TANESCO board split on MD Rashidi's fate


Pasco nakubali muda wake umeisha sikatai kuna kurudishwa ofisini au kutolewa kabisa but huyu mzee ni mtu makini kwa hili mie siko pamoja na nyinyi. Na pia mzee muda ukiisha na usiishe mtu huweza kuongezewa contract ya mwaka mmoja au mitatu kutokana na umuhimu wake ndani ya shirika. Lakini kusema aondoka hatufai nyie kama nani???

Na pia kuna kikundi cha watu kinasema public opinion imesema wapi?? mnadai Rashidi alikuwa hana ethics kuna ethics gani ??? wizarani katibu mkuu inasemekana yuko karibu au anatembea na mkurugenzi mmoja wa fedha pana ethics za kikazi??? mie mjadala wangu sio idrissa tu wengine je wakoje???
 

Sasa wewe unayesema aongezewe muda, unasema hivyo kama nani?

Unatulaumu kwa majungu halafu unaleta ya katibu Mkuu na Mkurugenzi wake! Unaweza kuweka facts za haya madai yako?

Aondoke tu. Won't shed no tears!

Amandla......
 
Wewe mie sijasema katibu mkuu hafai kama anafanya kazi yake na kwa ufanisi his personal life is none of my business. But unapozungumzia ethics za kazi kwa Tanzania hakuna ethics kabisa labda tuanze kuwafundisha vijana wetu elimu ya utendaji kazi but hakuna ethics kwa Tanzania.

Wewe unaedai humtaki Rashid tupe sababu mzee!!! acha blah blah
 
Sasa wewe unayesema aongezewe muda, unasema hivyo kama nani?

Unatulaumu kwa majungu halafu unaleta ya katibu Mkuu na Mkurugenzi wake! Unaweza kuweka facts za haya madai yako?

Aondoke tu. Won't shed no tears!

Amandla......

Kwenye mashirika ya umma sasa hivi miaka yako ikifika ni kuondoka, hiyo ya kuongezewa mkataba nadhani imekwisha?? au kwa kibari maalum cha mwaka mmoja hapo sijui tuhabarishane.
 

Hivi majungu kwako ni kusema mtu hafai tu? Wewe unapo-insinuate Katibu Mkuu ana uhusiano usio mwema na Mkurugenzi wake hauoni kuwa ni majungu? Halafu, bila aibu unasema kuwa personal life yake ni none of your business! sasa ulimwingiza humu wa nini?

Sababu kede kede umetolewa lakini haukubali. Hatuko hapa kupotezeana muda. Endelea kumpigia debe swahiba wako lakini wengine tunamuona bomu. Aondoke.

Amandla......
 
wizarani katibu mkuu inasemekana yuko karibu au anatembea na mkurugenzi mmoja wa fedha pana ethics za kikazi??? mie mjadala wangu sio idrissa tu wengine je wakoje???

Basi kama ni hivyo umepotea njia - mada hapa inaihusu bodi ya TANESCO na hatma ya Swahiba wako Dr. Idris. Ukitaka kuwajadili na wengine anzisha mada na tutachangia. Unawaingiza hata marehemu Dr. Balali humu na BOT, je wajua Balali alivyochambuliwa humu mpaka siku anaingia kaburini kama aliingia kweli. Huu utetezi wako kwa hili jizi si bure kwani maCEO wangapi wameongelewa na kutupiwa madongo pamoja na bosi wao anaewateua. Hivi una habari Tanzania ni nchi pekee duniani ambapo ukiutaka umeme eti ununue nguzo ya kukufikishia umeme nyumbani kwako - huu ni ujinga, wenda wazimu na wizi wa nchana kwani baada ya hapo eti hiyo nguzo inakuwa mali ya TANESCO ! Acha hizo, Dr. Idris Rashidi ni moja wa mafisadi wakubwa wa nchi hii na wako wengi tu.
 

Kwa namna moja ama nyingine namkubali dr. rashid, na kubwa zaidi ni kwamba kwa mazingira ya nchi kama ze2 anahitajika m2 anayeweza kukisimamia kile anachokiamini bila kuyumbishwa na wanasiasa. Hata hivo sukubaliani na ww kwamba dr. rashid ndie aliyeifikisha nmb hapa ilipo kwani nae kaikuta ikiwa ni ggod performing bank ikishindana na nbc,std pamoja na crdb na ndio status iliyonayo hadi hivi sasa
 

Kusimamia kile anachoamini kama kukarabati nyumba kwa shilingi milioni 650 katika nchi masikini kama Tanzania?

Ndicho anachoamini hicho? Ndio msimamo wake madhubuti huu?
 

This is non-sense kwanza mie nimetolea mfano Balali na madudu yake BOT. Pili sina haja kuanzisha thread nyengine ikiwa hii bado haijajibiwa. Wewe unanunua nguzo. Wakati wa Kasambala nakumbuka mzee wangu alilipa laki 7 kuunganishiwa mita hapo bado akaja kulipa 35000 ya mita yenyewe na kuhonga juu. haya nani msafi!!

Acheni bwana ufisadi Tanzania nzima imeoza leo nimesoma article moja online inasema TRA kuna watu wanakopa milioni 800 halafu unaweza kurudisha bila ya kudaiwa yale yale ya EPA!!!! Hii nchi kweli tunakoelekea kuzuri!! mafisadi wanadhani nasie hatupendi kuendesha bmw x5 au vogue mjini!!!
 

Mdondoaji, nashauri, tuishie hapa tulipokubaliana kuwa muda wake umeisha, he is one of the best CEO ever Tanzania has ever had!, sawa. Mpaka afie kazini?. Ile dola laki sita ya mgao toka vijisent, ilionyesha kakopa kwa mradi wa kuku, haikuonyesha kalipa, haufikiri huu ni muda muafaka apumzike aput his house in order atajakufa na madeni!, dunia ya leo, the end, justfy the means, siku yako ikifika, watu wanaangalia umeacha nini, sio ulifanya nini, ndio maana kina Ben walijimegea mapande ya kuacha material legacy let alone moral legacy, watoto wako na watoto wa watoto wako, watakula morals or materials, no wonder life is more materialistic than realistic. Dr. Rashid, thanks for a good job, well done!, now its time to take a break, just rest!.
 

Mwongo usie na haya. Wakati wa kasambala laki saba unanua kijiji! Hautakumbuka lakini ni wakati wake huo ambapo tulibinafsisha nyumba zilizokuwa na thamani ya zaidi ya sh. laki moja kwa sababu ni za kifahari!

Unamtetea swahiba wako ati kwa sababu wengine wanafanya maovu? Upuuzi mtupu.

Amandla.....
 

Mwongo wewe ndiye uliyezitoa laki saba??? Unasahau wakati wa Kasambala kupata mita ulikuwa unakaa miezi if not miaka kuipata hiyo mita eti kuna foleni ndefu!!! Au wewe ndie uliyekuwa ukisimamia umeme Tanesco acha uzushi bro Hakuna hoja ya kwamba Rashidi afai zaidi ya smear campaign zenu za kijinga eti fisadi mnao ushahidi majungu majungu tu!!!

Wewe kama unamtetea Kasambala mie simtetei either of them but mzee huyu amejitahidi best CEO aliyepo sasa katika Parastatal mzee huna sababu za kumpinga zaidi ya majungu majungu yasiyokuwa na mpango

Eti Public opinion!!! mlipiga nyie mnamchukia mzee wa watu labda
 

Kasambala aliongoza Tanesco miaka ya 70. Dola ya Marekani ilikuwa Sh. 7.50. Sasa unataka kutuambia kuwa mzee wako aliombwa takriban dola 100,000( zaidi ya sihilingi milioni 100 kwa hela ya sasa) kuangishiwa mita? Halafu yeye akakata dola 5,000 ( karibu milioni 5) za sasa! Au haujui Kasambala alikuwepo wakati gani? Wakati wa Kasambala nauli ya DMT ilianzia senti 20! Ulizia kwanza kabla haujabandika.

Amandla......
 
Mdondoaji
Mdondoaji is always against unfairness
Senior Member



Duuhh.......hivi nikukuita wewe sio fair kama unavyodai hapo juu nitakuwa nimekosea?.........

yaani unaona kwa CEO kutumia millioni 650 "kukarabati" nyumba ni fair kwa sisi walipa kodi?
 

Fundi Mkuu.........msamehe bure ndugu yetu huyo......

.......ajabu sana unaweza kuta watu kama hao ndio washauri wakuu serikalini.........hawawezi hata "jumlisha/kutoa" issues.........
 
Mkuu heshima mbele labda niulize nani alikuwa mkurugenzi mkuu wa Tanesco 1986-1990? Halafu nikuandalie majibu. Na hiyo exchange rate ya 1960s unataka kuniambia iliremain constant hadi 1985?
 
Mkuu heshima mbele labda niulize nani alikuwa mkurugenzi mkuu wa Tanesco 1986-1990? Halafu nikuandalie majibu. Na hiyo exchange rate ya 1960s unataka kuniambia iliremain constant hadi 1985?

Naona utoto au ujinga ndio unakusumbua ndugu yangu - kama nilivyosema mwanzo huu utetezi wako una lake.

  • Katika kipindi cha miaka zaidi ya ishirini toka tupate uhuru mwaka 1961 thamani ya dola moja ya marekani ilikuwa chini ya shilingi kumi hadi wakati Mwalimu anang'atuka mwaka 1984.
  • Katika kipindi cha miaka kumi ya Mwinyi thamani ya dola iliweza kupanda na kuvuka shilingi mia mbili wakati anaachia madaraka.
  • Katika kipindi cha Mkapa thamani ya dola kwa mara ya kwanza iliweza kupanda hadi kuvuka shilingi elfu moja wakati anaachia madaraka.
 
Huna haja tena ya kuendelea kutoa ufafanuzi kwake, kwani anabisha ili abishe ilhali hali halisi inafahamika...

Shukrani kwa ufafanuzi juu ya maendeleo ya shilingi dhidi ya dola..
 

Mie sio mjinga na mtoto kama unavyofikiria but sikukatazi uhuru wako wa kuzungumza. Pili inawezekana kabisa Kasambala hakuwapo kipindi hicho but it does preclude who was in charge (ambaye si Idrissa) kutumaliza sisi walalahoi kwa kutucharge laki saba tuunganishiwe mita kisa eti ziko haba.

Pia huna haja ya kunielekeza jinsi exchange rate zilivyobadilika and for your information exchange rate zimeanza kubadilika after the Kagera war sema kutokana Central bank controlling mechanism (Hakuna kununua fedha hadi utoe sababu) pesa ya Tanzania ilikuwa ikishuka taratibu. Mzee mwinyi alipokuja akaruhusu free market economy ndipo thamani ya shs iliposhuka kwa kasi but kilichoishusha pesa ya Tanzania ni vita vya kagera.

Msilete hoja zenu za kipuuzi na kujitia mnajua kuzungumza leteni hoja za msingi humu JF mnamuandama Idrissa mnatuletea sababu za majungu majungu na siasa ili aonekane hafai
 

Hii unaitoa wapi ? Tumeingia vita ya Kagera dola ikiwa kati ya sh. 7.00 na sh. 8.00. na tumemaliza vita dola ikiwa bado sh. 8.00. Miaka mitano baadaye 1984 dola ilikuwa bado ni chini ya sh. 10.00. Haya madai yako unayatoa wapi ? Kama kuna kitu alikitaa Mwalimu kata kata ni misaada yenye masharti na sharti mojawapo lilikuwa ni kushusha thamani ya fedha yetu. Unajua kwa nini alituomba tufunge mkanda ? Utanisamehe huu ni mchango wangu wa mwisho, kwaheri.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…