TANESCO kufanya matengenezo ya Mfumo wa LUKU, huduma haitopatikana kuanzia saa 4 usiku hadi saa 1 asubuhi Sept. 12-15

BARD AI

JF-Expert Member
Joined
Jul 24, 2018
Posts
3,591
Reaction score
8,826
Shirika la Umeme Tanzania limetangaza kufanya matengenezo hayo kwenye Kanzi Data ya Mfumo wa manunuzi ya Umeme (LUKU) ili kuongeza ufanisi.


Matengenezo hayo yatachukua siku 4 kuanzia Jumatatu Septemba 12 hadi 15, 2022 na wateja wataweza kununua Umeme muda wote isipokuwa kuanzia saa 4 usiku hadi saa 1 asubuhi.

Shirika limeshauri wateja kununua Umeme wa ziada au kufanya manunuzi nje ya muda wa matengenezo ili kuepusha kukosa huduma.
 
Wafanye na task force kuwahudumia wateja wapya wanaohutaji huduma bila mizengwe na mizungusho🤔
 
Wafanye na task force kuwahudumia wateja wapya wanaohutaji huduma bila mizengwe na mizungusho🤔
 
Majenereta na solar power zilikosa wateja kwa muda mrefu. Acha wafidie hasara!😀
Wenzetu unafidiaje🤸🏿‍♀️🤸🏿‍♀️🤸🏿‍♀️🤸🏿‍♀️🤸
 
Hawa mafala hii ndiyo michezo Yao wanataka tununue umeme Kwa fujo ili watupige
Hawa wezi Wana mbinu nyingi sana za kutuibia pesa zetu, makamba ni tapeli Sana aisee anajua watakusanya hela nyingi
 
Mbona hawajasema luku hazitafanya kazi? Hapo wanazungumzia manunuzi ya luku kutoweza kufanyika kwa muda waliotaja....

Binafsi sijaona lolote. Tuchape kazi
Kwa hiyo manunuzi ya luku kutowezekana ndiyo luku zitaendelea kufanya kazi?!
 
Siku nne mnatengeneza nini
Acheni hizo
Wekeni umeme tusisumbuane
Mnatuchosha mtatupumzisha lini khe!
 
Leo tarehe 24 ila bado matengenezo yanaendelea!!!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…