Taliban yatoa onyo kali kwa Marekani, Uingereza kutoendelea kukaa Afghanistan baada ya Agosti 31

Taliban yatoa onyo kali kwa Marekani, Uingereza kutoendelea kukaa Afghanistan baada ya Agosti 31

Sam Gidori

Senior Member
Joined
Sep 7, 2020
Posts
165
Reaction score
417
Wanagambo wa Taliban wametishia kuyachukulia hatua mataifa ya Marekani na Uingereza ikiwa watashindwa kuondoa wanajeshi wao kufikia Agosti 31 mwaka huu.

Kauli ya Taliban inakuja siku moja baada ya Rais Joe Biden kusema kuwa kuna uwezekano wa kuongeza muda wa wanajeshi wao kuendelea kukaa nchini Afghanistan, wakati Waziri wa Ulinzi wa Uingereza, Ben Wallace akisema shughuli ya kuwaondoa wanajeshi wa Uingereza inaweza kukamilika ndani ya saa, sio wiki.

Msemaji wa Taliban, Dkt. Suhail Shaheen amesema kundi hilo halitakubaliana na hatua ya mataifa hayo kuongeza muda wa wanajeshi wao kukaa nchini humo, na kuahidi kuchukua hatua kali ikiwa wanajeshi wataendelea kubaki nchini humo.

Awali, Rais Biden alionya kuwa shughuli ya kuwatoa Wamarekani wote nchini Afghanistan inaweza kuwa ndefu na ya kuumiza.

“Haitawezekana kuwatoa maelfu ya watu nchini Afghanistan bila kushuhudia maumivu na kuwapoteza watu na picha tunazoziona kwenye televisheni,” Rais Biden alisema, akiongeza kuwa zaidi ya watu 11,000 wameondolewa nchini Afghanistan ndani ya saa 36, na kufanya jumla ya watu walioondolewa nchini humo kufikia 33,000 siku ya Jumapili.

Zaidi ya watu 20,000 wanasubiri kutolewa kutoka uwanja wa ndege wa Kabul. Uingereza inataka kuongeza idadi ya watu wanaotolewa nchini Afghanistan kufikia 12,000, lakini Waziri Mkuu wa Uingereza, Borris Johnson amesema kufanikiwa kwa hatua hiyo kunategemea wanajeshi wa Marekani kuendelea kudhibiti Uwanja wa Ndege.

Zaidi ya watu 20 wameripotiwa kufariki nje ya Uwanja wa Ndege wa Kabul, wengine wakitajwa kufariki kwa kukanyagana, kwa mujibu wa Shirika la Habari la Reuters. Waziri Mkuu wa Uingereza anatarajiwa kufanya mkutano na Rais Biden hapo kesho kumshawishi kuendelea kuwabakisha wanajeshi wa Marekani nchini humo. Onyo la Taliban ni pigo kubwa kwa mataifa hayo ambayo yanajitahidi kupata muda zaidi kufanikisha kuwaondoa wananchi wao nchini humo.

Taliban, kwa upande wao, wamesema wananchi wa Afghanistan hawakimbii nchi yao kutokana na wasiwasi, bali kutokana na sababu za kiuchumi.

Msemaji wa Taliban, Dkt. Shaheen ameongeza kuwa taarifa zinazosambaa za kufungwa kwa shule za wasichana si za kweli, akisisitiza kuwa wanawake nchini humo wana haki sawa kama hali ilivyo kwenye nchi za Magharibi, “lakini tu wakiwa na hijabu.”

Chanzo: Daily Mail

1629722065130.png

Wanajeshi wa Uturuki wakitoa maji kwa Waafghanistan wanaosubiri kuondolewa kutoka Uwanja wa Ndege wa Hamid Karzai mjini Kabul [Picha: AA]
 
Taalibani ni freedom fightets sisawa kusema wameachiwa nchi.

They fighted from begining to the end hadi Wavamizi wakasarenda.
The power is on the hand of Taliban, hawajamaa hawajali kurudi milimani na kupambana tena
Inategemea na unaangalia katika angle ipi.
 
Vita ndio imeanza rasmi, tutaanza kuona warlords kila kona ya Afghanistan loaded with cash and weapons from US, China, Russia etc, Marekani kamwachia mzigo Taleban apambane nao, US kaondoka jina tuu weapons supply and cash vitaendelea kumiminika kwa wingi....kitaeleweka tuu
 
Biden huyo anajaribu kuaminisha watu kwamba haraka zake ni kwasababu ya Taleban. Ukweli ni kwamba yule Babu kachemka
 
Mimi najiuliza tu hao wazungu wengi namna hiyo walifuata nini huko Afghanistan kama sio wahalifu?

Taliban inatakiwa iwakamate iwape adhabu kali.

Biashara ya madawa ya kulevya inalipa sana na wao wako huko miaka wakifanya biashara hiyo

Angalia wanavyolinda mashamba halafu wanaidanganya dunia na kusema wanaondoa Ugaidi

Duniani nchi nyingi wanaongeza pato Lao kwa dhulma na ubabe bila kuiba uchumi chali

IMG_2131.jpg

IMG_2129.jpg

IMG_2127.jpg
 
Sasa inatakiwa serikali ya Taleban iwashughulikie na sio kuwapa upenyo wa kutoroka

Tatizo wanajuana vizuri na hii baishara ilikuwa na baraka zote pande zote ingawa wengine (waafghani) walikuwa hawapendi ila ndio zao lao kubwa linapowaingizia kipato na hao wazungu wakagawana mashamba
UK akiwa na sehemu kubwa inayolimwa sana huko Helmand
 
Rais wa marekani Joe Biden ni kituko cha karne. Ameishushia marekani hadhi kupita maelezo. Cowards and loosers of the highest order.
 
Vita ndio imeanza rasmi, tutaanza kuona warlords kila kona ya Afghanistan loaded with cash and weapons from US, China, Russia etc, Marekani kamwachia mzigo Taleban apambane nao, US kaondoka jina tuu weapons supply and cash vitaendelea kumiminika kwa wingi....kitaeleweka tuu
Nadhani hujuwi historia ya TAALIBANI. Hawa ndio kiboko wa Warloard.
Talibani ilianzishwa ili kuwasambaratisha Warload baada ya vita na warusi.

Talibani ndio walioleta AMANI Afgani hadi maharamia na wavamizi walipowapenduwa., ila waependuwa na hasara wameipata
 
Back
Top Bottom