Tamthilia na Mpira zinavyochangia migogoro ya ndoa

Tamthilia na Mpira zinavyochangia migogoro ya ndoa

Black Butterfly

Senior Member
Joined
Aug 31, 2022
Posts
130
Reaction score
368
Wanawake na wanaume wengi ni wapenzi tamthilia za vipindi vya maigizo na mechi za mpira na kuwa wakati wengine hujikuta wakisalia sebuleni au kuweka umakini kwenye TV na kuacha wenza wao wakitangulia kulala peke yao au kukosa wa kuzungumza nao mambo mengine ya kimaisha

Vitendo hivyo vinafanya wanandoa wengi wajione wapweke na wakati mwingine wanaona hakuna umuhimu wa kuoa au kuolewa na mwisho hali hiyo inazalisha migogoro ambayo hatima yake ni kuvunjika kwa ndoa kwa kuwa baadhi hujiongeza kutafuta faraja nje ya ndoa zao.

Wanandoa watambue kuwa wenzao wanapenda kusikilizwa hasa wanaporudi kutoka kwenye mihangaiko ya ya kila siku, hivyo wanahitaji kufarijiwa na wenza wao sasa inapotokea mmoja kati yao anaanza kuwa na ratiba nyingine baada ya mihangaiko inawapa ugumu na kuwanyima nafasi ya kuzungumza au kuwa karibu na wenza wao.

Nashauri kuwa pamoja na kuwepo mapenzi binafsi ya vipindi vya TV bado wanandoa wanatakiwa kujua kuwa wanawajibika kupeana muda wao kwa wao bila kujali kuna vipindi gani vipo kwenye TV. Vinginevo hali hiyo isipodhibitiwa huwa chanzo ha kuharibu mahusiano mengi ya ndoa na familia kiujumla.
 
Ni kumuelewa tu mwenzako.

Muda mwengine ni kumpa mwenzako nafasi ya kufanya anachopenda maadamu hakina madhara. Na muda mwengine burudika pamoja nae.

Mi wa kwangu wote tunashangilia Man U. Wote ni wapenzi wa movie ijapokuwa mi napenda za adventure, horror n.k zaidi.

Tamthilia zimenikalia kushoto labda nimpe sapoti tu kwa sababu huwa sipendi tutofautiane kwa vitu ambavyo vinaepukika.

Ninachopishana nae kwenye mazoezi tu hataki kufanya. Anakula sana hainipi shida ni vizuri. Shida ni mwepesi wa kunenepa. Huwa namwambia afya bora inaendana na mazoezi.

Ila nampenda hivyo hivyo! Ana macho mazuri, mashavu mazuri na rangi nzuri. Nikichanganya na tabasamu lake usoni mwake masha Allah! Naburudika!
 
Mm napenda sana Telemundo movies,mpira ni kidogo sana.ila Kwa kuleta usawa inabidi tuwe na support Kwa Kila burudani.

Ila yote ayo ata kama mnaongea na kujuliana hali mwisho wa siku duniani ni batili[emoji23].
 
Hakika technology inatupeleka mbali sana tumekuwa binadamu tunaohitaji kujifunza na kuonana mengi at once wewe wewe utafute hela, wewe utunze familia, uende kuangalia mpira, upate muda na mwenzako, marafiki, ndugu, ni vigumu otherwise uache kimoja ufanye kingine na ni vizuri kama kila mmoja akimsoma mwenzake!
 
Sikuiz ata ukihisi kumiss unyumba unamkuta kitandani hana boxer uku kashikilia sim anabishana na wanagrp la man u we jiingizie ulale hutaki acha,,.
 
Back
Top Bottom