TAKUKURU yamrejeshea mstaafu mamilioni aliyodhulumiwa

TAKUKURU yamrejeshea mstaafu mamilioni aliyodhulumiwa

Nyendo

JF-Expert Member
Joined
Jun 4, 2017
Posts
1,336
Reaction score
4,731
Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) mkoa wa Dodoma imemrejeshea Bi. Frida Nahamani (62) mkazi wa Michese Jijini Dodoma kiasi cha shilingi milioni kumi (10,000,000) alizodhulumiwa na Bwana Maswe Wambura Mgaya ambaye ni mmiliki wa Taasisi ya SWAHILI TRUST MICROFINANCE ya Jijini Dodoma inayofanya kazi ya ukopeshaji fedha.

Uchunguzi wa TAKUKURU ulianza baada ya kupokea malalamiko kutoka kwa Bi. Nahamani ambaye ni muuguzi mstaafu ambapo umeonesha kati ya Julai na Disemba 2018 alikopa fedha kiasi cha sh. 15,000,000/= na akakabidhi kadi yake ya benki kwa Taasisi hiyo ili warejeshe pesa yao mara baada ya mafao yake kutoka. Hata hivyo mnamo tarehe 31/1/2020 aliporudishiwa kadi yake alikuta hakuna kiasi chochote kwenye akaunti yake wakati alilipwa zaidi ya milioni arobaini na sita kwenye mafao yake

TAKUKURU imejirizisha kabisa kuwa Taasisi ya SWAHILI TRUST MICROFINANCE ilizidisha kiasi cha shilingi milioni kumi ambacho ilizidisha kwenye kukata marejesho na hivyo imelazimika kuzirudisha baada ya TAKUKURU kuingilia kati na kuwataka kufanya hivyo
 

Attachments

Hao Maswe walishawahi kumkopesha mama mmoja hivi, hehehehehe, alinipigia simu anaomba akawarejeshee. Ni wamembana hapumui.

Mwingine kakopa 5M marejesho 8M within 3 months. Hapo ndo wanaanzia sasa kupiga pesa.
Ukizidisha pesa inafika hadi 40M.
 
Alikopa Million15.
Mafao yake ni million 46.
Amerudishiwa million 10.

Ikwesheni:- 46-(15+10)=
= 46-25=21
Kwa hiyo tunaweza kusema alikopa million 15 kwa riba ya million 21? Hapa hata sijaelewa kabisa. Na kama ni hivyo watoto wa huyu mama kama wapo Mungu awasaidie.
 
Alikopa milioni 15 na mafao yake aliyolipwa yalikuwa zaidi ya milioni 40, na baada ya kurudishiwa kasi hakukuta hela yeyote, na PCCB ilipochunguza ikakuta alikatatwa ziada ya milioni 10, mbona hesabu hazibalance hapa
 
Alikopa milioni 15 na mafao yake aliyolipwa yalikuwa zaidi ya milioni 40, na baada ya kurudishiwa kasi hakukuta hela yeyote, na PCCB ilipochunguza ikakuta alikatatwa ziada ya milioni 10, mbona hesabu hazibalance hapa
aibalance vip unajua hapo inawezekana riba ilikua kubwa
 
Hivi kwani huwa wanalizimishwa kwenda kukopa?


Tunaishi ulimwengu wa kibepari, waache kuwa wanatetea watu wanaoingia makubaliano wenyewe.
 
aibalance vip unajua hapo inawezekana riba ilikua kubwa
Tufanye sawa riba ilikuwa kubwa, amelipwa zaidi ya milioni 40 (may be 45m) ukitoa na mkopo 15m jumlisha na walizorejesha PCCB 10m inabaki 20m. Ina maana hapa deni lake la milioni 15 linakuwa na riba ya 20m? ( yaani jumla ya mkopo na riba ni 35M, maana mafao 45 na haikukutwa kwenye akaunti ila pccb wamerejesha 10M, 45 toa 10 inabki 35 ndo imelipa mkopo? )
 
Tufanye sawa riba ilikuwa kubwa, amelipwa zaidi ya milioni 40 (may be 45m) ukitoa na mkopo 15m jumlisha na walizorejesha PCCB 10m inabaki 20m. Ina maana hapa deni lake la milioni 15 linakuwa na riba ya 20m? ( yaani jumla ya mkopo na riba ni 35M, maana mafao 45 na haikukutwa kwenye akaunti ila pccb wamerejesha 10M, 45 toa 10 inabki 35 ndo imelipa mkopo? )
Hapa uchunguzi ufanyike itakuwa kadhulumiwa 15 izae riba 20 million uyo nesi alikuwa sio msomi . Na huu ndo ubaya wa kufoji vyeti vya shule ya msingi na sekondary . Mana inaoneka hajui hesabu za riba katika benki.

Ivi humu Kuna jukwaa la hesabu kweli

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ina maana mkopo wa 15M unazaa 15M nyingine?maana kapewa 10 tu kwenye 40M yake.
 
  • Thanks
Reactions: amu
Haya ndio matatizo ya mfuko wa pension (PSSSF) kuchelewesha mafao ya wastaafu hadi kufikia kudhulumiwa fedha.

Bora awamu ile mifuko ilikuwa mingi na ushindani wa kibiashara na utoaji huduma uliongezeka licha ya kuwa yote ilikuwa chini ya serikali.
 
Back
Top Bottom