Elections 2010 Tamko la Dr.Slaa

Elections 2010 Tamko la Dr.Slaa

Nimefurahi kusikia kauli ya Rais wa Watanzania. Lakini Chadema na Dr. Slaa watoe maelezo haraka na mapema kwa Watnzania ili kukabili hayo matatizo yaliyohamia kwenye kura za urais. Wapiga kura wako Dr Slaa wanahitaji kuona kura zote walizokupigia zinahesabiwa kwako.
 
Asante Mh. Dr. W. P. Slaa, ubarikiwe. Kwangu mimi binafsi, familia yangu, ndugu zangu, wafanya kazi wenzangu, watanzania wenzangu na rafiki zangu popote walipo nchini Tanzania na nje ya Tanzania, wewe ni shujaa wetu. Wananchi wametimiza wajibu wao wa kikatiba wa kumchagua kiongozi wanayeamini ana uwezo wa kuwaongoza katika kipindi cha miaka mitano kutoka 2010 mpaka 2015 lakini uamuzi wao unataka kuchakachakuliwa na waovu wasioitakia mema Tanzania. Badala yake waovu hawa wanatafuta kila njia ya kujikwamua kwa kung'ang'ania madaraka bila kujali matakwa ya wananchi kwa njia za giza, ulaghai, wizi wa kura na nguvu za dola. Hata hivyo tuna imani kuwa moto uliouwasha hautazimwa hivi hivi wala taa ulioiwasha mwanga wake hautatoa nafasi kwa giza hili zito lililo mbele yetu. Kwa hili hatukati tamaa, a luta continua !
 
Kura za JK kutoka Afrika Kusini, zimeingizwa kwa wingi sana majimboni, na vituo hewa vipo vingi mno.
 
nashauri chadema watoe tamko lenye facts mapema

ili tupambane na hawa jamaaa
 
Angalau nitapata usingizi manake nilinyong'onyea sana baada ya kuona viongozi wa chadema kimya kabisa.
 
Bw. Rutashubanyuma,

Naomba uwe REALISTIC. Huwezi kuanza kuhesabu kura zilizoharibiwa; zingine zimechomwa moto, zingine zimeongezwa (mfano, kuna watu wako Lupango kwa kukamatwa na masanduku ya kuchakachulia). Cha kufanya ni kujumlisha UPYA, siyo kuhesabu kura!


Mmoja wapo ni Makongoro mahanga alikamatwa live juzi na ....polisi akiwa na masanduku ya kura kwenye gari ambayo yamepenyezwa kwenye kura za buguruni......kama kuna mtu unamfahamu pale buguruni police wanajuwa hilo[but kwa amri toka juu imeagizwa taarifa hiyo ibaki siri]..nina uhakika hizo kura alizopenyeza za maruhani zitampa ushindi maana nasikia alikuwa amezidiwa kura chache na mpiganaji Mpendazoe
 
Ni mkewe usitake kujua zaidi. Kula jiwe. Kauka.:shut-mouth::shut-mouth::shut-mouth:
 
Inaudhi sana kwa kweli,huu ni uhuni wa waziwazi kabisa unafanyika,matokeo sehemu zote ambazo wamezidiwa hawayatangazi hata kidogo,huyo anayesoma matokeo hata nafsi yake inamsuta,lakini mstari umeshachorwa na Historia itawahukumu siku za usoni!
 
i don believe in majic, i believe in the present and seenable
Dr Slaa you are the Presdent to be in my country
 
Mi nasema siko nyuma yako Dr. ila NIKO SAMBAMBA NAWE, BEGA KWA BEGA tusonge mbele mpaka kieleweke. Najuwa Central Criminal Mob wanajifariji kwa walichokifanya. Nakuelewa na NINAKUAMINI kwa UMAKINI wako. Kusanya data za kutosha kisha uutangazie ulimwengu nini kilicho tokea kwamba si uchaguzi bali ni usanii wa demokrasia,:doh:
 
Wala mie sina wacwac wee waache watangaze kwanza halafu Dk wee subiri najua wameiba tena sana tu, tafuta evidence kama kawaida yako then tuwaumbue!!! hatuna presha
 
Hongera Baba kwa kazi nzuri na nzito, kweli umakini wako ni chachu muhimu katika Taifa letu, asante sana. Tuko pamoja nawe!!!!:smile-big:
 
Nawashukuru wote mliojitokeza kupiga kura na kukipa chama chetu ushindi wa kukumbukwa, ushindi wa kihistoria mkikaribisha mapambazuko mapya ya uongozi katika taifa letu. Kama ilivyokuwa kwenye matokeo ya Ubunge matatizo yamehamia kwenye matokeo ya Urais na kutokana na unyeti wa nafasi hii tunahitaji uangalifu katika kushughulikia. Msife moyo kwani tukiwa tayari muda si mrefu ujao tutazungumza nanyi kwa taarifa zaidi.

Dr. Wilbrod Slaa | Facebook

Ina maana kwenye UBUNGE tayari mshamaliza?
 
Dr tunajua na CCM/JK/NEC wanajua kile walichokifanya ktk kura za urais ila wasishangae kitakachotokea watakapotangaza siku ya mwisho!
Piga ua uchakachuaji wa hali ya juu umefanyika,angalia sehemu kama Karagwe,Shy mjini,na kwingineko ni dhahiri kabisa wizi mtupu!!
Dr tupo nyuma yako tunasubiri tamko rasmi.
 
Back
Top Bottom