Tetesi: TANESCO 'kwazizima' Makamba kuhamishwa Nishati. Waendelea na 'mfungo'

VUTA-NKUVUTE

JF-Expert Member
Joined
Nov 25, 2010
Posts
6,137
Reaction score
17,908
Katika hali ya kustaajabisha, maafisa na wafanyakazi wa kawaida wa Kampuni ya Umeme Tanzania (TANESCO) walirukaruka kwa furaha baada ya kusikia na kujua uhamisho wa aliyekuwa Waziri wa Nishati Januari Makamba. Maafisa na watumishi hao wa Makao Makuu ya TANESCO walionesha furaha yao ya wazi kwakuwa walikuwa 'hawamtaki' Waziri Januari Makamba.

Wana-TANESCO wanashukuru na kumkaribisha Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati Daktari Doto Biteko na kujiapiza kufanya naye kazi vyema. Hatahivyo, watumishi hao wamedai kuwa wanaendelea na maombi na mfungo wao ili Mungu amuongoze Rais Samia kumuondoa Mkurugenzi Mtendaji wa TANESCO Maharage Chande.

Makamba na Chande ambao ni marafiki wa karibu wa muda mrefu walikuwa hawakubaliki na wafanyakazi wa TANESCO kwa kile kinachosemwa kuwa wana kiburi, dharau na waligusa na kuondoa haki mbalimbali za wafanyakazi zikiwamo kufutwa kwa safari za kikazi. Nyaraka za ki-TANESCO zinaonesha kuwa kuna safari nyingi-hata zile zenye umuhimu ambazo zimefutwa na Chande kwa maelekezo ya Makamba.

Maombi ya wana-TANESCO yatafanikiwa?

Mzee Tupatupa wa Lumumba, Dar es Salaam
 

Kama sababu ni kufutwa kwa safari basi wenyewe ndio tatizo
 
Acha waendelee kuumia hao wapuuzi wanawavumilia kwa muda wote huo si ujinga
 
Kwahiyo safari ni haki ya mfanyakazi??
 
Tatizo ni hao wafanyakazi
 
Leta video acha umbea mtoto wa kiume
 
Bila shaka na wewe u miongoni mwa Wafanyakazi wa TANESCO, au siyo ndugu VUTA-NKUVUTE?

Na wewe uko kwenye mfungo? Unashangilia?
 
Kwa hali hii nahisi kuwa baada ya uchaguzi mkuu wa 2030 kuna watu watahama nchi,,

Hii system sioni ni kwa namna gani itashindwa kufanikisha jambo lao,,

Kipara pamoja na spana zote anazopigwa lakini kaweka pamba masikioni na anasonga mbele,,

Tuombe tu asipate roho ya visasi,,
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…