DOKEZO TAKUKURU na Usalama wa Taifa, fuatilieni haya; nchi inahujumiwa. Kuna rushwa, urasimu na ufisadi mkubwa

DOKEZO TAKUKURU na Usalama wa Taifa, fuatilieni haya; nchi inahujumiwa. Kuna rushwa, urasimu na ufisadi mkubwa

Hili ni dokezo maalum toka kwa mwananchi mtumiaji wa JF mwenye nia ya kuusaidia umma kuwa na taarifa 'maalum'
Kwa hali hii ambayo nchi inapitia, uongozi mbovu, rushwa, ubinafsi, ufisadi, nepotism na vetting mbovu, uonevu nk tatizo ni TISS.
Nimekusoma hadi mwisho bila kupumua! Ahsante sana, mkuu 'TrueVoter'.

Mara nyingi tumekuwa tukipotoshwa sana juu ya taasisi hii ya TSS, ni kama kila mtu anayo hadithi yake kuihusu tofauti na wengine.
Leo, kwa mara ya kwanza kabisa umeleta taarifa iliyo tofauti na yenye maana zaidi.

Sijawahi kukusoma humu JF, nashukuru leo nimepata fursa ya kujifunza jambo jipya toka kwako.

Hii ndiyo faida ya kuwa na JF, kila mara kuna jambo jipya la kujifunza.
 
Soma tena kwa utulivu utaelewa ninachokisogeza mbele ya meza ya mfalme..
Siyo rahisi kuielewa jinsi ulivyoiweka.
Nami nilimezea tu nilipokusoma na kuanza kushangaa leo imekuwaje?
 
Nimesoma ripoti yote hakuna la uongo hata moja

1. Kwenye hilo la NIDA mpaka 50 watu wanapokea.. Rushwa!
2. La mbagala hili lilishasemwa sasa! Mpaka namna tenda ilivyopatikana.. Rushwa!
3. La petrol kuna andiko limeichambua vizuri mno.. Rushwa!
4. La LATRA ni mulemule.. Rushwa..!

Ni rushwa ni rushwa ni rushwa mwanzo mwisho! Lakini si tunakumbuka angalizo la mkuu wa kaya kuhusu kula kwa urefu wa kamba? Dosari ilianzia hapo
Na sasa nasikia humo maofisini watu hawakai ni uzembe uzembe na rushwa , hakuna usimamizi
 
4. Nauli za mabasi za LATRA.

Hivi mnajua mabasi yote ya mikoani katika stendi zote za mikoani wanachaji nauli zaidi ya zile zilizoidhinishwa na LATRA?!

USHAHIDI upo.

Hapa namaanisha hata LATRA na mapolisi wanalijua hilo. Je, ni fungu wanapewa au kuamua kuacha tu unyang'anyi huu uendelee?!

Nasisitiza iko hivyo, stendi zote, mikoa yote.

Nenda Dsm, Mwanza, Morogoro, Iringa, Dodoma, Tabora, Kagera, Mbeya, Arusha, Tanga, Mtwara, Kigoma, n.k, kote huko wana 'overcharge'.

Sasa kama watu wa mabasi wanaona nauli zilizopangwa ni ndogo, haziwapi faida, si bora LATRA ipitishe hizo hizo wanazolipishwa wananchi ili ifahamike moja.

Je, unataka kusema ripoti za haya zipo mezani kwa mh. Rais ila jinsi alivyo anajali watu wake kweli asichukue hatua.?!

Narudia ripoti hii ni kwa nia njema ya kujenga Taifa letu.

Ukweli huduma za umma zimezorota kiasi kikubwa, tusifiche tatizo na wananchi wengi wanaumia sana na hili.

Naomba kuhitimisha hapo kwa leo.

Karibuni wachangiaji kwa mengi zaidi.
Ni kweli

Mabasi sasa hivi yanatoza nauli zilezile kwa wote wanaoshuka njiani na wanao kwenda linakoishia basi, kwa mfano, mtu anaanzia safari Dar kwenda Singida, akipanda bus la Shinyanga atatozwa nauli ya Shinyanga badala ya Singida,

Ukipanda Shabiby Dodoma kwenda Morogoro unatozwa nauli ya Dar
Ukipanda Abood Morogoro unakwenda Chalinze unatozwa nauli ya Dar
Ukipanda ABC Mbeya kwenda Morogoro unatozwa nauli ya Dar
Ukipanda bus la kutoka Mwanza kwenda Dodoma kama unashuka Singida utatozwa nauli za Dodoma
 
Nimesoma ripoti yote hakuna la uongo hata moja

1. Kwenye hilo la NIDA mpaka 50 watu wanapokea.. Rushwa!
2. La mbagala hili lilishasemwa sasa! Mpaka namna tenda ilivyopatikana.. Rushwa!
3. La petrol kuna andiko limeichambua vizuri mno.. Rushwa!
4. La LATRA ni mulemule.. Rushwa..!

Ni rushwa ni rushwa ni rushwa mwanzo mwisho! Lakini si tunakumbuka angalizo la mkuu wa kaya kuhusu kula kwa urefu wa kamba? Dosari ilianzia hapo
Msimlishe rais wetu maneno, kuhusu kamba haina uhusiano na rushwa
 
Wa juu asipokuwa na sauti wa chini wataishia kulogana tu. Kikubwa ufahamu tu kwa sasa nchi ipo kwenye autopilot..tuendelee kupigia kelele sakata la bandari labda Mungu atasikia pambio zetu.
 
Ni mwaka wa 5 tangu nijiandikishe NIDA. Bado Sijapata Kitambulisho.
Nilidhani ni mimi peke yangu, kumbe wapo wengi!

Something will have to give, it cannot continue this way for ever.
 
KWA NINI UNAANDIKA UONGO, MAJUZI NIMEKWENDA OFISI ZA NIDA UKONGA, WAMEFANYIA PROCESS ZOTE FREE TENA KWA HARAKA WAMENIPA WIKI MBILI NIKACHUKUWE NAMBA, KWANZA ID ITAFUATA.

ACHENI UONGO NA UPOTOSHAJI.
Kwa hiyo hata huku majirani zangu mtaani wanachokisema kuhusu urasimu wa NIDA ni uongo?

Kuwa mzalendo usifiche uovu
 
Hawa jamaa wanaitwa SINOHYDRO ni Wala rushwa balaaa, Sasa viongozi wengi Sana wakifika wanapewa Chao wanaishia kupiga mkwara fake na kuondoka, mnakumbuka Yule DC Gondwe? Alienda akapiga mkwara Yule mbongo akawa anacheka TU?

Ujenzi wowote nchini ulio chini ya SINOHYDRO au STECOL (NDIO Huyo huyo SINOHYDRO) ni mibovu balaaa na hawajawahi kumaliza on time.

Wana kashfa za kuwanyanyasa wafanyakazi Sana na wale jamaa wa TAMICO hawana Cha kufanya.

Huu mradi wa BRT waliwahi kupata kashfa ya kutumia lami ambayo source yake ilikua nchi ambayo imewekewa vikwazo.

Na NDIO hawa hawa wamepewa SGR bila kutumia utaratibu wa manunuzi, yaani single source, Kuna siku Tanzania itaomboleza wallah.
KUna ule Mradi wa SGR unaoendelea kule Mwanza ambapo Mkandarasi Mchina anachakachua viwango vya ubora vya nguzo kwenye madaraja ya reli.

Usalama wa Taifa wwmejaa kedekede pale na hakuna linalofanyika
 
KUna ule Mradi wa SGR unaoendelea kule Mwanza ambapo Mkandarasi Mchina anachakachua viwango vya ubora vya nguzo kwenye madaraja ya reli.

Usalama wa Taifa wwmejaa kedekede pale na hakuna linalofanyika
Usalama wa Taifa wanatafuta vyeo CCM
 
KUna ule Mradi wa SGR unaoendelea kule Mwanza ambapo Mkandarasi Mchina anachakachua viwango vya ubora vya nguzo kwenye madaraja ya reli.

Usalama wa Taifa wwmejaa kedekede pale na hakuna linalofanyika
Wamekuwa wafanyakazi wa mkandarasi😃
 
Nimeipitia ripoti Yako ni kweli kabisa,mfano juzi niliamua kukata tiketi online bus Shabiby lakini nikaiona ipo ya saa saba na saa nane mchana semi luxury Kwa tsh 25000/= bus za asubuhi hawakuziweka.Ila nikaenda stand Mbezi Kwa Magufuli nikazikuta Shabiby nyingi hazijajaa na ticket bei ni tsh 30000/=
Bei juu na Latra haiwajibiki.Kwa ujumla vyombo vya serikali haviwajibiki na Wala hakuna kiongozi anaechukua hatua.
 
Ni usiku mnene. Naamua kuandika DOKEZO hili.

Kwa uchungu wa yanayoendelea katika nchi yangu.

Katika mada hii, nitaomba wachangiaji kujadili kwa uwazi kabisa, na kuongezea mifano mingine baada ya hii nitakayokuwa nimeiweka hapa.

Lengo ni Nia njema kabisa kurekebisha pale tulipokosea na kusaidia WaTz ambao wanakosa kufaidi matunda ya nchi yao.

Hapa chini ni jinsi ambavyo mambo ya ovyo yanafanywa wazi na TISS wala TAKUKURU hawafanyi kazi yao iliyotukuka.

1. NIDA na Utoaji wa NAMBA/Vitambulisho vya Taifa.

Hili jambo ni kubwa sana. Mimi nimelithibitisha. Na wote wanaofika kuhudumiwa katika ofisi zote za NIDA nchi nzima wanasema wazi.

Iko hivi, huwezi kufanikisha kupata namba ya NIDA ikiwa huna kiasi fulani cha fedha. Na huwezi kupata ile ID ikiwa huna kiasi kikubwa zaidi cha fedha.

Yani utaenda utafuata taratibu zote na kuwa na viambatanisho vyote, lakini huwezi kupata kimojawapo kati ya hivyo bila fedha. Kiufupi hadi mlinzi wa getini anajua hilo.

Baadhi ya Ofisi za NIDA DSM kupata namba ya NIDA inaanzia sh. 150,000/-. Kupata ID ni kuanzia sh. 500,000/-
Lakini kadri utakavyoongeza dau maana yake utawahishiwa zaidi mchakato wako.

Kwanza hakuna huduma pale, zaidi ukifika upangwe foleni na walinzi, ukiingia unakuta mtu anachat tu, hadi jioni uambiwe njoo tena kesho.

Haya yana muda mrefu yanafanywa wazi kabisa. Hatari hii ni kwamba sasa hata mgeni je, akiwa na milion zake mbili si anapewa zake ID kama MTz??

Mh. Rais wetu ni msikivu, je, ulishasikia amepewa ripoti hii akashindwa kuifanyia kazi?!

Nani wa kumpelekea ripoti kama sio TISS?


2. Mradi wa mwendokasi Mbagala

Huu mradi nendeni mchunguze, ni mbovu na umejengwa chini ya viwango vibaya mno.

Uchunguzi unaonesha baadhi ya miundombinu kuanza kuharibika hata kabla ya matumizi rasmi kuanza.
Wasichokijua ni kwamba hii miradi ya miundombinu ya barabara huwa na zaidi ya miaka 20 ya uhai kabla ya marekebisho.

Sasa ukifika pale ukakuta baadhi ya beacon zimeanguka, kumeguka, n.k, Unajiuliza shida ni nini? Bajeti ndogo ya ujenzi? Lakini hilo linakataa kwa sababu hizi fedha ni mkopo tumepata kutoka Benki ya Dunia (WB), hawawezi kutenga fedha chini ya inayotakiwa.!

Sasa vile vituo vya abiria ndio utacheka kabisa. Mabati ni chini ya viwango, hizo frame walizichomelea ni chini ya viwango, uchomeleaji wenyewe ni wa dizaini za fundi maiko.

Hata wakibisha, nawahakikishieni, barabara ya mwendokasi ya Posta KIMARA itadumu, na hii ya Mbagala itakuja kuharibika mapema kabla yake. Tuko hapa mtakuja kuthibitisha panapo uhai.

Sasa kwa hali hii, utasema Rais wetu alivyo msikivu, ana hii ripoti mezani kweli? Na hatujasikia akichukua hatua zozote?


3. UHABA wa Petroli sasa hivi nchini.

Hapa siandiki sana.

Fahamuni kwamba mafuta yapo. Si mlisikia hata Waziri anasema hakuna upungufu wa petrol. Si amesema mara nyingi tu!

Sasa Mimi na wewe tuulizane, Waziri anasema yapo, vituoni ukifika hakuna, yapo wapi? Eeh...

Jamaa wana mafuta, ila hawatoi kuyauza. Wanasubiri bei mpya za August, zipande usiku wa leo tarehe 31/07/2023 ndio wataanza kutoa mafuta.

Sasa "syndicate" ya namna hii, hapo unasema TISS wapo na wananchi, au wametuma ripoti Rais hajachukua hatua?!

Achaneni na mambo ya ooh Dola $ kuadimika, hiyo inaathiri uagizaji wa mzigo mpya. Sio stock iliyopo ambayo huagizwa miezi mitatu au zaidi nyuma.

4. Nauli za mabasi za LATRA.

Hivi mnajua mabasi yote ya mikoani katika stendi zote za mikoani wanachaji nauli zaidi ya zile zilizoidhinishwa na LATRA?!

USHAHIDI upo.

Hapa namaanisha hata LATRA na mapolisi wanalijua hilo. Je, ni fungu wanapewa au kuamua kuacha tu unyang'anyi huu uendelee?!

Nasisitiza iko hivyo, stendi zote, mikoa yote.

Nenda Dsm, Mwanza, Morogoro, Iringa, Dodoma, Tabora, Kagera, Mbeya, Arusha, Tanga, Mtwara, Kigoma, n.k, kote huko wana 'overcharge'.

Sasa kama watu wa mabasi wanaona nauli zilizopangwa ni ndogo, haziwapi faida, si bora LATRA ipitishe hizo hizo wanazolipishwa wananchi ili ifahamike moja.

Je, unataka kusema ripoti za haya zipo mezani kwa mh. Rais ila jinsi alivyo anajali watu wake kweli asichukue hatua.?!

Narudia ripoti hii ni kwa nia njema ya kujenga Taifa letu.

Ukweli huduma za umma zimezorota kiasi kikubwa, tusifiche tatizo na wananchi wengi wanaumia sana na hili.

Naomba kuhitimisha hapo kwa leo.

Karibuni wachangiaji kwa mengi zaidi.
Hili la nauli ni uongo wa mchana,mbona ushahidi haipo? Nimesafiri siku za karibuni mbona sijakutana na Hilo? Mbona watu wasilalamike?

Nida huko Kuna shida Toka kitambo sana Hadi Leo haijulikani shida ni ipi maana Kila Bunge Hawa wanasemwa ila hakuna kinachobadilika,labda Bunge litengeneze azimio.

Kuhusu Petrol ni kawaida kukiwa na uhaba lazima wafanyabiashara watumie fursa hiyo kutafuta faida kubwa,japo binafsi Mkoa wangu hiyo shida haipo Mikoa yote ya Nyanda za Juu Kusini mafuta yapo na bei ni Ile Ile sijui Kwa Vijijini.

Kuhusu Mwendokasi Wala hakuna shida uzuri mkataba uko clear ukijenga chini ya kiwango Kuna kipindi Cha Matazamio ikiharibika mkandarasi atarudia Kwa gharama yake.mfano wale waliopita Barabara ya Mpemba -Isongole na Mpanda-Tabora na Sumbawanga -Kasanga mtaona Kuna sections kibao wakandarasi wamefumua na wanarudia.

Bunge litoe azimio kuhusu nida Ili tujue shida Iko wapi
 
Mtag mheshimiwa Rais moja Kwa moja Ili asikie na kusoma mwenyewe, hizi habari za kupelekewa ni za kidwanzi

Yeye mwenyewe alishasema huwa anapita humu
Maeneo machache yakiwa na shida sio lazima Rais Kuna Waziri wa Ujenzi au PM wanaweza shughulikia.

Rais mpaka aje asome ni issue sana
 
KWA NINI UNAANDIKA UONGO, MAJUZI NIMEKWENDA OFISI ZA NIDA UKONGA, WAMEFANYIA PROCESS ZOTE FREE TENA KWA HARAKA WAMENIPA WIKI MBILI NIKACHUKUWE NAMBA, KWANZA ID ITAFUATA.

ACHENI UONGO NA UPOTOSHAJI.
Majinga kama wewe ndio hasara Kwa Taifa,Kwa hiyo Kila mtu ana ID ya NIDA nchii hii?Kila aliyeenda kwenye ofisi zao amepata hicho kitambulisho au namba?
 
Hawa jamaa wanaitwa SINOHYDRO ni Wala rushwa balaaa, Sasa viongozi wengi Sana wakifika wanapewa Chao wanaishia kupiga mkwara fake na kuondoka, mnakumbuka Yule DC Gondwe? Alienda akapiga mkwara Yule mbongo akawa anacheka TU?

Ujenzi wowote nchini ulio chini ya SINOHYDRO au STECOL (NDIO Huyo huyo SINOHYDRO) ni mibovu balaaa na hawajawahi kumaliza on time.

Wana kashfa za kuwanyanyasa wafanyakazi Sana na wale jamaa wa TAMICO hawana Cha kufanya.

Huu mradi wa BRT waliwahi kupata kashfa ya kutumia lami ambayo source yake ilikua nchi ambayo imewekewa vikwazo.

Na NDIO hawa hawa wamepewa SGR bila kutumia utaratibu wa manunuzi, yaani single source, Kuna siku Tanzania itaomboleza wallah.
Labda hii kampuni Ina mkono wa viongozi wa Serikali, Viongozi wa Mkoa wapige kelele zaidi ,Yale Yale ya Mayanga Construction.

Mbona kampuni zingine zinaogopa sana kurudia kazi?
 
Sio msikivu!!!!!!! Hakuna kitu asichojua, rushwa ni hatari, ukienda pale Latra Oysterday, pana mwavuli kuna wala rushwa officially wanangoja wateja.

Ukiingia ndani, kuna kijana pale anakwambia kabisa nenda hapo nje bla bla, ukigoma wanapiga simu hata kupa inspection copy wanakaza.

Hii nchi inanuka rushwa, mimi huwa sito rushwa 100%, mazila ninayokutana nayo ni hatari, anajua Mungu peke yake.
LATRA kuna uozo, ushahidi ninao mwingi tu.

Hongera kwa ushahidi huu.

Pole kwa madhila hayo
 
Labda hii kampuni Ina mkono wa viongozi wa Serikali, Viongozi wa Mkoa wapige kelele zaidi ,Yale Yale ya Mayanga Construction.

Mbona kampuni zingine zinaogopa sana kurudia kazi?
A very serious problem but no one cares
 
Back
Top Bottom