TANESCO board split on MD Rashidi's fate


- Lakini hao watu wanaweza pia kuja hapa na kusema jana Mzee Kombo kasema kumbe hakusema yeye ila ni jamaa tu katika familia yake, standards za uandishi sio kazi yetu JF kuamua, kazi yetu JF ni ku-deal na hoja, facts na evidence.

- Zitto ana haki zote za kuwafikisha kwenye sheria kama imevunjwa na hayo maneno ya gazeti, it is none of our business, our business ni kukata ishu kwa kuchambua maneno ya Zitto na maneno ya gazeti katika kutafuta masilahi ya taifa! na wala sio tatizo kuyaona masilahi ya taifa katika hii ishu yapo wazi tena nje kabisaa!

Respect.


FMEs!
 

Ingependeza ungeyataja mengine ya binafsi kama yapi ili tuweze kuyachekecha zaidi.

So far mi naona hoja tupu hapa, kuna hoja nyingine zinagusa nafsi by default kwa sababu zinahusu verifiability of the source, kwa hiyo huna jinsi ila kuhusisha watu binafsi, kwa sababu hoja na mtu vinachanganyika. Na kama mifano ya familia inakukwaza hapo ndipo utakapoona umuhimu wa point yangu kwamba waandishi hawatakiwi kuandika vitu visivyo verifiable na attributable.
 

- Wapi hapo nilipokwazika na familia au unajisema mwenyewe mkuu? Mimi ninakata ishu ninasema kwamba Zitto amesema na amenukuliwa kama alivyosema na yeye amethibitisha kwamba alisema lakini imeandikwa gazetini kwa nia mbaya, sasa hatachangia tena JF, kwangu inaeleweka na sioni tatizo,

- Naona kuna mnaojaribu kumtetea kuliko alivyjitetea mwenyewe, that is wasup!


Respect.


Es!
 
Ingependeza ungeyataja mengine ya binafsi kama yapi ili tuweze kuyachekecha zaidi.

- Hukuona pale juu niliposema Mzee kombo, yaani aliyekwua mbunge wa zamani wa Tanga mjini au?

- Mkuu tunaweza tu kwenda mifano ya familia kama unavyotaka haina noma!

Respect.


FMEs!
 
- Hukuona pale juu niliposema Mzee kombo, yaani aliyekwua mbunge wa zamani wa Tanga mjini au?

- Mkuu tunaweza tu kwenda mifano ya familia kama unavyotaka haina noma!

Respect.


FMEs!

Mzee Kombo sijapata bahati ya kumfahamu.

Since you are a big fan of keeping things simple.

Unaona sawa au si sawa kwa waandishi kuja hapa na kufanya quotations bila further verification?

Hii ndiyo beef yangu.
 
-
- Naona kuna mnaojaribu kumtetea kuliko alivyjitetea mwenyewe, that is wasup!

Respect.

Es!

Mkuu issue sio kumtete Mh. Zitto, issue tunajaribu kutetea haki yake ya kikatiba ya kutoa maoni na uhuru wa kujieleza. Kama wakati wote akitoa maoni watu wanajaribu kuyatumia kwa njia tofauti na kuywakilisha kwa mitazamo itakayomchonganisha na jamii hilo ni hatari, tunapaswa kuliona na kukemea. Mwandishi alikuwa sahihi kumquote Zitto, lakini kama anavyosema Bluray alipaswa kuverify kutoka kwakwe mwenyewe. Mbona hata uwazi wanawatafuta wahusika na kuwahoji pamoja na kuwa wanakuwa na picha zao za kufumaniwa? Hawa walishindwa nini??

Jambo la Pili tunatetea maadili ya uandishi wa habari, Watu kuwa na realible, Aunthentic source. Source ambayp it will not be questionable. It should be proved beyond doubt kuwa unachoongea ndicho kilichotolewa na huyo unayesema ni mtoaji wa hilo ulilowakilisha. Kulikoni hapa walichemsha, wameshusha credibility yake.

Na wewe na mwenzio Tina mnakubalina kuwa Zitto ajitoe kwenye hizi Forums, na hilo naliona lilikuwa lengo la Kulikoni, kumfunga mdomo, sasa nyie mnashabikia kwani kuna madhara naamini mnayapata (I am judgemental) kutokana na kuzungumza kwake.
 
Unaona sawa au si sawa kwa waandishi kuja hapa na kufanya quotations bila further verification?

Hii ndiyo beef yangu.


- Mkuu haya ni maoni yako, yangu ni kwamba Zitto amesema au hakusema, kama amesema amesema, it does not matter amesemea wapi na namna gani sasa hapa verification ya nini tena?

Respect.


FMEs!
 

- Unajua inafurahisha sana kwamba leo unataka maadili ya uandishi, ninasema hivi the ishu ni kama Zitto amesema au hakusema, muandishi hakuwa na sababu ya ku-verify anything,

- Kama Zitto anataka kuondoka sina uwezo wa kumzuia, lakini ninachotaka ajue kwamba siamini kwamba muandishi amekosea anything, yeye amesema na imeandikwa kama alivyosema, kama katiba yake imevunjwa angesema lakini masikini ya Mungu hakusema hivyo amesema maneno yameandikwa kwa nia mbaya, kwa bahati mbaya hatuna sheria za ku-deal na nia mbaya au nzuri!

Nimemaliza hapo wakuu!


es!
 
Inshort JF sio source ya kutoa habari nje katika jamii.
 
- Mkuu haya ni maoni yako, yangu ni kwamba Zitto amesema au hakusema, kama amesema amesema, it does not matter amesemea wapi na namna gani sasa hapa verification ya nini tena?

Respect.


FMEs!

FMES unachekesha sana mazee.

Sasa bila verification utajuaje kama kasema au hakusema?

I mean unasema kabisa "yangu ni kwamba Zitto amesema au hakusema" (unaonyesha umuhimu wa kuwa na uhakika kwamba amesema au hakusema)

Halafu hapo hapo unajikanganya kwa kusema "sasa hapa verification ya nini tena"

Verification ya nini wakati hujui kama alisema au hakusema? Bila verification utajuaje kama alisema au hakusema?
 
Nakubaliana na wewe kwa sana ni nguvu ya ufisadi

Kuna mahali gani Zito original alikowahi kulalamika kuwa jina lake linatumiwa vibaya?


Asante sana mkuu hapo umewakoma manyani giladi. Aibu tupu eti mara eti tutajuaje aliyeandika mara waandishi mara imemepotoshwa almradi kuchanganya watu. Umewauliza vizuri tu. Alisema hakusema? Hawana majibu.

Tina kakujibu vizuri tu


Ningestaajabu sana kama mpambe wa mafisadi usingekuja hapa na kuanza kumshambulia Mengi.

My take ni kwamba Kulikoni wamewakilisha maoni ya JF kwa watu wasionauwezo wakufikia mtandao. Gazeti hata likifungiwa chapati laweza kusomwa. Badala yakuwashutumu inatakiwa kuwashukuru
 
Huyu jamaa kisha poteza mwelekeo, kishakula hela za watu hana tena uhuru wa kusema mambo yake. Misimamo yote kwisha.


Kakutuma nani kuja kuturubuni hapa ? Zitto kama mtu ukiondoa Ubunge wake ana haki ya kusimamia ancho kiamini . Kama anadhani Idrisa ana quality hizo na sisi tunaona Idrisa hana ni kumpinga Zitto kwa heshima na si kejeli za kijinga kama hizi za huyu jamaa hapa juu . Names calling na uongo umeanza lini hapa JF . Tume ingiliwa na ndiyo maana wengine tunakuja hapa mara moja moja na umakini maana najua CCM wamejipanga haswa .Ila ni kweli hapa sisi wazee wa siku nyingi wa JF hatuli kasa . Pole sana .
 
 
Wakuu nawaomba tuendelee kuitunza sifa ya JF kwa kumkoma nyani bila kumtazama uso awe Zitto au Jepesi ndiyo jadi yetu hapa. Pili mara nyingi magazeti mbali mbali yameandika mambo mengi tu source kubwa ikiwa JF lakini sijashuhudia mjadala kama huu kuhusu Kulikoni, sasa nawauliza kulikoni ? Ni kwa sababu mfalme kaambiwa yuko uchi ama vipi ? Hakuna mahali msimamo wa Mh. Zitto umewahi kusifiwa na kuungwa mkono hapo nyuma kuliko hapa JF, hili linathibitika kwa kuperuzi kidogo tu michango ya huko nyuma - labda kwa wageni wa JF.

Ni pale tu alipoanza kuchukua misimamo iliyoshabahiana na mafisadi ndio wengine tulianza kuhoji, ja Zitto kulikoni ? Nakumbuka mara ya kwanza alipokosolewa, alihamaki hadi akatoa maneno humu ambayo hivi leo bado atakuwa anayajutia - siju alitegemea nini, kusifiwa tu ? Ukweli ni kuwa wengi wanaopinga msimamo wake kwa sasa ni wale waliomuunga mkono mwanzoni na wanaomshabikia kwa sasa ni wale waliokerwa na msimamo wake wa mwanzo. Ni juu yake Zitto kuamua kuwa kati ya haya makundi mawili, lipi lamtakia mema.

Kwa kifupi tuliokuwa mashabiki wa Zitto mwanzoni tunakerwa na mambo yafuatayo:

  • Kuchangamkia kamati ya Kikwete ya madini badala ya kamati ya Bunge.
  • Kutetea ununuzi wa mitambo ya wizi ya Dowans.
  • Kupendeza tume huru eti ya majaji kuichunguza upya Richmond.
  • Kuusifu utawala huu pamoja na mapungufu yake.
  • Kumwita Rashidi eti one of the best CEO the country ever had.
Nawapa pongezi wote ambao mmesimama kidete kutetea msimamo wa JF kama the place where we dare !. Wengine wanaruhusu mapenzi yao ama chuki zao kwa mtu kutawala fikra na mawazo yao na hii hakika ni hatari sana. Kocha mzuri wa timu ya soka atasifiwa pale tu timu ikifanya vizuri na kubeba kombe - nje ya hapo, hafai. One of the best CEO na shirika linachungulia kaburi, wapi na wapi !
 
Eti Mwandishi wetu Dar!! Unajificha ficha unaogopa nini kuweka jina lako kama una uhakika na unachoandika?


Duu sio mchezo nadhani sasa hivi Chadema ipo under fire,watu wanapiga majungu mpaka waone hawana mwelekeo wowote!!
 

Thank you....Thank you...thank you Mkuu Mushi.........

Katika hiyo taarifa gazetini sidhani kama kuna ubaya wowote....isipokuwa kama mwandishi.......alitakiwa azingatie hayomaneno ya Zitto "devil advocate"....ni maneno muhimu ili kuelewa ni jinsi gani Mh zitto alitaka mjadala wa Dr Idriss uwe......na alisema yuko huru kubadili msimamo wake endapo itathibitishwa visivyo..........

....nahisi kwa Mwandishi alikosa kulisema hilo ndio maana Mh Zitto ame-point kuwa......."mwandishi ana nia mbaya"...............
 

Mh FMES nina amini utasimamia maandiko yako Mh yuko mbioni kujiunga nanyi CCM binafsi halitanishangaza hata kidogo! tuliache hilo, hiki kinachoendelea hapa ni kutiana ujinga tu!

Respect
 
 


Mheshimiwa Zitto kwanini uwakimbie hao watu?Gazeti hili mmiliki wake unamjua, agenda yao unaijua.

haya ni matokeo yako ya kugombea uenyekiti. ungekuwa mwepesi kama Kafulila ungekuwa umevuliwa uanachama lakini kwa vile wewe ni Mzito kama jina lako wenye NGO hawa njia ya kukutoa zaidi ya kukuletea habari kama hizi.tunakuhitaji sana.

tizama habari zako zinavyopewa uzito na JF ikiwa mbaya ndiyo zaidi lakini ikiwa ya yule mtia saini za akaunti ya Chadema zinaminywa na kufichwa.
mimi nikiandika habari yeyote lazima ibadilishwe kichwa cha habari kama ni ya Mwenyekiti na kutafuta kichwa cha habari kilichokaa vizuri kumfurahisha Mwenyekiti.

wewe baki na changia hapa.sisi ndio tunaofaidika na habari zako.wabaya haya ukiwakimbia hapa utakutana nao njiani.huna njia ya kuwakwepa.jihadhari na safari za magari na uwe na dereva mmoja unayemuamini ikiwezekana awe ndugu yako. please rudi mkuu Zitto.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…