TAMISEMI kama mmeshindwa kuandaa mifumo mizuri ya watu kuomba ajira ni bora mkarudisha zama za posta. Mfumo umekuwa usumbufu

Yap mfumo unazengua lakini katika hyo changamoto ya kuedit taarifa ipo unachotakiwa kufanya ni kama unatumia simu inatakiwa uiseti kwenye mfumo wa desktop kwa kubonyeza vitufe vitatu vya kulia kwenye browser unayotumia na utaweza kufanya editing
Kukosea kujaza unapoomba kazi ni uzembe wa kupindukia issue nzito kama hiyo inabidi kutuliza kichwa

Tatizo unakuta kijana anawaza huku ana head phone masikioni akiburudika na mziki!!

Aende internet cafe kujaza mbona ziko kibao na komputa kibao
 
Digrii ya bachelor of education administration sio degree ya kufundisha ni ya uongozi katika shule na taasisi za elimu sio ya kufundisha darasani
 
Watuma maombi mjiandae tu kisaikolojia! Maana mtapigwa na kitu kizito kwa mara nyingine tena.

Haiwezekani watu 100 muombe nafasi ya kazi kwenye shule moja yenye uhitaji wa mwalimu mmoja tu wa somo husika! Hapa maana yake watu 99 hawana chenu!


Kama vipi vijana ingieni tu mtaani mpambane. Maana hakuna namna nyingine. Hii serikali yenu inawachezea tu shere. Mko zaidi ya laki 1! Halafu wanaajiriwa watu 9000 tu!

Hapo hapo kuna watu huko Tamisemi wana ndugu zao, wake zao, waume zao, watoto wao, vimada wao, wanaotaka kuajiriwa! Bado waliotoa rushwa, nk!
 
Kujaza kuomba kazi ni kama kufanya mtihani ukishakusanya hakuna kusema nipe ni edit!!

Uki send au move next basi ushakusanya hivyo no room for editing

Huko vyuoni mlikosoma hakufundishwa hayo?

Unakosea kosea kujaza application tu ukifika kazini kama daktari si utasahau kushona mgonjwa uliyemfanyia operation
 
Tunapolaumu mfumo tujipime wenyewe tunajua kuutumia huo mfumo? Mfumo was ajira ni mzuri na ni rafiki Kwa mtumiaji mwenye uelewa.
Changamoto kizazi Cha Facebook Kuna shida ya kuutumia mifumo.
Mfumo huu unaweza ku edit au kuondoa na kuweka upya taarifa zako changamoto Iko wapi?
 
Serikali isimamie mchakato wa kuwapangia mikoa/wilaya/vituo vya kazi waombaji wapya kwa weledi na bila upendeleo.Katika kikao Cha Bunge kinachoendelea,Kuna baadhi ya wabunge wamekiri kuwa, wapiga kura wao wanakwenda kuwalilia wawabebe vijana wao
Ushauri
1).Serikali Ni vema ikatoa vigezo vya kufanya uchaguzi wa waajiriwa wapi
2). Kamati ya upangaji wa watumishi wapya iongozwe na vigezo hivyo
 
Jinsi unavyoona ugumu wa mfumo kufunguka ndio ugumu huo huo utakao upata utakapofanikiwa kupchaguliwa kufanya kazi tamisemi
 
Kutumia dakika 45 hiyo indicator mfumo unashida
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…