Taliban yatoa onyo kali kwa Marekani, Uingereza kutoendelea kukaa Afghanistan baada ya Agosti 31

Taliban yatoa onyo kali kwa Marekani, Uingereza kutoendelea kukaa Afghanistan baada ya Agosti 31

Nadhani hujuwi historia ya TAALIBANI. Hawa ndio kiboko wa Warloard.
Talibani ilianzishwa ili kuwasambaratisha Warload baada ya vita na warusi.

Talibani ndio walioleta AMANI Afgani hadi maharamia na wavamizi walipowapenduwa., ila waependuwa na hasara wameipata
Warlords njaa walikuwa hao, wanaokuja wana cash na weapon kuliko Talebans, i hope wote wapate akili wapatane tuu, unafikiri lile jeshi la serikali na weapons zote zimeyeyuka tuu
 
True. Statistic inaonesha biashara ya MUKHAADARAATI iliongezeka maradufu baada ya talibani kuvamiwa na Marikani

Na wabebaji wakubwa ni USA na UK
Yaani wanajua mpaka street value ya madawa yakiwa London
Bei za market serikali inajua kwa sababu wao ndio wanaendesha hii biashara
 
Nani humu ana support mtoto wake akikamatwa kazini apigwe mawe mpaka kufa au kukatwa shingo?? ni swali tuu
 
Mimi najiuliza tu hao wazungu wengi namna hiyo walifuata nini huko Afghanistan kama sio wahalifu?
Serikali ya Taliban inatakiwa iwakamate iwape adhabu kali.
Wala hao siyo Wazungu, hao ni wa Afghanistan wenye uraia wa Marekani (Uraia pacha)
 
Iran ajiandae,maana Taliban na Iran ni maji na mafuta.
iran ndio muendesha game hapo ndio hivi ulidhani iran ilifurahishwa na uwepo wa markeni hapo hiyo ni michezo ya iran. Sasa bado huko iraq lazima marekani asepe mama yaan siku hii unaishabikia talban ha ha ha kweli umeikatia tamaa marekani
 
Chinja kabisa hao wazungu ni magaidi walikuja kuchafua nchi ya afgjanistan
Hongera jeshi la afgjanistan kuwashinda hao wazungu pumzi imekata baada ya miaka 20 tu na kila wakipima wanaona malengo hayafikiwi
Hana jeuri hiyo kwani hata yeye miaka 20, anaishi kama ndege, unadhani alipenda?na zamu hii hawezi kuwa na ukatili kama ule, kwani kama ni somo naye amelipata!!ajaribu kushambulia vikosi hivyo uone nini kinaweza tokea?!!USA anawez badirika akaona kama ni hasara , tulishapata sana, potelea poteee!!!
 
Hana jeuri hiyo kwani hata yeye miaka 20, anaishi kama ndege, unadhani alipenda?na zamu hii hawezi kuwa na ukatili kama ule, kwani kama ni somo naye amelipata!!ajaribu kushambulia vikosi hivyo uone nini kinaweza tokea?!!USA anawez badirika akaona kama ni hasara , tulishapata sana, potelea poteee!!!
Wanaweza fanya kusudi tu kutokamilisha hilo zoezi Hili waone nini kitatokea
 
Hana jeuri hiyo kwani hata yeye miaka 20, anaishi kama ndege, unadhani alipenda?na zamu hii hawezi kuwa na ukatili kama ule, kwani kama ni somo naye amelipata!!ajaribu kushambulia vikosi hivyo uone nini kinaweza tokea?!!USA anawez badirika akaona kama ni hasara , tulishapata sana, potelea poteee!!!
Vita ya saa hii ni uchumi,
Utemi umepitwa na wakati,
Ni kweli us ana nguvu nyingi
Ila akiyumba kiuchumi kuna wanaume watatake over na hapo ndio utakuwa mwanzo wa mwisho wao,
Na hilo wanalijua
Sio wajinga kuondoka pale,
Kiukweli wameshindwa,
Muungwana akivuliwa nguo huchutama
 
Iran ajiandae,maana Taliban na Iran ni maji na mafuta.
Iran ndiye aliyewasapot wataleban hadi wakashinda hiyo vita pia wamefurahishwa marekani kuondoka Afghanstan na jana wametangaza kufungua njia upya za kuanza kuuza mafuta upya afghanistan
 
Biden huyo anajaribu kuaminisha watu kwamba haraka zake ni kwasababu ya Taleban. Ukweli ni kwamba yule Babu kachemka
Unaelewa nini wewe kula ugali wako na miwa ukalale waache wenye dunia yao wacheze na akili za watu wanavyotaka.... Jiulize swali Kwann America alivyokuwa Afghanistan taleban hawakuchukua nchi na America amekaa Afghanistan miaka 20 why American ametangaza kuondoka na ameanza kuahamisha majeshi yake ndo taleban inafufuka inachukua nchi kwa lugha nyingine taleban inamhofia America hata hilo tu hulijui au Kahawa imekulevya?
 
Unaelewa nini wewe kula ugali wako na miwa ukalale waache wenye dunia yao wacheze na akili za watu wanavyotaka.... Jiulize swali Kwann America alivyokuwa Afghanistan taleban hawakuchukua nchi na America amekaa Afghanistan miaka 20 why American ametangaza kuondoka na ameanza kuahamisha majeshi yake ndo taleban inafufuka inachukua nchi kwa lugha nyingine taleban inamhofia America hata hilo tu hulijui au Kahawa imekulevya?
Sawa mama Khadija, ila ukweli ni kwamba Ushawishi wa Ulaya na Marekani umepotea Duniani. Wamedhalilika wamevuliwa nguo mchana
 
Unaelewa nini wewe kula ugali wako na miwa ukalale waache wenye dunia yao wacheze na akili za watu wanavyotaka.... Jiulize swali Kwann America alivyokuwa Afghanistan taleban hawakuchukua nchi na America amekaa Afghanistan miaka 20 why American ametangaza kuondoka na ameanza kuahamisha majeshi yake ndo taleban inafufuka inachukua nchi kwa lugha nyingine taleban inamhofia America hata hilo tu hulijui au Kahawa imekulevya?
Hapana mimi natofautiana na wewe kidogo
Us hawakuichukua Afghanistan ili waje wairudishe kwa wenyewe,
No hakuna mwizi anaiba ili amrudishie mwenyewe alichoiba, lengo la us ni kuitawala au kuweka vibaraka wao, sasa kwa 20 yrs kichapo walichopata cha reja reja bila ya lengo lao kufikiwa imebidi waondoke tu,
Wanachinjwa sana ila wamemiliki media kwahiyo kupata habari ni shida sana
Lakini wao ni welevu sana kukiko kuendelea kufa ni bora wakajipange na pengine wanaweza kurudi tena kivingine
Ila kwa sasa pumzi imekata
 
Unaelewa nini wewe kula ugali wako na miwa ukalale waache wenye dunia yao wacheze na akili za watu wanavyotaka.... Jiulize swali Kwann America alivyokuwa Afghanistan taleban hawakuchukua nchi na America amekaa Afghanistan miaka 20 why American ametangaza kuondoka na ameanza kuahamisha majeshi yake ndo taleban inafufuka inachukua nchi kwa lugha nyingine taleban inamhofia America hata hilo tu hulijui au Kahawa imekulevya?
Amerika ametumia miaka 20 kupigana na Taliban, zaidi ya $2trillion kupigana na Taliban, wanajeshi wake kufa kupigana na Taliban na kuwa-replace Taliban kwa Taliban (hao hao).

Ndiyo kafanya nini sasa?
 
Wanagambo wa Taliban wametishia kuyachukulia hatua mataifa ya Marekani na Uingereza ikiwa watashindwa kuondoa wanajeshi wao kufikia Agosti 31 mwaka huu.

Kauli ya Taliban inakuja siku moja baada ya Rais Joe Biden kusema kuwa kuna uwezekano wa kuongeza muda wa wanajeshi wao kuendelea kukaa nchini Afghanistan, wakati Waziri wa Ulinzi wa Uingereza, Ben Wallace akisema shughuli ya kuwaondoa wanajeshi wa Uingereza inaweza kukamilika ndani ya saa, sio wiki.

Msemaji wa Taliban, Dkt. Suhail Shaheen amesema kundi hilo halitakubaliana na hatua ya mataifa hayo kuongeza muda wa wanajeshi wao kukaa nchini humo, na kuahidi kuchukua hatua kali ikiwa wanajeshi wataendelea kubaki nchini humo.

Awali, Rais Biden alionya kuwa shughuli ya kuwatoa Wamarekani wote nchini Afghanistan inaweza kuwa ndefu na ya kuumiza.

“Haitawezekana kuwatoa maelfu ya watu nchini Afghanistan bila kushuhudia maumivu na kuwapoteza watu na picha tunazoziona kwenye televisheni,” Rais Biden alisema, akiongeza kuwa zaidi ya watu 11,000 wameondolewa nchini Afghanistan ndani ya saa 36, na kufanya jumla ya watu walioondolewa nchini humo kufikia 33,000 siku ya Jumapili.

Zaidi ya watu 20,000 wanasubiri kutolewa kutoka uwanja wa ndege wa Kabul. Uingereza inataka kuongeza idadi ya watu wanaotolewa nchini Afghanistan kufikia 12,000, lakini Waziri Mkuu wa Uingereza, Borris Johnson amesema kufanikiwa kwa hatua hiyo kunategemea wanajeshi wa Marekani kuendelea kudhibiti Uwanja wa Ndege.

Zaidi ya watu 20 wameripotiwa kufariki nje ya Uwanja wa Ndege wa Kabul, wengine wakitajwa kufariki kwa kukanyagana, kwa mujibu wa Shirika la Habari la Reuters. Waziri Mkuu wa Uingereza anatarajiwa kufanya mkutano na Rais Biden hapo kesho kumshawishi kuendelea kuwabakisha wanajeshi wa Marekani nchini humo. Onyo la Taliban ni pigo kubwa kwa mataifa hayo ambayo yanajitahidi kupata muda zaidi kufanikisha kuwaondoa wananchi wao nchini humo.

Taliban, kwa upande wao, wamesema wananchi wa Afghanistan hawakimbii nchi yao kutokana na wasiwasi, bali kutokana na sababu za kiuchumi.

Msemaji wa Taliban, Dkt. Shaheen ameongeza kuwa taarifa zinazosambaa za kufungwa kwa shule za wasichana si za kweli, akisisitiza kuwa wanawake nchini humo wana haki sawa kama hali ilivyo kwenye nchi za Magharibi, “lakini tu wakiwa na hijabu.”

Chanzo: Daily Mail

View attachment 1904873
Wanajeshi wa Uturuki wakitoa maji kwa Waafghanistan wanaosubiri kuondolewa kutoka Uwanja wa Ndege wa Hamid Karzai mjini Kabul [Picha: AA]

Mabeberu ni mapumbafu kabissa. Yanawazushia watalibani kila ki2, kanakwamba wao ni wasafi kumbe!!!!!
 
Mungu wa ajabu sana yani kila nchi imepewa baraka zake kwenye maendeleo

Umeona eeh
Kweli kabisa
Halafu wanawafuata kwenye baraka zao
Kama waarabu na mafuta na sisi kwa madini yetu ila ndio hivyo tena
 
Back
Top Bottom