Takwimu za MOI zinaonesha Lema yupo sawa kuhusu "laana" ya bodaboda

Takwimu za MOI zinaonesha Lema yupo sawa kuhusu "laana" ya bodaboda

fazili

JF-Expert Member
Joined
Jun 10, 2011
Posts
16,427
Reaction score
22,418
Godbless Lema hakueleweka na watu kwa kauli yake kuwa kazi ya bodaboda ni laana. Lakini ukiangalia takwimu kutoka taasisi ya mifupa Muhimbili utagundua Lema ana point. Hapo ni Muhimbili tu, nchi nzima ni zaidi ya vijana 1500 huumizwa vibaya kwa mwezi sawa na zaidi ya vijana 15,000 kwa mwaka! Hii ni laana!

TAASISI ya Tiba ya Mifupa Muhimbili( MOI), imesema kwa mwezi inapokea wagonjwa 600 walioumia vichwa kutokana na ajali za Pikipiki.

Akizungumza na Waandishi wa Habari jijini Dar es Salaam jana, Ofisa Habari wa taasisi hiyo, Patrick Mvungi, alisema ajali hizo zinasababishwa na madereva pamoja na abiria kushindwa kuvaa kofia ngumu pindi wanapokuwa barabarani.

Mvungi, alisema taasisi hiyo ikiwa katika kipindi cha mpito cha mageuzi ya utoaji huduma za afya nchini, imefanikiwa kwa asilimia 95 kutoa huduma muhimu za tiba na upasuaji kwa wagonjwa na hivyo kupunguza vifo na rufaa za kusafirisha wagonjwa nje ya nchi.

Alisema zaidi ya wagonjwa 4,500 wa mifupa wamepatiwa huduma kwa kutumia utaalamu wa kufanyiwa upasuaji na kuwekewa kifaa maalum (Sign Nail), kwa wagonjwa waliovunjika mifupa kinachowasaidia kupona mapema na kurudi katika hali zao za kawaida.

“Kwa upande wa Upasuaji Mkubwa wa Nyonga (Total Hip Replacement), zaidi ya wagonjwa 1,256 walipasuliwa salama na wamepona, huku zaidi ya wagonjwa 703 wakifanyiwa upasuaji mkubwa wa kubadilisha viungo vya goti vilivyoharibika (Total Knee Replacement), kwa kuweka vifaa maalum vya bandia (Artificial Implants), ambapo zaidi ya 95 ya wagonjwa wameweza kutembea na kurudi katika hali zao za kawaida,” alisema.

Mvungi, alisema taasisi hiyo pia imefanikiwa kutoa matibabu kwa wagonjwa ya ubongo (Brain Surger diseases), waliokuwa wakihitaji upasuaji kwa zaidi ya asilimia 80.

Na Janeth Jovin
 
Sema namna Lema anavoiweka itamgharim sana
 
Hapo wa kulaumiwa ni serikali inayoshindwa hata kuwaongoza madereva
Mkuu wa polisi kama anashindwa wajibu wake aachie ngazi

Kama mnaona vijana wanaishia MOI hilo sio kosa lao bali ni sheria mbovu
Na hongo zilizokithiri
Wengi wanajifundisha usiku na asubuhi anapewa license na kuingia barabarani

Wa kulaumiwa ni wahusika wanaotoa leseni
Police wanawamaliza kwa hela ya kubrashia viatu
 
Sasa hizo ni takwimu za MOI kwamba inapokea wagonjwa wa mifupa 600 kila mwezi.

Ili tujadili hili swala kwa kina, tujue kama ni janga au sio janga, tunasubiri na takwimu za kila mwezi za;

1) Wagonjwa wanaopata "PNEUMONIA (Nimonia)" kwasababu ya baridi na mvua kuathiri mapafu kutokana na kuendesha pikipiki.

2) Wagonjwa wa akili kutokana na athari za kuendesha pikipiki kwenye jua kali, baridi kali na mvua. Kisayansi uendeshaji wa pikipiki kwenye mchanganyiko wa hali ya hewa huathiri akili.

3) Wagonjwa wa mwili kudhoofika kutokana na stress za uendeshaji pikipiki na kukoswa na ajali barabarani (Kuna watu wanakoswa na ajali mpaka anachanganyikiwa).

4) Madereva bodaboda wanaokufa/kuuliwa kwasababu ya kuibiwa hizo pikipiki.

5) Wizi unatokoea wa bodaboda kuibiwa.

N.K
 
600 kwa mwezi!!! duh Tumuombe sana Mungu atuepushe na ajali pindi tunapotumia vyombo hivyo.
 
6000*12 ni 7200, kwa tz nzima inaweza kufika 50,000
 
Back
Top Bottom