TANESCO inarudi mikononi mwa mafisadi?

TANESCO inarudi mikononi mwa mafisadi?

Kuna combination chachu sana kwenye hii wizara, kuanzia waziri mwenyewe, bodi aliyoiunda, Zitto, na uhusiano wao na mwenye mamlaka ya nchi, historia zao huko tulipotoka hazileti matumaini kabisa kwenye suala la kumkomboa mtanzania wa hali ya chini, tupo kwenye circle ya wapigaji tunaishi kwa matumaini tu.
Hiyo combination iliyopo sasa ni hatari Sana. huwezi amini zitto ndio wanamtumia kusema
 
Ufisadi haujawai kuisha TANESCO hata awamu ya mwendazake ulikuwepo tena wa kutisha...kila awamu inakuja na MAFISADI wake ila kinachofanyika ni kuwabrain wash WADANGANYIKA kwamba tulikuwa tunaibiwa sana.
Mkuu pamoja na ubaya wote wa mwendazake,Ila kwa Tanesco tutakuwa tunamuonea. Hakukua na kampuni ilifyofilisi Tanesco Kama kipindi Cha Dowans, Richmond, iptl, symbion n.k
Fikiria tu kipindi hicho symbion aliingia mkataba na Tanesco ili kuwauzia umeme milele.
Wanasheria wa Tanesco wanaishauri Tanesco ivunje mkataba na Dowans, alafu haohao wanaenda mahakamani tena kuiwakilisha Dowans.
 
Mafisadi walianza muda mrefu Sana kuila tanesco record zinaonyesha TANESCO ilianza kuliwa toka mwaka 1994.

Magufuli alipoingia akajaribu kuwaondoa mafisadi wote kuliteka shirika la TANESCO ingawa alikuwa anatumia nguvu ila kiasi alifanikiwa ingawa watu Kama Tundu Lissu walimshauri kwamba atengeneze Sheria zitakazodumu muda wote kwenye rasilimali za Nchi.

Kwa kujua atatawala milele aligoma na kujisemea atawashugulikia apendavyo na kweli aliwashughulikia .

Sasa hayupo yamerudi ndani ya shirika labda angemsikiliza Tundu Lissu juu ya kufuata mfumo wa Bolivia leo tungekuwa salama.

Walianza kuwatumia watu wanaotumbuliwa kuongea bungeni, Mnakumbuka kauli ya Nape kwamba serikali awaachie sector binafsi kuwekeza kwenye umeme? Jamaa alitaka Rufiji ijengwe na sector binafsi na wawauzie umeme tanesco.

Yaani turudie Yale Yale ya Symbion, Dowans, Richmond na IPTL!!

Leo January na Zito wakitumiwa na magege ya wezi na mafisadi wanataka kuuza hisa za tanesco shirika la umma ili umeme wa Nchi ulioshika usalama wa taifa uwe chini ya matajiri?

Waipangie Tanesco Bei ya umeme Kama wanavyotaka?

Vyanzo vyote vya umeme vilivyojengwa kuanzia utawala wa nyerere Leo viwe chini ya mjamaa tu wengi wao Wala hata hawaishi nchini!!

Yaani hatujifunzi tu kutokana na makosa, sasahivi umeme umeanza kukatika katika hovyo tu na biashara za vijana mnajua zinategemea umeme,!!

Kuna maeneo unaamhiwa umeme unakatika mara 5 kwa siku Sasa najiuliza Yale majamaa yakiingia Tena tunapona ? Wakati yanaingia na mikakati ya kuagiza makotena ya Generator?

Vijana waliojiajiri na masaloon waliomaliza vyuo wanaishije!! Tuiombee tanesco na Nchi.
Wewe ndiyo ulikuwa kinara wa kumtukana Magufuli , acha laana iwatafune mtanyooka tu na bado.
 
Ufisadi haujawai kuisha TANESCO hata awamu ya mwendazake ulikuwepo tena wa kutisha...kila awamu inakuja na MAFISADI wake ila kinachofanyika ni kuwabrain wash WADANGANYIKA kwamba tulikuwa tunaibiwa sana.
Ufisadi wote tunaujua toka mkapa Hadi Kikwete haya tuambie wa Magufili.
 
Ufisadi wote tunaujua toka mkapa Hadi Kikwete haya tuambie wa Magufili.
Kuna watu ni wagonjwa wa chuki za kupitiliza kwa JPM. Hata Lissu aliyepigwa risasi yapo mengi ameanza kujua uhalisia wa mambo hasa picha halisi za wanasiasa wengi. Tatizo kubwa la Lissu kwa JPM na alilojitahidi kumrekebisha (ingawa hakuwa na approach rafiki) ni ubabe ambao wakati mwingine unakosa maarifa ya msingi. Ziko vita unaweza kushinda bila kuingia vitani.

Ila ukimpa Lissu nchi leo tofauti yake na JPM ni atatumia sheria halali kunyoosha watu ila Lissu ni aggressive kama JPM! Akiwa Rais hata Chadema wenyewe watachukia kama ilivyotokea kwa CCM dhidi ya JPM.
 
Kuna watu ni wagonjwa wa chuki za kupitiliza kwa JPM. Hata Lissu aliyepigwa risasi yapo mengi ameanza kujua uhalisia wa mambo hasa picha halisi za wanasiasa wengi. Tatizo kubwa la Lissu kwa JPM na alilojitahidi kumrekebisha (ingawa hakuwa na approach rafiki) ni ubabe ambao wakati mwingine unakosa maarifa ya msingi. Ziko vita unaweza kushinda bila kuingia vitani.

Ila ukimpa Lissu nchi leo tofauti yake na JPM ni atatumia sheria halali kunyoosha watu ila Lissu ni aggressive kama JPM! Akiwa Rais hata Chadema wenyewe watachukia kama ilivyotokea kwa CCM dhidi ya JPM.
Lisu ni bingwa wa kujipendekeza kama Zito tu wala hawana uaggressive wowote.
 
Ndo hvyo ndugu technically, hata tukisema Hadi tulie, wenye mpini wanafanya yao cc tunaleta jukwaan..two different dimensions..na hakuna wa kuwazuia, unaweza kukuta wanasoma post wanacheka tu
Wewe ni mmoja wao nn Mkuu???
 
Mafisadi walianza muda mrefu Sana kuila tanesco record zinaonyesha TANESCO ilianza kuliwa toka mwaka 1994.

Magufuli alipoingia akajaribu kuwaondoa mafisadi wote kuliteka shirika la TANESCO ingawa alikuwa anatumia nguvu ila kiasi alifanikiwa ingawa watu Kama Tundu Lissu walimshauri kwamba atengeneze Sheria zitakazodumu muda wote kwenye rasilimali za Nchi.

Kwa kujua atatawala milele aligoma na kujisemea atawashugulikia apendavyo na kweli aliwashughulikia .

Sasa hayupo yamerudi ndani ya shirika labda angemsikiliza Tundu Lissu juu ya kufuata mfumo wa Bolivia leo tungekuwa salama.

Walianza kuwatumia watu wanaotumbuliwa kuongea bungeni, Mnakumbuka kauli ya Nape kwamba serikali awaachie sector binafsi kuwekeza kwenye umeme? Jamaa alitaka Rufiji ijengwe na sector binafsi na wawauzie umeme tanesco.

Yaani turudie Yale Yale ya Symbion, Dowans, Richmond na IPTL!!

Leo January na Zito wakitumiwa na magege ya wezi na mafisadi wanataka kuuza hisa za tanesco shirika la umma ili umeme wa Nchi ulioshika usalama wa taifa uwe chini ya matajiri?

Waipangie Tanesco Bei ya umeme Kama wanavyotaka?

Vyanzo vyote vya umeme vilivyojengwa kuanzia utawala wa nyerere Leo viwe chini ya mjamaa tu wengi wao Wala hata hawaishi nchini!!

Yaani hatujifunzi tu kutokana na makosa, sasahivi umeme umeanza kukatika katika hovyo tu na biashara za vijana mnajua zinategemea umeme,!!

Kuna maeneo unaamhiwa umeme unakatika mara 5 kwa siku Sasa najiuliza Yale majamaa yakiingia Tena tunapona ? Wakati yanaingia na mikakati ya kuagiza makotena ya Generator?

Vijana waliojiajiri na masaloon waliomaliza vyuo wanaishije!! Tuiombee tanesco na Nchi.


That is the fact. Nashangaa mgao umerudi kwa kasi. Tuone aibu kuendelea kuizika Tanesco. Chande Maharage ana kazi kubwa sana ndugu yangu yule. Kivule tutarudi salama kweli? Watanzania wakituchukia ni tatizo
 
Nasema hivi,kwa uelewa wangu hii nchi kuna genge kubwa na la hatari Sana lenye nguvu kubwa kuliko Serikali tunayoijua.Ndilo linaloyumbisha na kufukarisha nchi.Ni mfano wa MAFIA au YAKUZA.Kiongozi pekee aliyethubutu kulishughulikia genge hili na kufanikiwa kwa kiwango kikubwa ni Hayati JPM.Sasa hayupo tena mwenye jeuri hiyo.Wameshika hatamu kwa kasi ya tsunami.Tutarajie maumivu maradufu huko tuendako maana genge hili limepenya kila mahali.

Sent from my M100 using JamiiForums mobile app
 
Hao mafisadi wafe tu, kama Mwenye Enzi Mungu anavyo taka maana kachoka na mafisadi uchwara walahi
 
On the other side of the coin private sector imeonyesha efficiency ya hali ya juu. Jiulize tungekuwaje kama TTCL ingeendelea na ile monopoly. By mwaka 1993 kabla Tigo hawaja connect mteja wa kwanza, TTTCL ilikuwa na landline subscrbers kama 105,000 tu.

Leo hii hawa mobile operators wana connect zaidi ya Watanzania 26 Milioni. Ngoja tuwape benefit of doubts
Private sector ilifeli kwenye ATCL Ikafeli kwenye TRC,lakini wacha tuone
 
Back
Top Bottom