TAKUKURU Shinyanga inamshikilia Joseph Jonas Tasia kwa kukutwa na doti mia sita (600) za vitenge vyenye nembo ya Chama Cha Mapinduzi na vya kawaida

Mwaka uchaguzi nina jamaa yangu dereva wa bodaboda ana bendera zote za CCM,CUF na CHADEMA yy hana chama anaangalia hela kote yupo hela yako tu.
 
Reactions: Auz
sasa takukuru hawataki bibi zetu wale matunda ya uchumi wa kati
 
Doti 600 za Khanga na Vitenge vya CCM vyadakwa na TAKUKURU vikihisiwa kutaka kutumika kuwahonga wapiga kura kuelekea Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2020.

 
Kosa liko wapi apo,je kama anataka kuuza!?[emoji1787]au kuvaa na familia yake?au kwa sasa ni nyara za serikali hizo mbogamboga?!
 
Usanii tu uchunguzi wa takokuru wa baiskeli na pikipiki za Hamisi madigirii kule Igunga umeishia wapi!?

Doti 600 za Khanga na Vitenge vya CCM vyadakwa na TAKUKURU vikihisiwa kutaka kutumika kuwahonga wapiga kura kuelekea Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2020.

 
Takukuru wanaishi dunia gani? Kuna wanaofanya kampeni bila kujitangaza kwenye mavazi? Inategemea tu utamaduni wa eneo husika. Mfano Marekani, kama si kofia ni t-shirts, wao hawavai vitenge. Sasa Tz wajinadi vipi?
 
Sasa hapo rushwa iko wapi? Yaani hamna kesi kabisa. Sema kutishana kunamfanya asijiamini.
 
Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru) Mkoa wa Shinyanga, imemkamata mfanyabiashara wa magari ya teksi, Joseph Tasia, akiwa na doti 600 za vitenge vyenye nembo ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) nyumbani kwake na kushindwa kutoa maelezo yanayojitosheleza.

Nipashe

TAKUKURU mkimaliza huko kote Mzukulu ninawaombeni sana ikiwezekana mkite Kambi Jimbo Tajiri la Kawe kwani kuna Makubwa yanaendelea.
 

Attachments

  • 2448897_facebook_106462946_1652883354871216_2490927066034797977_n.mp4
    1.8 MB
Mzigo wa Rushwa huo. CCM bila rushwa HAIWEZEKANI.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…