TAMISEMI fuatilieni Wakurugenzi wa Halmashauri zote kuhusu ajira mpya za Waalimu kuna urasimu mkubwa

TAMISEMI fuatilieni Wakurugenzi wa Halmashauri zote kuhusu ajira mpya za Waalimu kuna urasimu mkubwa

Basi una mshahara wa December na wasipokulipa maana yake utawadai haina shida.

Possibly kilichosababisha pesa za kujikimu zichelewe basi ni hilo swala la uhakiki kutoka necta, kuweni na subra.
Kuna aliyedai salary arrear akalipwa kweli??
 
Bila kukomaa hiyo hela ya kujikimu hamtaipata na mbaya zaidi mmeingia shule zimefungwa mitihani mmeshasahihisha na kupanga matokeo sasa hakuna effect kwa idara ya elimu hata mkigoma.
Mimi nakumbuka tulipata post wakati masomo yanaendelea na kukuta hali ni mbaya hakuna waalim wa sayansi. Yaaan tukakinukusha tulipewa hela fasta za kujikimu halmashauri yetu ila mshahara ulichelewa mwezi mmoja.
Ila tulisain 716,000 mshahara wa degree ila awamu hiibwa degree wamesaini 756,000.
Sijaelewa hapo inakuwaje mbona magepu hayaaa
Ilikuwa mwaka gani mkuu?
 
LKN mdogo wangu, Umeweza kuishi Mtaani bila Ajira tangu 2016 au 2017 unaona shida gani kuvumilia Desemba ipite ili Januari ufurahie Maisha mpaka utakapotimiza miaka 60. Tuache kulalamika kila Wakati mnachafua Taswirra nzuri ya Kada ya Ualimu.

Walikuwa nyumbani, hawakulipa kodi wala hawakulipia chakula. Mnategemea waishije kwa kipindi hicho mnachohakiki vyeti vyao?
 
In short hizi ajira walikurupuka kwa sababu za kisiasa kutafuta kura, sasa ndio mmekutana na uhalisia wa mambo. Poleni sana.
 
Basi una mshahara wa December na wasipokulipa maana yake utawadai haina shida.

Possibly kilichosababisha pesa za kujikimu zichelewe basi ni hilo swala la uhakiki kutoka necta, kuweni na subra.
Mkuu uko vizuri sana kwa ushauri na ufariji. Hongera kwa huo moyo
 
Mimi mmojawao. Kinachoudhi ni kutokuwa na accountability kuhusu hili suala la mishahara. Usishangae mwezi huu ukapita free tena
 
Back
Top Bottom