayoyataja Kapwani ni potential detention kwa viongozi/watendaji wakuu wa Chadema kabla ya Uchaguzi Mkuu 2020.

Hizi ni njama za ku-weaken upinzani hapa nchini. Ni dhahiri CCM/Serikali ina hint fulani kuhusu potential serious opposition kupitia Chadema, come election 2020.
 
Taasisi ya Kuuzuia na Kupamban na Rushwa TAKUKURU imewaita Leo wabunge 69 wa Chadema wa zamani na wa sasa kuhojiwa kuhusiana na matumizi ya fedha walizokuwa wanakatwa kwenye mishahara yao kila mwezi.





20200610_114201.jpg
 
Hongera sana Takukuru lini mnaanza uchunguzi wa 1.5 T? Pia zile Trilion 490 za Barrick/Acacia nasikia tunapata kishika uchumba pekee $300M kwa mafungu.

Peleka malalamiko takukuru kuhusu hiyo 1.5 t kam una ushahidi, kwanza uhojiwe ilitumikaje kisha watuhumiwa wataitwa.
 
TAKUKURU mkimalizana na CHADEMA pigeni hodi na CCM mkawa hoji wabunge na vingozi wa 'chama', na kwenyewe wabunge 'wanachangia' shuguli za chama chao ni vizuri wananchi tukijua matuzimi ya hiyo 'michango'.
 
Katiba ya Chadema ( a party legal document) iko bayana kuhusiana na suala la michango ya wabunge kwenye Chama na matumizi ya michango husika.

PCCB haihusiani na kupanga matumizi ya pesa za chama, isipokuwa vipaumbele vya chama husika kama viwekwavyo na kusimamiwa na maamuzi ya vikao vya chama husika.

Mzee Yusuph Makamba bado analalamikia CCM kumtolipa pensheni yake, kwa nini PCCB haijakwenda kuchunguza huko? Pengine PCCB inafahamu fika kuwa huko ni nje ya mipaka yake.

Wanachotaka kukifanya Chadema ni mchezo mchafu. Makosa anayoyataja Kapwani ni potential detention kwa viongozi/watendaji wakuu wa Chadema kabla ya Uchaguzi Mkuu 2020.

Hizi ni njama za ku-weaken upinzani hapa nchini. Ni dhahiri CCM/Serikali ina hint fulani kuhusu potential serious opposition kupitia Chadema, come election 2020.

Katiba ya chadema imejieleza kuwa matumizi ya pesa hizo lazima yapitishwe na mkutano mkuu na kamati kuu na pengine kwa wingi wa wajumbe,
sasa kama hilo. halikufanyika unatetea nini?
Pia kuna mchangiaji humu alisema kuwa katiba ya chadema haikumfungamanisha mwenyekiti kwenye kwenye mambo ya pesa kama signatories lakini nasikia yeye ndo master sasa hapo sio matumizi mabaya ya madaraka?
 
TAKUKURU mkimalizana na CHADEMA pigeni hodi na CCM mkawa hoji wabunge na vingozi wa 'chama', na kwenyewe wabunge 'wanachangia' shuguli za chama chao ni vizuri wananchi tukijua matuzimi ya hiyo 'michango'.
Nadhani kama sikusahau,Timu Bashiru alishalifanyia kazi hilo! Ila hakuna aliyefikishwa kwenye Mahakama ya Mafisadi baada ya kugundua makaburi yakifukuliwa huenda hakuna atakayesalimika.Na haijulikanai hata ripoti yake ilishia wapi.
 
Katiba ya Chadema ( a party legal document) iko bayana kuhusiana na suala la michango ya wabunge kwenye Chama na matumizi ya michango husika.

PCCB haihusiani na kupanga matumizi ya pesa za chama, isipokuwa vipaumbele vya chama husika kama viwekwavyo na kusimamiwa na maamuzi ya vikao vya chama husika.

Mzee Yusuph Makamba bado analalamikia CCM kumtolipa pensheni yake, kwa nini PCCB haijakwenda kuchunguza huko? Pengine PCCB inafahamu fika kuwa huko ni nje ya mipaka yake.

Wanachotaka kukifanya Chadema ni mchezo mchafu. Makosa anayoyataja Kapwani ni potential detention kwa viongozi/watendaji wakuu wa Chadema kabla ya Uchaguzi Mkuu 2020.

Hizi ni njama za ku-weaken upinzani hapa nchini. Ni dhahiri CCM/Serikali ina hint fulani kuhusu potential serious opposition kupitia Chadema, come election 2020.
Akili yako inawalakini
 
50% ya watakaohojiwa wameshakihama chama na hata salamu hawapewi. Tutarajie nini?

Wasisahau na swala la Mwenyekiti kukikopesha chama.

Je ana leseni ya kufanya biashara hiyo?

Isije kuwa ni chaka la kutakatishia pesa!

"Kwa hizi vurugu za kitatange,je demani kutakalika?"
 
Nadhani ule mchakato wa kukifuta chama cha CHADEMA ndiyo umeanza rasmi!
 
Back
Top Bottom